Daftari la Wapiga kura: Chadema kuchukua maamuzi magumu


Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene. Picha Na Immanuel Herman
Dar Es Salaam.Wakati Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) ikisisitiza kuwa ratiba ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura itaenda kama ilivyopangwa, kamati kuu ya chama cha Demokrasi na Maendeleo imesema itachukua maamuzi magumu endapo shughuli za uboreshaji huo zitachelewa na kuharibu mchakato wa kura ya maoni.
Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba alisema leo kuwa uboreshaji utaanza Februari 16 kama ilivyotangazwa awali na utamalizika kwa wakati ili kupisha ratiba ya kura ya maoni.
“Ratiba inazingatiwa, vifaa vitafika kwa wakati na kuanza kazi kwa wakati,” alisema Malaba.
Akizungumza wakati wa kikao cha dharura cha Kamati Kuu ya Chadema, Afisa Habari wa Chadema, Tumaini Makene amesema chama hicho kimeitisha kikao hicho ili kujadili hatma ya uboreshaji wa daftari hilo na muda uliobaki kabla ya kupiga kura ya maoni Aprili 30, mwaka huu.
Pia Chadema walisema kuwa watachukua hatua zaidi iwapo mashine za Biometric Voters Registration(BVR) zitabainika kuwa na kasoro katika uboreshaji huo.
Zoezi la kuandikisha Watanzania milioni 26 wenye sifa ya kupiga kura lilitakiwa kuanza mwezi huu lakini Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imesema zoezi hilo litaanza Februari 16, mwaka huu kwa sababu bado inasubiri mashine 7,750 za (BVR) kwa ajili ya kazi hiyo.
 “Kwa mazingira ya kawaida muda uliobaki kwa ajili ya kazi hiyo kubwa hautoshi ndiyo maana kuitishwa kwa kikao cha dharura ili kufanya uamuzi,”alisema Makene-
Powered by Blogger.