Rais Kikwete awasili Maputo kwenye sherehe za kuapishwa Rais mpya wa nchi hiyo.

                                          Taarifa kwa vyombo vya habari
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewasili Maputo, mji mkuu wa Mozambique, usiku wa Jumatano, Januari 14, 2015, kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais mpya wa nchi hiyo, Mheshimiwa Filipe Jacinto Nyusi. 
Sherehe zinafanyika Independence Square, mjini Maputo leo, Alhamisi, Januari 15, 2015. Mheshimiwa Nyusi anakuwa Rais wa nne wa Mozambique tokea uhuru wa nchi hiyo mwaka 1975.
 
Kiongozi mwingine mkuu wa Tanzania aliyealikwa kuhudhuria sherehe hizo ni Rais wa Tatu wa Tanzania, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa, ambaye amewasili akifuatana  na mkewe, Mama Anna Mkapa.
 
Ujumbe wa Tanzania kwenye sherehe hizo ni pamoja na Mama Salma Kikwete, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Mheshimiwa Mahadhi J. Maalim,  Mheshimiwa Mohamed Abood Mohamed ambaye ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Philip Mangula ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa CCM,  Mheshimiwa John Magale Shibuda ambaye ni Mbunge wa CHADEMA na Mheshimiwa Halima Dendegu ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
15 Januari,2015
 
 
Powered by Blogger.