Ufundi nao kukopeshwa

Arusha. Serikali imeahidi kuangalia utaratibu wa kuanzisha mfumo wa kugharimia elimu ya ufundi nchini ili kuwawezesha wanafunzi kupata mikopo kama wa elimu ya juu. Lengo likiwa ni kuwapata wataalamu wa kutosha katika viwanda na sekta nyingine.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenista Mhagama alitoa kauli hiyo juzi wakati wa kuwatunuku vyeti wahitimu wa ngazi mbalimbali katika mahafali ya Sita ya Chuo cha Ufundi Arusha (ATC). Alisema Serikali inatambua jitihada zinazofanywa na chuo hicho za kupanua udahili ili kuziba pengo la uhaba wa mafundi sanifu uliopo nchini.
Katika mahafali hayo, wahitimu wa kwanza katika fani ya uhandisi wa umeme na vifaatiba walitunukiwa stashahada zao. Naibu Waziri huyo alisema wataalamu hao watasaidia kutengeneza vifaatiba katika hospitali jambo litakaloongeza ubora wa huduma za afya na ajira.
Mkuu wa Chuo hicho, Dk Richard Masika aliomba kuendelea kutolewa kwa Sh10 milioni kwa wanafunzi bora 10 katika masomo yao. ya mwisho ili kuongeza ushindani katika masomo ya sayansi na ufundi hapa nchini.
Powered by Blogger.