Maji ya mvua kero kwa baadhi ya wakazi Mtwara



Maji ya mvua kero kwa baadhi ya wakazi Mtwara
Wakazi wa manispaa ya mtwara mikindani wameiomba manispaa  kuharakisha ujenzi wa mtaro wa kukusanya maji ya mvua  na kuyamwaga baharini wenye lengo la kupunguza tatizo la mafuriko katika baadhi ya maeneo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi wa mtaa wa kiangu kata ya shangani wamesema ujenzi huo kwa sasa umechangia njia za maji kuzibwa na hivyo kuleta usumbufu kwa mvua zilizoanza sasa.
 
Akizungumzia hali hiyo mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa kiangu chadema -ALLY MAKANJILA amesema eneo lake linatatizo la kujaa maji lakini mtaro huo umechangia nyumba nyingi kupata mafuriko kutokana na mtaro huo kujaa maji na kuzagaa katika majumba ya watu.
 
Kufuatia hali hiyo ameiomba manispaa kuharakisha ujenzi huo ili wakazi wake waondokane na adha hiyo vinginevyo hali itakuwa mbaya kulingana na mvua za masika ndiyo kwanza zimeanza.
 
Powered by Blogger.