MASWALI NA MJIBU YA NECTA



Mwandishi           ; Mwl GODLOVE J GWIVAHA
ENEO LA KAZI; SHULE YA SEKONDARY TEGETA
 MWAKA            ;2015

1.Kwa kutumia mifano, thibitisha ubantu wa Kiswahili kwa hoja madhubuti (nect 2010 swali la 10)
KISWAHILI NI KIBANTU
Nadharia hii hutumia ushahidi wa kiisimu na kihistoria katika kuchunguza lugha ya Kiswahili katika mfumo mzima wa historia ya mgawanyiko wa kusambaa kwa lugha za kibantu. Nadhalia hii huitimisha kuwa Kiswahili ni mojawapo ya lugha katika jamii kubwa ya lugha ya wabantu.
Wataalamu wa nadharia hii ni kama vile makon Guthrie, meinhof c na rohlc.
Malcon Guthrie amethibitisha kuwa Kiswahili kilikuwepo kabla ya wageni na kimeonyesha kuwa Kiswahili kina   uhusiano mkubwa na lugha za kibantu. Mwisho amehitimisha kwa kusema Kiswahili kimeanza Pwani ya afrika mashariki.
Mein holf  na Rolh wao wanaamini kuwa wakati wa utawala wa washirazi katika upwa wa afrika mashariki kulikuwa na kabila la waswahili ambalo ni dhulia la wazaramo wa leo. Wazalamo walizaliwa katika harakati za biashara hivyo wakafuata nyayo za wazazi wao na lugha yao ilikuwa kibantu na kwa kuwa wabantu ni wengi zaidi lugha yao ikaanza kutumika na kuenea katika makabila mengine. Kutokana na waswahili kufanya biashara na waarabu, washirazi, wamalaysia, wahindi na wareno vifaa na majina ya vitu vya biashara vya wageni hao vikaenea na kuingizwa katika mfumo wa lugha hiyo ya kibantu.
Nadharsia hii imekubalika kuwa ndio sahihi juu ya asili ya Kiswahili kwa kuzingatia ushahidi wake wa kiisima na kihistoria.
USHAHIDI  WA KIHISTORIA
Ushahidi wa kihistoria unathibitisha kuwa lugha ya kiswahili ilizungumzwakatika upwa au pwani ya afrika mashariki hata kabla ya ujio wa wageni kama vile waarabu, na wazungu.Ushahidi huu ulitolewa na wageni mbalimbali waliofika hapa afrika mashariki.wote wamehitimisha kwa kusema kuwa lugha ya Kiswahili ilizungumzwa hapa afrika mashariki hata kabla ya ujio wa wageni.
A.UGUNDUZI WA AL-IDRIS (1100-1166)
Ugunduzi huu ulifanyika huko sicily mnamo mwaka 1100-1166kwenye mahakama ya mfalme Roger , Al-idris alikuwa wa kwanza kugundua kuwa jina la kwanza la zamani la Zanzibar kuwa ni unguja. katika maelezo yake aliandika baadhi ya majina kama kikombe, mkono wa tembo,muriani na sukari ambayo ni majina ya ndizi mbalimbali zilizokuwa zikipatikana Zanzibar.
B.USHAHIDI WA MARCO POLO
Huyu ni mzungu ambaye alijishughulisha sana na maswala mbalimbali ya kijografia na alisafi sehemu nyingi duniani Marco polo aliandika hivi:
“Zanzibar ni kisiwa kizuri ambacho kina ukubwa na mzunguko wa maili 200. Watu wote wanaabudu (Mungu).Wana mfalme na wanatumia lugha yao, na hawalipi kodi (ushuru) kwa mtu.
Safari ya Marco polo
Aliandika kitabu cha kijografia ambacho kinasemekana kuwa hakikupata kuchapishwa lakini sehemu zake zimepatwa kufanisiwa kwa kirusi na kifaransa. Katika lugha ya Kiswahili ni kama ifuatavyo:
Katika visiwa vya Djawaga vilivyoshughulikiwa katika sura hii ni kile cha Andjaba ambacho mji wake mkuu unaitwa katika lugha ya kwao-zanzibar –ungudya na wakazi wake.
Japokuwa ni mchanganyiko kwa sasa wengi wao ni waislam chakula chao kikuu kikiwa ndizi, kuna aina tano ambazo zilijulikana kama kundi, fili ambao uzito wake waweza kuwa wakia 12, omani, mariyani, sukari.
Maelezo haya ya Marco polo yalithibitisha mambo ya msingi kuhusu wakazi wa pwani ya afrika mashariki na lugha yao.
C.USHAHIDI WA AL- MASUDI (915, BK)
Katika moja ya maandiko yake Al-masudi anazungumza juu ya wakazi wa mwambao ambao wanajulikana kwa jina la “Wazanji” kwa dhana hii neno Zanzibar linalotokana na neno “zanjibar” yaani pwani ya “Zenji” katika maelezo yake Al-masudi anaonyesha kuwa wazenji walikuwa na watawala, wakilimi ambao waliaminiwa kuwa walitawala kwa nguvu za Mungu.Kuna maelezo kuwa  huanda neno wakilima lina maana ya wafalme.Al-masudi alisisitiza katika maelezo yake kuwa wazenji wasema lugha yao kwa ufasaha na walikuwa na viongozi waliohutubia kwa lugha yao, kutokana na neno Zenji kuna uwezekano kuwa kabla ya maajilio ya waarabu, Kiswahili kiliitwa “Kiazania” au Kizenji na wageni waliofika pwani ya afrika mashariki.
D. HISTORIA YA KILWA,Kimsingi habari zinaeleza historia ya kilwa karne 10-16 B.K na zinahusisha na kutajwa majina ya utani kama mkoma watu, nguo nyingi” nk ambao walipewa masltani wa kwanza wa kilwa Ali Ibnhussein na mwanae Mohamed Ibn Ali.Kutokana na habari hizi huenda lugha ya Kiswahili ilishaanzwa kusema mnamo karne ya 10 au ya 11 B.K. Maelezo juu ya sultani aliyeitwa Talt Ibn Al Hasani ambaye alipewa jina la utani “Hasha Hazifiki” nayo pia yalitolewa.
      E.USHAIRI WA KISWAHILI
A.    utenzi wa tambuka (karne ya 18 b.k)
Utenzi huuuliandikwa mnamo karne ya 18 kuanzia mwaka 1700 na kuendelea (tarehe kamili haijulikani). Utenzi huu umeandikwa kwa kutumia lugha (lahaja ya kimvita )ambayo ni moja ya lahaja za lugha ya Kiswahili.


B.Utenzi wa fumo liyongo
Shairi hili linasemekana liliandikwa karne 13 B.K. kuwepo kwa shairi hili kunadhihirisha uwepo wa lugha ya Kiswahili kabla ya hapo. Huenda kilianza kutumika kabla ya karne ya 10 B.K. baadhi ya beti za utenzi wa fumo liyongo ni hizi zifuatazo:
Ubeti 6      Liyongo  kitamkali
Akabalighi vijali
Akawa mtu wa kweli
Na hiba huongeya
Ubeti 7        Kilimo kama mtukufu
Mpana sana mrefu
Majimboni yu maarufu
Watu huja kwangaliya
Ubeti  10     Sultani pate Bwana
Papo nne akanena
Wagala mumemwona
Liyongo kiwatokeya
Lgha hii ni mfano wa lugha iliyokuwa ikitumika mnamo karne ya 13 BK.ni wazi kuwa lugha hiyo ilianzwa kusemwa mapema kabla ya muda huo.
F.Vitabu vya peryplus na yu-yang-tsa-tsu,Kitabu cha perplus kinahusu mwongozo wa Bahari ya Hindi. Inasemekana kiliandikwa karne ya kwanza huko Alexandria.kitabu hiki kinataja habari za Tanzania (afrika mashariki) na habari za vyombo kama nyalawa, madema, mitepe. Kinaeleza kuwa watu wageni hutozwa ushuru na wafanyabiashara wenyeji, wanaijua pia lugha ya wenyeji wao.
          Kitabu cha Yu-yang Tsa Tsu kinaeleza habari za upwa wa afrika mashariki na shughuli mbalimbali za wachina hapa afrika mashariki
    Kitabu kingine kiliitwa Chu fan chi kilichochapishwa 1226 kinaelezea habari za Zanzibar na biashara, vyakula, dini, na wanyama wa pwani ya afrika mashariki.
G.Ushahidi wa ibn batuta karne ya 14 bk,Mohamed bin Abdallah Ibn Batuta ana asili ya taifa la kiarabu. Alikika upwa wa afrika mashariki mnamo  mwaka 1331BK.katika maandishi yake anaeleza juu ya maisha ya watu wan chi hii ya afrika mashariki ingawa yeye aliita nchi ya waswahili. Anataja miji kama vile Mogadishu, na kilwa.anadai kuwa;
Basi nilianza safari baharini  kutoka Mogadishu  kwend nchi ya ya waswahili na nchi ya kilwa ambao umo ndani ya nchi ya Zanji. Tulipofika Mombasa kisiwa kikubwa, mwendo wa siku mbili kutoka nchi ya waswahili…………….watu hawajishughulishi na kilimo, ingawa huagiza nafaka kutoka kwa waswahili”
   Maelezo haya yanahusu eneo au mahali ambayo waswahili walikuwa wakiishi na inaonyesha kuwa watu hawa walikuwa wakiishi katika upwa au pwani wa afrika masharikikuanzia sehemu za bara upande wa kaskazini hadi msumbiji na bukini kwa upande wa kusini.
H.Maandishi ya Morice (karne ya 18 bk),Maandishi haya yalijitokeza mwaka 1776.katika maandishi yake morice  amewagawa wakazi wa afrika mashariki katika makundi matatu yaani masuriyama,waarabu na Waafrika.Anaendelea kusisitiza kuwa Masuriyama na wafrika walisha kaa na kuungana kama jumuia moja wakaelewana na kusema lugha moja ya kisuriyama.Kuna wazo kuwa huenda  kisuriyama ndicho Kiswahili cha leo.
USHAHIDI WA KIISIMU
Isimu ni nini?
Isimu ni sayansi au taaluma inayoiangalia lugha kwa undani(kisayansi) kwa kuzungukia tanzu kama vile;isimu jamii,isim historia,isimu linganishi,isimu matumizi,isimu nafsia na isimu fafanuzi.Ushahidi wa kiisimu ni ushahidiunaothibitisha kwa kutumia misingi inayohusu sayansi ya lugha.
Lugha ya Kiswahili ilifanyiwa utafiti na wataalamu kadhaa kwa lengo la kuainisha kama ina misingi ya kibantu.
Malcon Guthrie kutoka chuo kikuu London Uingereza alitumia miaka 20 kuchunguza uhusiano uliopo baina ya  lugha za kibantu ziliko katika eneo lote ambalo hukaliwa  na wabantu  yaani kusini mwa jangwa la sahara.
Alifanya Uchanganuzi wa mashina au mzizi(viini) ya maneno 22000 kutoka lugha 200 za kibantu .Kibantu Uchunguzi wake alikuta mzizi (mashina)2300 imezagaa katika lugha mbalilmbali za kibantu na kiswahli kikiwezo.Mashina au mizizi 500 yalilingana katika lugha zote 200.Mashina haya yalipatikana  katika lugha zote za kibantu.Mashina haya yalikuwa ya asili moja.Baadhi ya lugha hizo 200 zilizofanyiwa uchunguzi,lugha ya Kiswahili ilionesha kuwa na ulinganifu sawa na kikongo(44 asilimia)
Katika kuchunguza  ni asilimia ngapi za mashina hayo 500 yamo katika kila lugha ilionekana mgawa ufuatao;
Kiwemba kizunguzwacho Zambia 54%
Kiluba   kizungumzwacho Katanga 51%
Kikongo  kizungumzwacho 44%
Kiswahili kizungumzwacho Afrika Mashariki  44%
Kisukuma  kizungumzwacho Tanzania  41%
Kiyao kizungumzwacho  Tanzania/Msumbiji 35%
Sotho kizungumzwacho Botwana  20%
Rundi kizungumzwacho Burundi  43%
Kinyoro kizungumzwacho  Uganda  37%
Zulu kizungumzwacho Afrika kusini  29%
Matokeo ya utafiti huu yanathibitisha  kuwa;
                                                              i.            Mashina mengi ya lugha za kibantu yapo afrika ya kati hasa  sehemu zinazozungumkia mkoa wa Katanga huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kupungua kadri unavyoelekea mbali nako. Hivyo ni dhahiri kuwa wabantu walienea kutoka sehemu hizo na kuja sehemu mbalimbali zikiwemo zile za afrika mashariki.
                                                            ii.            Kufuatana na matokeo ya utafiti hua ni wazi kuwa, lugha ya Kiswahili ni kibantu kama madai yake ya kusema Kiswahili madai yake ni kiarabu yangekua sahihi basi lugha hiyo ingehusiana mno na kiarabu.
1.      MSAMIATI,Msamiati ni msingi wa lugha ya Kiswahili na kibantu unafanana kabisa. Msamiati wa msingi ni ule unaohusu ambayo hayabadiliki badiliki kutokana na mabadiliko ya utamaduni tofauti zinaweza kujitokeza katika matamshi au mabadiliko kidogo ya viambishi, kakini si katika mzizi.
Mfano;
Kiswahili     kindali              kizigua              kijita         kikurya
Mtu           umundu      mritu         omontu       omonto
Maji           amishi        manzi          amanji       amanche
Moto           umlilo        moto            omulilo       omoro
2.      Tungo (sentensi) za Kiswahili ,miundo ya tungo (sentensi) za maneno ya Kiswahili zinafanana sana miundo ya tungo za maneno ya kibantu. Sentensi za kiswahili na lugha za kibantu zina kiima na kiarifu.
Mfano  Kiswahili – Juma/ anakula ugali
                                   K           A
           Kizigua – Juma/ adya ugali
                          K         A
        Kisukuma – Juma/ alelya bugali
                             K           A
           Kindali – Juma /akulya ubhugli
                               K     A
           
               Kijita –Juma/ kaiya ubusima.
                               K        A
   3.Ngeli za majina,Hapo kuna makubaliano kufuatana na ngeli katika mambo ya nomino (umoja na wingi wa majina) pamoja na kisarufi.
                          i.            Kigezo cha maumbo ya majina
Kigezo hiki hufuata mambo ya umoja na wingi katika kuyaainisha majina. Majina yaliyo mengi katika lugha ya Kiswahili na lugha za kibantu hufuata mkondo wa umoja na wingi. Majina ya lugha ya Kiswahili na lugha za kibantu yaliyomengi yana maumbo dhahiri ya umoja na wingi.
Mfano            Umoja                                                      wingi
              Kiswahili           Mtu                                                        Watu
             Mtoto                                                      Watoto
             Kikrya               Omonto                                                   Banto(abanto)
                                    Omona                                                    Baria (abana)
          Kizigua              Mntu                                                       Bhantu
        Mwana                                                     Bhana
       Kindali              Mundu                                                     Bhandu
     Mwana                                                      Bhana
                        ii.            Kigezo cha upatanisho wa kisarufi
Katika kigezo hiki tunaangalia uhusiano uliopo kati ya nomino na kivumishi na viambishi vya awali vya nafsi katika vitenzi vya Kiswahili na kibantu.vivumishi majina pamoja na vitenzi hivyo hubadilika kutokana na maumbo ya umoja na wingi.
Mfano
                             Umoja                                         wingi
Kiswahili             Baba analima                          Baba wanalima
Kindali                Utata akulim                            Abhatata Bhakulima
Kikury                  Tata anarema                           Batata abalima
Kijita                    Tata kalmia                               Batata abalima
3.      Vitenzi vya kiswahili na kibantu,Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya vitenzi vya Kiswahili na vile vya kibantu. Vipengele vinavyothibitisha uhusiano  huu ni viambishi, mnyambuliko pamoja na mwanzo/mwisho wa vitenzi.
a.      Viambishi
Lugha ya Kiswahili na lugha za kibantu vitenzi vyake hujengwa na mzizi (kiima) pamoja na viambishi  vyake (awali na tamati)
Mfano
Kiswahil – analima – a-na-lim-a
                                  1  2   3   4
Kikurya – ararema – a-ra-rem-a
                                  1  2   3    4
Kindali- akulima – a – ku – li – ma
                               1     2    3    4
ü  Kiambishi awali kipatanishi cha nafsi.
ü  Kiambishi awali cha njeo.(wakati uliopo)
ü  Mzizi /kiima
ü  Kiambishi tamati
b.      Mnyambuliko wa kitenzi (uambishaji)
Mnyambuliko ni kitendo cha kuunda neno jipya kwa kuunganisha viambishi kwenye mzizi wa shina au neno mnyambuliko wa vitenzi vya Kiswahili hufanana na ule wa vitenzi vya lugha ya kibantu.
Mfano
Kiswahili – kucheka – kuchekesha – kuchekelea
Kindali – kuseka – kusekasha – kusekelela
Kibena – kuheka – kuhekesha – kuhekelela
Kinyamwezi – kuseka – kusekasha – kusekelela
Kikagulu – kuseka – kusekesha – kusekelela
c.       Mwanzo wa vitenzi
Vitenzi vyote vya Kiswahili na vile vya lugha za kibantu huanza na viambishi ambavyo ni viwakilishi vya nafsi:
Mfano
Kiswahili - Ninakwenda
            Kihaya – Ningenda
            Kiyao - Ngwenda
d.      Mwisho wa kitenzi
Vitenzi vya lugha za kibantu huishia na Irabu  a
Mfano
Kiswahili – kukimbia – kuwinda – kushuka.
Kindali - kukinda – kubhinga – kukola
Kisukuma - kwihuka - kuhiga – kisinga
2.Mofimu –u- yaweza kuwa na dhima mbalimbali ukitunga  sentensi kwa kila dhima,Onesha dhima tano (5).Pigia mstari mofimu –U- ili kubainidhima hiyo.(Mock 2014-Dar swali la 4)
(A) Inaweza kuwa mzizi wa neno
Mfano: Amemu-u-a
(B)Inaweza kutaja ngeli ya U-I,U-YA,U-ZI/Idadi
Mfano;Mti  U-mekatwa
(c) Inaweza kutaja nafsi ya pili umoja
Mfano; U-liondoka
(D) Inaweza kutaja kauli ya kutenda
Mfano; Fung-u-a
(E) Inaweza kusimama kama kitenzi shirikishi
Mfano;Wewe u- mgonjwa
DHANA NYINGINE
(A) “ NA”
i.                    Hutumika kama kiunganishi
Mfano Juma na Priska wanaimba
ii.                  Hutumika kama kiambishi cha nafsi ya kwanza
Mfano Naomba aje mwenyewe
iii.                Hutumika kama kihusishi
Mfano Amekaa mbali na maadui
iv.                Hutumika kama kiambishi cha njeo ya wakati uliopo
Mfano Elicia anaimba.
v.                  Hutumika kama kauli
Mfano Nani?
vi.                Hutumika kuunda mzizi wa kitenzi
Mfano Yeye anataka
vii.              Hutumika kuonyesha mtazamo wa msingi wa jambo
Mfano Na aje sasa.

TUMIA KIAMBISHI “KA” KUONYESHA MATUKIO KUMI (10)
(NECTA 2011 SWALI LA 3)
                          i.            Hutumika katika vitenzi vya kutoa amri,ari,au ombi
Mfano Nenda kamwite (amri)
Kafanye kazi yake   (ombi)
                        ii.            Hutumika katika kuonyesha wakati katika mtindo wa kukubali
Mfano Wakapanda
Mkapanda
                      iii.            Hutumika kama alama ya wakati na kuonyesha masimulizi ya matukio yaliyopita
Mfano Kati ya mwaka na mwaka
                      iv.            Hutumika kuonyesha matukio ya mfululizo
Mfano Nataka kusafiri niende mbali nikatafute.
                        v.            Hutumika katika vitenzi kuonesha hali  au kusudis
Mfano Naomba fedha nikanunue nguo
(B)  MATUMIZI YA “KI”

                          i.            Hutumika kuonyesha masharti
Mfano. Akija nitakupigia
                        ii.            Ngeli ya 4 (ki-vi)
Mfano. Kisu kimepotea
Visu vimepotea
                      iii.            Hutumika kuonyesha upungufu wa viungo katika mwili
Mfano. Kipofu,kiziwi, kibogoyo.
                      iv.            Hutumika kuonyesha uduni (kudunisha, udogo)
Mfano. Kizee kile kina mambo ya ujana
Kijana Yule ana mambo ya kizee
                        v.            Hutumika kufananisha
Mfano. Anaishi kikristo kweli kweli
                      vi.            Hutumika kuonyesha lugha mbalimbali
Mfano Kiswahili, kingereza
UKITUMIA MFANO WA SENTENSI KATIKA KILA TUMIZI ONYESHA MATUMIZI MATANO YA KIUNGANISHI “KWA”
(NECTA 2006 SWALI LA 8)
AU
KWAKUTOA MIFANO, TAJA MATUMIZI MATANO TOFAUTI YA KIUNGANISHI “KWA” (NECTA 2010 SWALI LA 5)

        i.      Hutumika kama kiunganishi
Mfano. Walikusanyika wazee kwa watoto.
      ii.      Hutumika kama kielezi cha mahali
Mfano. Juma alikwenda kwa rafiki yake
    iii.      Hutumika kama kisababishi
Mfano. Watu wengi hufa kwa ugonjwa wa Ukimwi
    iv.      Hitumika kama kielezi cha jinsi (namna)
Mfano. Atatembea kwa maringo
      v.      Hutumika kama kilingnishi
Mfano Simba ilifungwa magoli sita kwa mbili.
    vi.      Huonyesha hali ya kutakiana heri.
Mfano. Kwa heri
  vii.      Hutumika kuuliza
Mfano. Kwa nini?
viii.      Hutumika kufananisha jambo
Mfano. Kwa tabia anafanana na mama yake
    ix.      Hutumika katika nahau au misemo
Mfano. Sisi kwa sisi
Uso kwa uso
Jino kwa jino
KWA KUTUMIA LUGHA ONYESHA KAZI TANO (5) ZA MOFIMU “KU”
(NECT 2007 SWALI LA 5)
        i.      Kiambishi cha awali cha njeo ya wakati uliopita
Mfano. Mwandishi hakuandika ubaoni
      ii.      Kunominisha
Kufeli kunachukiza
    iii.      Kuonyesha mtendwa nafsi ya pili umoja
Nimekuona
    iv.      Kuonyesha mahali
Kule ni kuzuri
v.  Kuunda mzizi wa kitenzi
Kumbuka,kuna
vi.Kuonyesha mtendwa nafsi ya pili umoja
Nimekuona
vii.Kuonyesha wakati/njeo
Kufika kwetu

(C) MATUMIZI YA “N”
i.Hutumika kuonyesha nafsi ya kwanza umoja
Mfano Ninaimba, nimeolewa
ii.Hutumika kama urejeshi wa mtendwa
Mfano wameniuzi, wamenipiga
iii.Hutumika kama mzizi wa neno kiulizi
Mfano Nani,nini, lini ?
iv.Hutumika kushirikisha vitenzi katika sentensi
Mfano wewe ni mpole
(G)MATUMIZI YA “M”
(i)Hutumika kuonyesha nafsi ya pili wingi
Mfano ninaimba, mnastaajabu, mmeiba
ii.Hutumika kuonyesha idadi ya umoja
Mfano mti, mtu, mchezo
iii.Hutumika kuonyesha urejeshi wa mtendwa
Mfano Anavyomchezea, wanamsifu.
(H)MATUMIZI YA “JI”
i.Hutumika kuonyesha urejeshi wa mtenda jambo
Mfano anajiua
        i.      Hutumika kuonyesha kijenzi cha nomino
Mfano mwimbaji, mchezaji
      ii.      Hutumika kama mzizi wa neno
Mfano anakujia
3.Bainisha aina ya vivumishi katika sentensi
(Mock 2014 mkoa wa Dar, Swali 3 )
i.Mtoto wangu amechaguliwa jeshini
Wangu – Kivumishi kimilikishi
i.            Nani aliitisha mkutano huu?
Huu – kavumishi kionyeshi
ii.            Mtu wa chama atakuja leo
Wa chama – kivumishi
iii.            Yale matatu ya ache
Matatu – kivumishi cha idadi
iv.            Mwanafunzi mwenyewe ametoroka
Mwenyewe – kivumishi cha pekee

MOFIMU
Ni kipashio bkidogo chenye maana ya kisarufi au ya kileksika.Kipashio hicho kinaweza kuwa sehemu ya neno au neno zima.Mofimu zenye maana ya kileksika aghalabu huwa ni mofimu ambazo haziambatanishwi na kipashio kingine chochote.
Mfano; Baba,Mungu,Fikiri,Bora n.k
Mofimu zenye maana ya kisarufi ni mofimu zinazoambatanishwa na mofimu nyingine katika uundaji wa maneno.Mofimu hizo huwa n sehemu tu ya mmaneno yaambatanishwayo katika mzizi wa neno.
Mfano; A-na-lim-a
AINA ZA MOFIMU
 A.Mofimu huru
B.Mofimu tegemezi

 A.Mofimu huru,Ni neno/maneno yanayoweza kugawanyika katika vipande maana kisarufi.Ni maneno ambayo hatuwezi kuyavunjavunja katika vipande vidogovidogo na vyenye kuleta maana ya kisarufi. Agharabu ni maneno yasiyo na umoja kama vile Baba, Mama, Jana, Leo,StareheHuitwa mofimo huru kwa sababu ya maneno haya hujitoshereza.
B.Mofimu tegemezi,Hivi ni vipande vidogo kabisa vya neno vyenye maana kisarufi. Huitwa mofimu tegemezi kwa sababu vipande hivi vinategemeana ili kutoa maana kisarufi kipande kimoja cha neno hakiwezi kusimama peke yake na kutoa maana ya kisarufi mfano. Sikukuona
a. Si-ku-kuon-a
Si – mofimu awali kanushi nafsi ya kwanza.
Ku-mofim awali ya  nafsi ya pili
Kuon-mzizi wa neno
a— mofimu/kiambishi tamati
DHIMA ZA MOFIMU
Ni matumizi au kazi za vipashio katika vitenzi. Dhima nyingi hutokea katika vitenzi na dhima chache zinazoweza kujitokeza katika baadhi ya nomino kivumishi au kiwakilishi
i.                    Hudokeza idadi
Mfano,                  umoja                       wingi
Ninasoma                  tunasoma
Limevunjika               yamevunjika
Kiatu                       viatu
ii.Hudokeza hali ya ukanushi na uyakinishi
Mfano; Uyakinishi      Ukanushi
Nitaondoka      Sitaondoka
Utafaulu           Hutafaulu
iii.Hudokeza  hali ya Mazoea
Maana yake jambo hufanyika mara kwa mara
Mfano;Hula,Hucheza,Huimba.
iv.Hudokeza  nafsi zote tatu(3)
Nafsi huoneshwa katika vitenzi kwa kutumia vipashio mbalimbali.Takribani kila nafsi  ina kipashio chake.
Mfano;
(a)    Nafsi ya kwanza
Umoja             Wingi
Ninasoma       Tunasoma
Ananipiga       Wanatupiga
(b)   Nafsi ya pili
Umoja               Wingi
Unacheza               Mnacheza
Nilikufundisha       Tuliwafundisha
(c)    Nafsi ya tatu
Umoja               Wingi
Alimpiga          Waliwapiga
v.            Hudokeza  hali ya  Masharti
Hali ya masharti katika Tungo huwaklishwa na vipashio kama vile;
Ngali,ngeli,nge-,ki.
Mfano;
Angesoma kwa bidii angefaulu mtihani.
Akija nitamchinjia mbuzi
vi.            Hudokeza njeo(wakati)

(A) Wakati uliopita
Huoneshwa na vipashio “li” na  “ku” kipashio ‘li’ hudokeza wakati uliopita uyakinishi na ku- katika ukanushi.
Mfano.            Uyakinishi                  ukanushi
Alisoma                     hakusoma
Alikunywa                 hakunywa
Nilikuja                    sikuja
Alilia                         hakulia
(B)Wakati uliopita timilifu
Wakati uliopita timilifu maana yake ni si muda mrefu tangu jambo lifanyike na matokeo ya  kufanyika kwa jambo hilo bado yapo
Wakati uliopo timilifu huonyweshwa na vipashio me katika uyakinishi na ja katika ukanushi.
Mf.                       Uyakinishi               ukanushi
Nimekunywa              sijanywa
Nimekuja                         sijaja
Amekufa                            hajafa
C Wakati uliopo unaoendelea
Huu ni wakati unaonyesha tendo bado linaendelea na bado hatujui litakoma lini, wakati uliopo unaendelea  hudokez wa na vipashio Na, i, si
Kipashio na hutumika katika uyalimishi na vipashio ‘i’ na ‘si’ hutumika kwenye ukanushi ‘i’ hujitokeza mwishoni mwa kitenzi.
Mfano           Uyakinishi                  Ukanushi
Ninasoma                   sisomi
Ninacheza                  sichezi
D Wakati ujao maana yake bado jambo halikufanyika
Wakati ujao hudokezwa na kipashio
Mfano.        Uyakinishi               ukanushi
Atalima                   hatalima
Nitaondoka               sitaondoka
NB
Iwapo kitenzi cha wakati ujao kitakuwa na urejeshi (o-rejeshi) ndani kitapata kiambishi cha wakati ujao ka.
Mfano atakaye soma
Nitakapoondoka
vii.            Mofimu hudokeza hali ya urejeshi
Hivi ni viambishi au mofimu ambavyo hurejerea kutaja au kudokeza kitu, mtu au jambo ambalo linajulikana au lililokwaisha tajwa
Mfano                  Yaliyomwagika,
Waliotoroka
Aliyekamatwa
viii.            Mofimu hudokeza kauli mbalimbali
Kuna kauli nyingi katika vitenzi na kauli hizi nyingi hujitokeza mwishoni mwa kitenzi. Na kila kauli ina umbo yake linlosadifiana na kitenzi husika kilichomo katika kauli
Mfano
a. Kauli ya kutendwa
Mfano cheza, analima,anasali, anatubu.
Kiambishi tamati cha kauli cha kutenda huwa ni a,i,u hutegemea na asili ya neno.
b.Kauli ya kutendea
Kiambishi cha e au i hii inategemea asili ya mzizi
Mfano.                Anasomea – A-na-som-e-a
Tulipigia Tu-li-pig-i-a
c. Kauli ya kutendesha
Viambishi tamati vya kauli ya kutendeshani esh, ish
Mfano.                Chezesha chez-esh-a
Salisha Sal-ish-a
d.      Kauli ya kutendeshwa
Viambishi tamati vya kauli ya kutendeshwa ni eshw, ishw
Chezeshwa
Someshwa
Safishwa
ix.            Kauli ya kutendana
Kiambishi tamati cha kauli ya kutendeana ni an
Pigana
Chezeana
Imbana
x.            Kauli ya kutendwa Ni w
Mfano            Pigwa
Chezwa
xi.            Kauli ya kutendewa ni iw, liw, lew
Mfano.           Imbiwa
Somewa
Olewa
xii.            Kauli ya kutendeka
Viambishi vya kauli ya kutendeka ni ek, k, lik, lek
Mfano.            Pigika
Chezeka
Someka

6.Ni kipengele kipi kinachotumika kuunda ngeli za kimapokeo? Dhihirisha utumiaji wa kigezo hicho kwa kutunga sentensi (5) za ngeli tofauti.(nect 2010)
NGELI ZA MAJINA
Ngeli ni aina au namna ya kuweka majina katika makundi yanayofanana au yanayowiana
MIGAWANYO YA NGELI
Katika ngeli za nomino zimekuwa zikigawanywa kwa kuzingatia mitazamo mikuu miwili, mitazamo hiyo ni
i.  Mtazamo wa kimapokeo/Ngeli za kimapokeo
ii.Mtazamo wa kisasa/Ngeli za kisasa
MTAZAMO WA KIMAPOKEO
(NGELI ZA KIMAPOKEO) Kiimofolojia)
Hapa majina au nomino yalipangwa katika makundi yaliyofanana kwa kutegemea na maumbo yake.Ni hali ya kupanga majina katika makundi yanayofanana kwa kuoanisha viambishi awali vya majina hayo katika umoja na wingi.Mtazamo huu wa kimapokeo unaungwa mkono na Mein holf na ashton
Ngeli ya  1: M/WA
Katika ngeli hii majina yenye sifa zifuatazo yanaingia katika ngeli hii;
-Majina ya Viumbe vyenye uhai isipokuwa mimea.
Mzee –Wazee
Mtoto-Watoto
Mtu-Watu
Mwalimu-Waalimu
-Majina yanayotokana na Vitenzi yanayotaja watu
Mfano
Mfungaji-Wafungaji
Mchezaji-Wachezaji

Ngeli ya 2: M/MI
-Yanaingia majina ya mimea
Mti-miti
Mchungwa-Michungwa
Mpapai-Mipapai
-  Yanaingia ya vitu yanayoanza na M-
Mto -   mito
Msumari – misumari
Msumeno – misumeno
Mwiko – miiko nk.
-  Yanaingia majina ya matendo yanayoanza na M-
Mchezo – michezo
Mkato – mikato
Mtego – mitego

Ngeli ya 3: KI/VI
- Hapa yanaingia majina yanayoanza na Ki-(umoja) na Vi (uwingi)
Kiti – viti
Kisu – visu
Kikapu – vikapu
Kito – vito, nk.
-  Yanaingia majina ya vitu yanayoanza na ch- (umoja) na vy-(uwingi)
Chakula – vyakula
Chuma – vyuma
Chungu – vyungu
-  Yanaingia majina ya viumbe yaliyoambishwa Ki- ya kudumisha.
Kitoto – vitoto
Kizee – vizee
Kisichana – visichana
Kivulana – vivulana

Ngeli ya 4: N-
-Yanaingia majina ambayo huanza na N-inayofuata na konsonanti ch-,d-,g-,j-,-z-, -y- katika umoja na wingi
Nguo              njaa                     mvua
Nyama           mboga                   mvinyo
Nchi                ndizi
Mbuga             nyota, nk.
Yanaingia majina ya mkopo
Barua        taa          meza
Kalamu      redio, nk
Maumbo yote ya majina haya hayabadiliki kwa umoja na uwingi.
Ngeli ya 5: JI/MA
Yanaingia majina yanayoanza na Ji- (umoja) na Ma (uwingu)
Jiwe – mawe
Jicho – macho
Jina – majina n.k
Yanaingia majina ya sehemu za mwili na sehemu za mti.
Goti – magoti
Sikio – masikio
Ini – maini
Ua – maua
-  Yanaingia majina ya mikopo.
Bwana – mabwana
Shati – mashati
-  Majina yenye kueleza dhana ya uwingi japokuw hayahesabiki.
Maji      maisha  manukato
Mate      mafuta   mavi nk.

Ngeli ya 6: U/N
-  Yanaingia majina yanayoanza na U-(umoja)na N- au Mb- (uwingi).
Uso – nyuso
Uzi- nyuzi
Ubao – mbao

Ngeli ya 7: U/MA
Yanaingia majina yanayoanza na U-(Umoja) na Ma- (uwingi).
Uasi – maasi
Ugonjwa – magonjwa
Uchweo – machweo
Ununuzi – manunuzi

Ngeli ya 8: KU-
-  Yanaingia maneno yale yanayohusu vitenzi (Vitenzi jina).
Cheka – kucheka
Cheza – kucheza
Imba – kuimba

Ngeli ya 9: PA/MU/KU
Mahali  pale
Mahali  kule
Mahali  mule

Msingi wa kisintaksia/upatanisho w kisarufi.
Huu ni mtazamo wa kisasa unaogawa majina katika ngeli kwa kulingana na upashio wa kisarufi kati ya jina na viambishi awali vilivyo kwenye viamgishi. Kwa mujibu wa mtazamo huu, ngeli za majina ya Kiswahili ni tisa (9) kama ifuatavyo:-


Ngeli
Viambishi awalia vipatanishi.
Mifano
1.
A-WA
A-Umoja
WA-uwingi
Mtu anakuja – watu wanakuja
Mtoto analia – watoto wanalia
Mtoto anacheza – watoto wanacheza
2.
U-I
U-umoja
I-uwingi
Mti umeanguka -  miti imeanguka
Mto umekauka – mito imekauka
Mguu unauma - miguu inauma

3.
LI- YA
Li – umoja
Ya - uwingi
Jicho linaona – macho yanaona
Panga linakata – mapanga yanakata
Jicho linauma – macho yanauma
4.
KI - VI
Ki – umoja
Vi – uwingi
Kisu kinakata – visu vinakata
Kizee kimelala – vizee vimelala
Chakula kimechacha – vyakula cmechacha
5.
I – ZI
I – umoja
Zi – uwingi
Nguo imechakaa – nguo zimechakaa
Sahani imepasuka – sahani zimepasuka
Nchi inaliwa nchi zinaliwa
4.       
U -ZI
U – umoja
Zi – uwingi
Ukuta zimejengwa - kuta zimejengwa
Uzi umekatika – nyuzi zimekatika
Ubao umevunjika - mbao zimevunjika
7.
U – YA
U- umoja
Ya- uwingi
Ugonjwa umeenea - magonjwa yameeneo.
Uasi umeisha – maasi yameisha
8.
KU-
Ku – umoja
Kuimba kunachosha
Kucheza kunaburudisha
Kusoma kunachekesha
9.
PA-MU-KU
Pa – umoja
Mahali hapa pametuchosha
Mahali humu panafaa
Mahali huku kunapendeza.

7.Dini zisingefika Tanzania Kiswahili kisingekua na kuenea kwa haraka.Jadili kauli hii.(nectar 2004 swali la 1)
AU
Fafanua kwa hoja tano(5) madai kuwa dini zisingefika Tanzania,Kiswahili kisingekua na kuenea kwa haraka(Mock mkoa wa dar,2014 swali la 10)

Kuenea kwa lugha ni kuongezeka la watu wanaotumia lugha yenyewendani ya nchi.Ongezeko linakomaa kiasi cha kuvuka mipaka ya awali.

Wanaokubali
Ni kweli kabisa dini zisingefika Tanzania Kiswahili kisingekua na kuenea haraka kutokana na sababu za michango ifuatayo ya dini zote mbili yaani kiisilamu na kikristo.
Wamishenari,walifika  pwani ya Afrika mashariki kabla ya utawala wa wakoloni ,baadhi ya mashirika ya dini kama vile”Roho mtakatifu” White father yote kutoka Ufaransa pia Church Missionary Society(CMS) mambo waliofanya kukuza na kukieneza Kiswahili ni kama ifuatavyo;
Waliandika sarufi ya kwanza ya kiswahili ya kimvitakatika kitabu kilichoitwa “Outlines of the elements of Kiswahili language with reference to the kinika  dialects na walitafsiri injili ya luka na yohana kutoka kwenye lugha ya kiingereza kwenda lugha ya Kiswahili.
Walikiweka kiunguja katika maandishi Edward Steere alifanikiwa kuchapisha toleo la kwanza la sarufi ya Kiswahili cha kiunguja kitabu hicho kiliitwa “A handbook of Swahili Language as spoken at Zanzibar.
Walifanikiwa Kutoa kamusi mbalimbali za Kiswahili kwenda kiingereza na kiingereza kwenda kiswahili ambayo mwanzoni ilianzishwa na Edwrd steere na kumaliziwa na A.Madan.
Wamisheni walitumia Kiswahili katika kaziya kueneza dini yao huku wakitumia Kiswahili kama lugha ya mawasiliano hali hii ilipelekea Kiswahili kukua na kuenea kwa haraka.
Waislamu walifika pwani ya afrika mashariki wakakuta tayari wenyeji wana lugha zao za kibantu na Kiswahili kutokana na malengo yao ya kutaka kueneza dini ya kiislamu hivyo waliamua kutumia lugha ya Kiswahili katika mawaidha (mahubiri) hivyo walifanya Kiswahili kukua na kuenea zaidi.
Wamisheni walijenga vituo vyao vya dini katika maeneo mbalimbali ya Tanganyika kama vile Mpwapwa,Zanzibar,Bagamoyo, masasi n.k katika vituo hivyo Kiswahili kilitumika katika mawasiliano baina ya wamishenari na wenyeji hivyo kuchangia na kukua na kuenea haraka.
Pia Kiswahili kilitumika kufundishia elimu ya dini ya kiislamu (Madrasa) hivyo kukua na kuenea kwa lugha ya kiswahili pia kulichangiwa na mafundisho hayo.
Waarabu walijenga misikiti sehemu mbalimbali za Tanganyika kama vile Bagamoyo, Tabora, nk. Katika maeneo hayo ya vituo lugha iliyotumika ni Kiswahili hivyo kukua na kuenea haraka.
Wamisheni walijenga shule za msingi na sekondari (middle school) katika maeneo mbalimbali ya Tanganyika Kiswahili kilitumika kufundishia elimu ya shule ya msingi na sekondari walisoma kama somo la Kiswahili hali hii ilipelekea kukua na kuenea haraka



8.Fafanua matatizo yaliyojitokeza katika kukisanifisha wakati wa ukoloni.(necta 2004 swali la 2)
Usafishaji
Ni kulinganisha lugha na kuifanya ikubalike kwa watu wanaohusika kimatumizi.Mambo muhimu katika usanifishajiwa lugha ni pamoja na kuangalia usahihi wake,kisarufi na kimatamshi.Hapo awali hatukuwa na na aina moja ya Kiswahili ambacho kilikuwa na maandishi ya aina na matamshi(lafudhi).Viswahili hivi vyote vilisambaa pwani ya Afrika mashariki ndivyo tunavyoviita Lahaja.Uwepo wa lahajanyingi za Kiswahili ndiyoiliyokuwa chanzo cha na haja  ya kuwa lugha moja ambayo ingetumiwa na kila msemaji.
Matatizo yaliyojitokeza katika kusanifisha ni kama yafuatayo;
Uhaba wa fedha,kipindi cha kusanifisha lugha ya Kiswahili wakoloni walikuwa na mitazamo tofauti kuhusu kukisanifisha Kiswahili kwani walikuwa na lengo la kukifanya kiweze kutoa huduma katika maeneo waliyokusudiwa,kwa vile hawakuwa na lengo la kukiendeleza Kiswahili walihofia kuwa na hadhi sawa na kiingereza  hivyo walitoa fedha kidogo mno kwaajili ya kuendeshea kamati mbali mbali na shughuli za usanifishaji.

Kutowashirikisha wazawa wa lugha,Kipindi cha kusanifisha lugha ya Kiswahili  shughuli zote za usanifishaji zilifanywa na wazungu matumizi ya baadhi ya maneno yalipewa kibali yalikuwa na kasoro,Mfano nje(inje),nge(nje).

Kutokukubalika kwa uteuzi wa Lahaja ya usanifishaji,Watu wengi hawakukubaliana na uteuzi wa lahaja ya kiunguja,Baadhi walidai kimombasa kingeteuliwa katika usanifishaji kutokana na historia yake ndefu kuliko kiunguja hivyo wataalamu kutoka Kenya (Mombasa)walipinga kuteuliwa kwa kiunguja.

Tatizo la maneno(msamiati),Kipindi cha usanifishaji kamati  ilianzisha maneno jinsi yanavyotamkwa na kuandikwa ni tofauti,wenyeji walilazimishwa kukubaliana na kuyatumia maneno hayo yaliyoundwa  katika kiswahili,Mfano mba(maandishi),mbu(maandishi)-(umbu)matamshi.

Uhaba wa vitabu vya kusoma,Vitabu vilivyotolewa na kamati ya usanifishaji vilikuwa vichache hivyo havikukidhi mahitaji ya watumiaji wa lugha ya Kiswahili.kutokana na uchache wa vitabu kazi ya usanifishaji ikawa ngumu sana.
Watu hawakuthamini machapisho ya Usananifishaji,watumiaji wengi wa Kiswahili hasa wazalendo wa lugha hii hawakuthamni machapisho yaaaaliyotolewa na kamat ya usanifishaji,kwasababu machapisho hayo yalikuwa na kasoro nyingi.Wazungu waligeuza sarufi ya lugha ya Kiswahili ikawa sawa nay a lugha ya kiingereza.Vile vile waliogopa Kiswahili kikisanifiwa zaidi kinaweza kuzaa lugha nyingine tofauti kabisa.Kiswahili hiki kiliiitwa Kiswahili cha Serikali (The standard Swahili) Hivyo wananchi waliona kama wameundiwa lugha ambayo waliiona  si sahihi.

Matumizi ya Kiswahili yalikuwa duni ukilinganisha na kiingereza, Maneno ya lugha ya kiingereza yalikuwa juu(yaani hali ya ubora na kiwango kizuri)lakini matumizi ya Kiswahili yalikuwa duni,kilipangiwa maeneo ya chini mfano kufundishia shule za msingi na vyuo vya ualimu wa shule za msingi,pia ilionekana kuwa Kiswahili ni lugha ya watu wa hali ya chini (makabwela) na kingereza kilipangiwa maeneo ya  juu kama mahakama kuu,vyuo,sekondari na n.k.


“Serikali baada ya uhuru ilijitahidi sana katika kukuza Kiswahili nchini Tanzania”Thibitisha kauli hiyo kwa kutoa mfano dhahiri (Necta 2006 swali la 1)
Maana ya kukuza
Baada ya uhuru mwaka 1961 serikali ya Tanzania ilichukua hatua tofauti tofauti za kukuza Kiswahili hili mwaka 1962 iliunda kamati maalum ya kuangalia uwezekano wa kiswahili katika shughuli rasmi za kiserikali na iliamuliwa Kiswahili kitumike Bungeni na shughuli zote za kiserikali.
Baadhi ya jitihada zilizochukuliwa ni:-
Kuteuliwa kwa lugha ya Taifa Kiswahili mwaka kiliteuliwa kuwa lugha ya mwaka 1963, mwaka 1964 kilianza kutumika katika Bunge na shughuli zote za kiserikali wizara za kiserikali zilihimizwa kutumia Kiswahili katika mawasiliano yote.
Kuundwa kwa vyombo vya kukuza na kueneza Kiswahili vyombo hivi zilisaidia sana kukuza na kueneza na kueneza Kiswahili mfano TUMI, UWAVITA, TUKI, BAKITA, TAKIKUKI NK.

Vyombo vya habari
Vyombo hivi vilitumika sana na kukuza na na kueneza Kiswahili baada ya uhuru mpaka sasa.Vyombo hivi vilijishughulisha na shuhuli zinazohusu kiswahili mfano, Radio, Magazeti, Televisheni. Kulikuwa na vyombo vya habari vya serikali na watu binafsi vyote vilitumia lugha ya Kiswahili kurusha matangazo yake na vipindi mbalimbali mfano Redio na televisheni, kulikuwa na redio ya taifa ambayo  kwa sasa inaitwa TBC.
DINI
Dini zote zilitumika za kiislamu na kikristo zilitumia lugha ya Kiswahili katika mahubiri yake na kuchangia kukuza na kueneza.
BIASHARA
Misafara ya biashara katika sehemu mbalimbali za nchi zilisaidia kukikuza na kukieneza hadi nchi za nje ya Tanzania.

Kampeni za kisiasa
Kampeni za kisiasa kama CCM, TANU zilisaidia sana ukuzaji na kueneza na vingine vyama vingi tangu mwaka 1992 zilipoanzishwa kutokana na zilipoanzishwa kutokana na kampeni za uchaguzi wa viongozi vyama cvya siasa na serikali zimechangia sana kukuza na kueneza Kiswahili kutokana na matumizi ya Kiswahili.
Utawala
Shughuli zote za utawala tangu mwaka 1963 kiswahili kilitumika katika shughuli zote za utawalahivyo zilisaidia sana kukua na mfano, maofisini, bungeni, mikutano ya serikali pia kilichaguliwa na serikali kuwa lugha rasmi.
Elimu ya watu wazima
Elimu hii ilianzishwa nchi nzima ikiwa imelenga wasiojua kusoma na kuandika,afya, ufundi,siasa na Kiswahili yalifunisha kwa Kiswahili kutokana program hii Kiswahili kilikuwa na kuenea na watu wengi waliweza kuzungumza, kusoma na kuandika.

Uchapishaji wa vitabu na majarida mbalimbali vilevile uchapishaji wa vitabu. Na majarija umechangia sana kukuza na kueneza Kiswahili kulikuwepo na vitabu vilivyochambua sarufi ya Kiswahili pamoja na fasihi ya Kiswahilipia majarida mbalimbali yalichapishwa mfano, mulika, zindiko jarida la Kiswahili nk. Vyote hivi vilisaidia kukuza.

Shughuli mbalimbali za utamaduni
Shughuli tofautofauti za kijamii zilisaidia kukuza hapa nchini hii ni kutokana na shughuli ambazo ziliwakatisha watu kwa kutumia Kiswahili kama lugha ya mawasiliano katika misibi, harusi, jando, nk. Shughuli hizi zilisaidia kukuza Kiswahili.

Sherehe mbalimbali za vyama
Mara nyingi zimeshangia kukua kwa Kiswahili kutokana na hotuba ambazo hutolewa kwa lugha ya Kiswahili viongozi hutumia Kiswahili kuhutubia wananchi mfano, siku ya muungano, sikukuu ya CCM, na siku ys uhuru wa Taifa nk.
a.   Jadili sababu za Kiswahili kuwa lugha ya taifa nchini Tanzania kuliko lugha nyingine za Tanzania (nect 2006) swali la 2
Lugha ya taifa
Ni ile lugha iliyochaguliwa kutumika katika taifa zima na inayoweza kutekeleza wajibu wa taifa.Lugha ya taifa inaweza kuwa kitambulisho cha taifa.
Lugha ya kibantu ni lugha za asili (makabila) mfano kisukuma, kipare, kigogo, kikurya nk.
Ili lugha ichaguliwe kuwa lugha ya taifa inahitaji kuwa na  sifa zinazohitajika ambazo Kiswahili kilikuwa nazo na lugha za makabila hazikuwa na sifa zote hizi.
Kiswahili kilikuwa kimeandikwa vya kutosha katika vitabu na magazeti mbalimbali
Mfano vitabu vya fasihi, sarufi, magazeti kama vile habari za pwani, kiongozi, ukulima wa siasa nk. Bali lugha za kibantu hazikuwa na magazeti yaliyoandikwa/kuchapwa kwa kibantu.

Kiswahili kilitumika kwa namna moja
Katika makabila mbalimbali kilitumika kwa namna inayofanana na hii ni kutokana na kufanyiwa usanifishaji kwa kutumia lahaja ya kiunguja.

Kiswahili kilikuwa na utamaduni wake,
Lugha hii ilikuwa na utamaduni wake asili haikutegemea kutokatamaduni nyingine.
Kiswahili kilikubaliwa kwa watanzania wote,
Wananchi au watumiaji walikubali Kiswahili kuwa lugha ya taifa lakini baadhi ya lugha za kibantu hazikukubaliwa na watumiaji.
Kilitumiwa na watu wengi
Kiswahili kilikuwa na watumiaji wengi kwa sababu watu walikuwa wanakijua kuongea na kusoma na kilikuwa chepesi tofauti na lugha za kibantu ambazo zilikuwa na watumiaji wachache.
Kilijitosheleza na mahitaji ya watu
Hii nayo sababu ilipelekea kuteuliwa kuwa lugha ya taifa kilitumika Nyanja zote kiuchumi, kisiasa,kielimu na kiutamaduni.

b.   Maneno ya lugha nyingine yanapoingizwa katika lugha ya Kiswahili yanakidumaza Kiswahili. Jadili kauli hii (nect 2007 swali la 1)
Wanaokataa wana mitazamo ifuatayo
Lugha yoyote ina tabia ya kukopa maneno kutoka katika lugha nyingine mfano Kiswahili kimekopa maneno kama ifuatavyo stati- shirt (kiingereza) nyonge - dhaifu (kiarabu) shule – schule (kijerumani) nk.
Zifuatazo ni hoja za kuthibitisha;
Kukua kwa lugha, kutokana na kukopa manenokutoka lugha nyingine lugha itajipatia msamiati ili lugha ikue inahitaji kujionezea mmsamiati.
Kujitosheleza kwa lugha na kukidhi mahitaji ya watumiaji, kwasbabu ya ongeko la msamiati watumiaji wa lugha watakidhi mahitaji ya lugha.
Pia lugha itajipatia istilahi mbalimbali mfano sayansi, kiuchumi, na kisiasa Ambayo itakidhi mahitaji katika Nyanja hizo hasa istilah za kisayansi ambazo dunia nzima inauratibu wa kutumia lugha moja ya kilatina lazima Kiswahili kufuata utaratibu huo.
Vilevile lugha itajipatia tafsiri mbalimbali kutoka katika lugha, maneno yaliyokopwa katika lugha
Wanaokubali wana mitazamo ifuatayo;
Kutotumia badhi ya misamiati ya Kiswahili baadhi ya watumiaji wa lugha hupenda kuchanganya maneno katika lugha mbili hasa wasomi mfano. Nina degree (badala ya shahada) ninafatilia job(kazi) nimekumiss(nimekukosa)nk.
Lugha inapokuwa na maneno mengi sana ya kukopa kiasi cha kupelekea kukopa kubadilika kwa kugha husika na kuwa kama lugha nyingine hali hiyo itadumaza lughaa hiyo na hatimaye kutumika kwa lugha ambayo maneno yake ni mengi mfano, waasisi wa dini ya kiislamu nghini Tanzania walikizidishia msamiati ya kiarabu katika lugha ya Kiswahili kuwa kama kiarabu.

12.“Tungo ni sentensi na sentensi ni tungo” kubali au kataa kwa kutoa sababu za kiutalamu juu ya usemi huo (NECTA 2005) swali la 5
Tungo ni matokeo ya kuweka na kupanga pamoja vipashio sahihi kwa lengo la kujenga vipashio vikubwa zaidi. Kuna ain nne (4) za tungo neno, kishazi, na sentensi
Sentensi ni kifungu cha maneno/neno chenye kiima na kiarifu ambacho hutoa taarifa kamili si kweli kwamba sentensi ni tungo na tungo ni sentensi kutokana na tofauti zifuatazo
Maana,tungo ni matokeo ya kupanga na kuweka pamoja vipashio sahihi ili kujenga vipashio vikubwa zaidi lakini sentensi ni kifungu cha maneno kuanzia neno moja na kuendelea chenye kiima na kiarifu na inatoa maana iliyokamili.
Aina, kuna aina nne za tungo ambazo nni neno, kirai, kishazi, na sentensi lakini sentensi ina aina nne ambazo ni sentensi shurutia, sahili, ambatano na changamano.
Si kila tungo inatoa maana kamili mfano kirai, kishazi tegemezi vinaposimama peke yake havileti maana lakini kila sentensi huleta maana kamili
Kuonesha hali mbalimbali si kila tungo huonesha hali mbalimbali mfano neno, kirai lakini sentensi huonesha hali mbalimbali mfano hali ya maulizo kushangaa, ombi, kuamuru
Muundo si kila tungo ina muundo wa kiima na kiarifu bali sentensi ina muundo wa kiima na kiarifu au muundo wa kirai nomino KN na kirai kitenzi (KT)
13. Kwa kutumia lugha onesha kazi tano (5) za mofimu “ku” (Necta 2007) swali la 5
Jibu
Mofimu ni kipashio kidgo kabisa cha kiisimu chenye maana ya kisarufi au ya kileksika, mofimu hujidhihirisha maana yake kwa kisarufi amabapo uundaji wa maneno unaambatanishwa na viambishi katika mzizi wa neno mfano lim- analim, a-na-cheza, tulisafir nk. Na katika maana ya kileksia kipashio hicho huwa ni sehemu ya neno ambalo haliambatanishwi na kiambishi linajitosheleza lenyewe mfano kaka, babu, maji, mbuzi nk.
Vilevile mofimu inasifa ya kutokugawanyika au kuvunja katika vipande bila kupoteza maana pia mzizi wa neno nao ni mofimu zifuatazo ni kazi za mofimu “ku”
Huonesha hali ya ukanushi katika njeo ya wakati uliopita ikiambatanishwa na pamoja viambishi kanushi kama vile si, ha
Yakinishi                  Kanushi
Mfano   Azizi alichelewa      -    Azizi ha-kuchelewa
Prisca alicheka       -    Prisca ha-kucheka

Inaonyesha kauli ya urejeshi mtenda/mtendwa
Mfano mazigo aliku – andika barua wewe
(mtendwa)
Felicia ha-kumwona kujibu (mtenda)

Inaonyesha njeo ya wakati uliopita
Mfano Zainab ha-ku-imba siku ya idd

Inaonyesha ngeli ya mahali (pa-mu-ku, ngeli 9)
Mfano Kuhali kwenu kunapendeza
Mahali kule kunavutia

Inanominisha vitenzi
Mfano cheza – kucheza
Imba – kuimba

Kuunda mzizi wa neno
Mfano Fatuma anapenda kula maandazi

Kinasaidia ujenzi wa silabi katika nomino
Mfano kuta, Kulwa


14.“Hivi leo matumizi ya Kiswahili ni makubwa ukilinganisha na yale yaliyomo kwenye kamusi ya Kiswahili sanifu .Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano hai. (1983)”(Necta 2004 swali la 9)
Maana ya matumizi ya Kiswahili na Kamusi
Kamusi ni kitabu cha orodha ya maneno yaliyopangwa kwa mujibu wa alfabeti pamoja na maana na maelezo yake. Kuna aina mbalimbali za kamusi; Lugha moja peke yake na kuna kamusi inayohusisha lugha mbili mfano Kiswahili – kiingereza.

Hivi leo matumizi ya Kiswahili ni makubwa tangu mwaka 1983 kamusi iliyoandikwa kipindi hicho mpaka sasa kuna vipindi mbalimbali tumepitia vyenye matukio mbalimbali hivyo kila tukio huwa lina msamiati mipya inayoibuka na kuongezeka kwa maneno mapya ambapo awali hayakuwepo kwenye kamusi iliyokwisha tolewa/andikwa. Baadhi ya maneno yanayoibuka husanifiwa na vyombo husika vya Kiswahili na kuwa lugha sanifu.

Vile vile kuna istilahi za maneno ambazo huhitajika kuundwa kutokana na ongezeko la sayansi na teknologia na kupitia vipindi mbalimbali vyenye matukio tofauti tofauti hivyo hulazimu hubadilika kutokana na historia huwa ni tofauti na kipindi kingine.

Tangu mwaka 1983 kuna matukio ambayo tumepitia kama vile wakati wa ulegezaji wa masharti ya biashara nchini, wakati wa mfumo wa vyama vingi.

Kipindi cha ulegezaji wa masharti ya biashara nchini baadhi ya maneno yalizuka na kuanza kutumika katika jamii ambayo hawali hayakuwepo kwenye kamusi ya mwaka 1983. Mfano utandawazi, uwekezaji vitega uchumi, ubinafsishaji n.k

Kipindi cha mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992 hadi leo. Pia kuna maneno mapya yaliyojitokeza ambayo awali hayakuandikwa kwenye kamusi ya 1983 mfano mkereketwa, mfurukutwa, mpambe, ngangari na hivyo ongezeko la matumizi ya Kiswahili sasa ni kubwa ukilinganisha na mwaka 1983.

15.Fafanua dhana ya kiunganishi huru kwa kutumia mifano dhihirisha tofauti kati ya kiunganishi huru na aina nyingine ya ya kiunganishi.
Viunganishi ni maneno, kikundi cha amneno au kiambishi chenye kuunganisha maneno, kirai, kishazi, au sentensi.
Dhima ya kiunganishi ni kuunga vipashio viwili au zaidi vyenye hadhi sawa na kisarufi.
Viunganishi huru.
Ni viunganishi vinavyosimama pekee katika tungo katikati ya vipashio vinavyoungana japokuwa baadhi ya kiunganishi huweza kutoka kabla ya vipashio vinavyoungwa.
Mfano.     Nilitembea hata nikachoka
Hata ukiniimbia sitakubali
Tofauti ya kiunganishi huru na aina nyingine ya kiunganishi
i.  kiunganishi huru huonyesha nyongeza
mfano
Baba na mama wamekwenda shambani.
ii.Viunganishi huru huonyesha sababu
Mfano
Juma alipigwa kwa sababu alitoroka
Kwa vile nimerusiwa nitarejea nyumbani.
iii.                Viunganishi huru huonyesha utenzi au chaguo.
Mfano          Sitaki pilau wala ndizi
Utamwandikia barua ama utampigia simu
iv.                Viunganishi huru huonyesha ulinganishi au unyume
Mfano          Juma alikuwa Maskini ingawa aliikuwa mchezaji
Pamoja na elimu yake musa hakuwa na huruma.
v.Viunganishi huru huonyesha wakati
Mfano          Sara alitoroka kisha Haruna akamfuata
Tulisafiri mpaka Tanga badaye tukaelekea Mombasa.
vi.                Viunganishi huru huonyesha mashrti.
Mfano          Kama unataka kufaulu soma kwa bidii.
Mahindi yatastawi endapo utawekea mbolea.

16.Tofauti kati yakiambishi awali na kiambishi tamati
a)                  Viambishi awali ni viambishi ambavyo huwekwa kabla ya mzizi wa neno. Na kwa kawaida hutokea upande wa kushoto wa mzizi.
Mfano: Anaimba
A-na – viambishi awali
Imb – mzizi wa neno
A – kiambishi tamati
a)   Viambishi tamati ni viambishi ambavyo hupachikwa ndani baada ya mzizi     wa neno.
Mfano. Anacheza
A-na – viambishi awali
Chez-mzizi wa neno
a-      Kiambishi tamati
17.“Mofimu huru zina hadhi ya neno” fafanua husemi huu kwa kutumia sentensi tano (5) tofauti.
Mofimu huru ni mofimu ambazo huundwa kwa umbo linalojitosheleza kimaana.
Mfano
i.                    Lilian ni mwanafunzi wa shule ya sekondari tegeta.
     N
ii.                  Mtoto mdogo analia
                            V
iii.                Isaya na pascal wanaimba
                         U
iv.                Mungu anasema samehe mara saba sabini.
                                             T
v.                  Simu i mezani.
                        t
19.Wewe kama afisa manunuzi. Andika barua kwa mfanya biashara mashuhuri wilayani kwenu kuhusu agizo la bidhaa.










                                                                        WILAYA YA KASULU
                                                                        S.L.P 3456,
                                                                        KIGOMA
                                                                       13/8/2014
ELICIA BOOK SHOP
S.L.P 4784
DAR ES SALAAM

                Ndugu;
                            YAH: AGIZO LA BIDHAA
Mimi ni Afisa mnunuzu wa bidhaa mbalimbali, tafadhari naomba uniletee bidhaa zifuatazo.
i.                    Vitabu vya Kiswahili kidato cha 5-6  20@15000
ii.                  Vitabu vya phsics (oxford book 3) 30 @12000
iii.                Vitabu vya geography (oxford book 3-5) 50 @ 15000
iv.                Counter book (quire 3) 50 @ 3000
v.                  Vitabu vya history (oxford book 5-6) 40 @ 2000
Ninaambatanisha pamoja na hundi ya shilingi Milioni mbili 2,000,000/= ambayo ni gharama ya ununuzi pamoja na usafirishaji, Ninaomba bidhaa hizo zitumwe kwenye basi la “ulakozi trans”.
                     Wako katika kazi,
                   PRAXCEDA PROTAS
                    AFISA MNUNUZI.



20. Mofimu tegemezi zina kazi nyingi katika neno.
Taja kazi  (tano) 5 na uzielezee kwa kutumia Mfano.
Mofimu Tegemezi ni mofimu ambazo hufungamana na mofimu zingine na hazijitosherezi katika maana hutegemeana ili kueleza dhamira iliyokusudiwa.
i.                    Mofimu tegemezi huonyesha njeo/wakati
Mfano.  Nitaimba
ii.                  Mofimu tegemezi huonyesha urejeshi
Mfano. Mtoto aliyeanguka
iii.                Mofimu tegemezi huonyesha ukanushi.
Nimesoma – Sijasoma
iv.                Mofimu tagemezi huonyesha nafsi
Mfano. Nimekuona – Nafsi ya pili umoja ‘mtendwa’
v.                  Mofimu tegemezi huonyesha hali mbalimbali
Mfano.  Ukija utamkuta – masharti.
21. Eleza tofauti tano za barua ya kindugu (kirafiki) na barua rasmi (kikazi)
Barua ya kindugu ni barua ya inayoandikwa kwa ajili ya kusalimiana, kutoa shukrani nk.
Wakati barua ya kikazi ni barua inayoandikwa kwa ajili ya kuomba kazi, kuagiza vifaa, kumwalika kiongozi, kuomba ruhusa na mengineyo.
Barua ya kirafiki huwa na anwani moja ya maandishi tu. Wakati barua rasmi (kikazi) huwa na anwani mbili, anwani ya mwandishi na mwandikiwa.
Barua ya kirafiki (kindugu) huwa haina kumbukumbu namba wakati barua rasmi (kikazi) huwa na kumbukumbu namba ya mwandikiwa.
Barua ya kirafiki (kindugu)huwa haina kichwa cha habari wakati barua rasmi (kikazi) huwa n a kichwa cha habari kuhusu jambo Fulani. Mfano Kuomba kazi
Barua ya kirafiki (kindugu) huanza na salaam wakati barua ya kikazi (rasmi) huwa aina salamu.
Barua ya kirafiki (kindugu) haina sahihi ya mwandishi wakati barua ya kikazi huwa na sahihi ya mwandishi.

22. Fafanua misemo ifuatayo.
i.                    Mungu si athumani
ii.                  Kata mzizi wa fitina
iii.                Mtu kidole
iv.                Kondoo si mali
v.                  Kuiba kauli
Mungu si athumani
Maana yake Mungu ni Mungu si mwanadamu umuhimu wa msemo huu ni kwamba. Mungu hatendi kama mwanadamu.
Kata mzizi wa fitina
Maana yake ni kuondoa chanzo cha ubaya au fitina umuhimu wa msemo huu ni kuondoa chanzo au mzizi.
Mtu kidole
Maana yake mtu hatambuliki kwa kunyoshea kidole, umuhimu wa msemo huu ni kwamba hutambulika kwa mazuri na mabaya.
          Kondoo si mali.
Maana yake ni kumdharau mtu au kumshusha thamani/hadhi, umuhimu wa msemo huu, tusimdharau mtu wala kumshusha thamani.
       Kuiba kauli
Maana yake ni kuchangia jambo lisilokuhusu. Msemo huu unatufundisha kuwa tusifuatilie mambo yasiyotuhusu.

23. . Kwa kutumia sentensi; Onyesha maana ya kila neno kwa maneno yafuatayo.
AU
Maneno yafuatayo ni tata kwa kila neno tunga sentensi zenye maana zaidi ya moja.(Necta 2004 swali 7 na Necta 2006 swali la 7)
a. Kata
Ø  Ni kitendo cha kugawa kitu katika vipande kadhaa.
Ø  Ni eneo Fulani la kijografia
b.Panda
Ø  Kufukia mbegu ardhini.
Ø  Kukwea mlima au mti.
c. Paa
Ø  Sehemu ya juu ya nyumba
Ø  Mnyama wa porini anaye fanana na mbuzi.
Ø  Enda juu.
d.      Kamba
Ø  Aina ya samaki
Ø  Uzi unaotokana na nailoni unaotumika kufungia kitu.
e. Mbuzi
Ø  Ni mnyama wa kufugwa
Ø  Kifaa cha kukunia nazi
f. Nyanya
Ø  Ni kiungo.
Ø  Mzazi wa kike wa baba au mama
g.Kima
Ø  Ni mnyama jamii ya nyani.
Ø  Ni kipimo
h.Kifaru
Ø  Kifaa cha vita
Ø  Mnyama wa porini
i.  Juma
Ø  Ni jina (nomino)
Ø  Jumla ya siku saba
j.  Shinda
Ø  Faulu/fanikiwa
Ø  Kaa mahari kwa muda mrefu.
k.Tupa
Ø  Kifaa cha kunolea
Ø  Rusha kitu mbali
l.  Meza
Ø  Samani
Ø  Kitendo cha kutia kitu kinywani.
m.    Ua
Ø  Kitendo cha kutoa/kuondoa uhai kwa mtu au mnyama
Ø  Pambo
n.Kaa
Ø Kipande cha moto
Ø Kuweka makalio chini
Ø Mdudu wa majini/nchi kavu
o.                  Jiko
Ø  Mahali/kifaa cha kupikia
Ø  Mke
p.                  Kanda
Ø    Eneo Fulani lenye misingi ya kisiasa na kijamii
Ø    Kitendo cha kuchanganya unga na maji ili kutengeneza bonge la maandazi, chapati nk.
q.      Mama
Ø      Mzazi wa kike
Ø  Jinsia ya kike.
r.  Koo
Ø  Sehemu ya mwili wa binadamu
Ø  Chimbuko la udugu
s. Kibibi
Ø  Kufanya mambo kizee.
Ø  ………………………………………………
t.  shuka
…………………………………………
u.Wali
Ø  Wasichana waliowekwa ndani kwa ajili ya mafunzo.
Ø  Chakula cha wanga kinachotokana na mpunga.

24. Unganisha tungo zifuatazo kwa kutumia o-rejeshi
(nectar 2013 swali la 4)
O-REJESHI
Ni kiambishi kinachotumiwa kurejelea kwenye nomino ambayo huwa imetajwa kabla ya kitenzi chenyewe kutajwa.viambishi hivi ndivyo vinavyosababisha utegemezi katika sentensi.
Utegemezi ni hali ya kipashio kimoja kutegemea kipashio kingine.
O-rejeshi ni viambishi rejeshi vinavyotaja mtenda, mtendwa, mtendewa, wakati,hali au sababu kama mazingira ya kutokea jambo Fulani au jingine.

MAZINGIRA YA UTOKEAJI WA O-REJESHI
O-rejeshi hutokea katika mazingira mbalimbali ya neno. Huweza kutokea katikati,mwishoni au katika mzizi wa “AMBA”. mazingira hayo ni kama yafuatayo.
a. Kirejeshi kinachopachikwa katikati
Hapa huwa ni O-rejeshi ambayo huambikwa katikati ya viambishi awali kadhaa na mzizi wa kitenzi. Huwa na muundo wa: Awali+Rejeshi+Mzizi.
Mfano.                Mwalimu aliyesafiri jana amerudi leo
Kisu kilichopotea jana kimeonekana leo.
Nguo iliyochanika imetupwa
b.O-rejeshi  inayopachikwa mwishoni
Hapa huwa na kilejeshi ambacho hupachikwa mwishoni mwa kitenzi. Muundo wake huwa.
Kitenzi+Rejeshi. Viambishi hudokeza mazoea
Mfano.              Samba aungurumaye ni mkali
Jino liumalo hung’olewa.
c. O-rejeshi hupachikwa kwenye mzizi wa AMBA
Umbo la AMBA hupachikwa kirejeshi mwishoni na kuwa na muundo wa AMBA+Rejeshi.
Iwapo mzizi wa AMBA umetumika, kirejeshi huweza kutokea mwishoni tu mwa mzizi huu na hakiwezi kurudiwa tena katika kitenzi kingine.
Mfano,          Kitabu ambacho umesoma kimechanika
Juma amepata adhabu ambayo haiwezi
Mtoto ambaye hatafaulu hatapewa zawadi
Unganisha tungo zifuatazo kwa kutumia O-rejeshi.
a.       Mafisadi wamekamatwa. Mafisadi wamefikishwa mahakamani.
Mfisadi waliokamatwa wamefikishwa mahakamani.

b.      Kitabu kimenunuliwa. Kitabu kipo madukani.
Kitabu kilichonunuliwa kipo kabatini.

c.       Mfadhili amepatikana. Mfadhili mkarimu sana
Mfadhili aliyepatikana ni mkarimu sana.

Eleza maana ya Istilahi zifuatazo

i.  Esperanto
ii.Pijini
iii.                Lahaja
Jibu
a.      Esperanto
Ni lugha sesere iliyoundwa na binadamu lugha hiyo ilikusudiwa kutumika kama lugha ya pili ya kimataifa huko ulaya.
b.      Pijini
Ni lugha inatozuka baada ya makundi mawili au zaidi kukutana kila moja likizungumza lugha yake. Ili waweze kuwasiliana, kila moja katika makundi hayo hujaribu kurahisisha muundo wa lugha na sarufi yake, msamiati n.k. Ili kupata lugha rahisi itakayowezesha kuwasiliana. Lugha ambayo huzuka huitwa pijini.
c.       Lahaja
Ni tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika lugha kuu yenye asili moja. Tofauti hizo zipo katika matamshi (lafudhi),maumbo au matumizi ya maneno
AU
Ni upashanaji wa habari kwa kutumia ishara au sauti za nasibu unaotumiwa na kikundi Fulani cha watu.

Vitenzi vya Kiswahili vina tabia yake. Kwa kutumia mifano ya sentensi tano (5). Onyesha tabia tano (5) za vitenzi.
Jibu
Vitenzi ni aina ya neno linalotoa taarifa juu ya tendo linalofanyika au linalotendwa na kiumbe au kitu.
AU
Ni neno linaloeleza jambo lililotendwa au jambo lililotendeka. Kitenzi au vitenzi huarifu tendo linalofanyika au linalofanywa na mnyama, mtu au kiumbe chochote kinachoweza kutenda jambo kama vile.:
Soma, imba, kimbia, andika, sikiliza, kula, kunywa, lala, uliza, amuru nk.
Vitendo vya Kiswahili havisimami pekee vinapotumiwa katika tungo, bali huambatana na viwakilishi vingine vyenye kuwakilisha mtenda wa tendo au mtenda.huambishwa pia viambishi vyenye kuonyesha wakati tendo linapofanyika kama vile:
Dada            a-na-soma
Watoto         wa-na-ruka
AINA ZA VITENZI
                    i.            Kitenzi kikuu (T)
Ni kitenzi ambacho kinaweza kujitokezapekee katika sentensi.
AU
Ni vile ambavyo hubeba ujumbe muhimu wa kiarifu cha sentensi. Kitenzi kikuu lazima kiwepo katika sentensi, kwani ndicho hubeba maana ya kimsingi ya sentensi. Huitwa kitenzi kikuu hasa kinapoandamana na kitenzi kisaidizi.
Mfano
Mchezaji anacheza mpira
T
Mary anaimba nyimbo
T
Anna anaandika barua
T
                  ii.            Vitenzi visaidizi (TS)
Ni vitenzi ambavyo hutoa taarifa ya kusaidia kitenzi kikuu. Hutoa kama  vile uwezekano, wakati hali n.k. Vitenzi visaidizi daima hutumika pamoja na vitenzi vikuu, ndivyo vinavyobeba viambishi vya wakati.
Mfano              Mtoto alikuwa anacheza mpira
TS          T
Juma amewahi kunitembelea mara moja
TS               T
Sisi tutakuwa tumelala
TS           T
                iii.            Vitenzi vishirikishi
Ni vitenzi ambavyo hufanya kazi ya kuunga sehemu mbili za sentensi
Hushirikisha kitu kitabia, kihali na kimazingira. Sehemu ya kiarifu, yaani iliyo na kitenzi si kamilifu
Mfano:
Juma ni Daktari
Mtoto si mgonjwa
Vitenzi vya Kiswahili vina tabia zifuatazo.
i.                    Kuonyesha wakati tendo linapofanyika
Mfano
A-na-lima       wakati uliopo
A-li-lima         wakati uliopita
A-ta-lima        wakati ujao
ii.                  Kuonyesha hali ya tendo
Mfano:
A-na-lima - hali ya kuendelea kwa tendo
Hu-lima - hali ya mazoea
A-me-lima - hali timilifu
A-nge-lima - hali ya mashart
iii.                Kuonyesha nafsi
Mfano
Ni-na-lima. Tu-na-lima. Nafsi ya kwanza
U-na-lima. M-na-lima. Nafsi ya pili
A-na-li-ma. Wa-na-lima. Nafsi ya tatu.
iv.                Kuonyesha hali mbalimbali za tendo.
Mfano
Baba analima shamba
Lima - kutenda
Limwa - kutendwa
Limiwa  - kutendewa
Limika - kutendeka
v.                  Kuonyesha urejeshi wa mtenda/mtendwa/mtendewa.
Mfano
Mwanafunzi anayesoma ni mwelevu (mtenda)
Mwalimu amempiga mwanafunzi mtoro (mtendwa)

Kwa kutumia mifano dhihirisha, fafanua dhana zifuatazo (nectar 2012 swali la 3)
A.    KIIMA (K)
Ni sehemu katika sentensi ambayo hujaza nafasi ya mtenda au mtendewa jambo linaloelezwa. Katika sentensi kiima hutokea kushoto mwa kitenzi
Mfano
Baba/amempiga mtoto
K
Mtoto amepigwa na Baba
K

Vipashio vya kiima
Kiima huundwa na vipashio vifuatazo:-
i.                    Nomino peke yake (N)
Mfano
Mtoto /anacheza mpira.
N
Daktari/anamtibu mgonjwa
K
ii.                  Nomino, kiunganishi na nomino (N+U+N)
Baba na mama /wanalima shamba.
K
Kaka na dada wanacheza
K


iii.                Nomino na kivumishi (N+V)
Mfano
Watoto wote/ ni wagonjwa.
K
Wakulima wote/ wameondoka.
K
iv.                Kivumishi na nomino
(V+N)
Mfano
Yule mtoto/ ni mlevi
K
Kile kipini /ni cha dhahabu
K
v.                  Kiwakilishi peke yake
Mfano,
Wangapi/wamesafiri leo
K
Wewe/huna matatizo
K
vi.                Kiwakilishi na kivumishi
Mfano.
Vile vyao/vilivyookotwa kule
K
Zile zingine/zilikuwa imara
K
B.     CHANZO (CH)

Ni neno au kikundi cha maneno kinachojaza nafasi ya kielezi katika tungo. Chagizo huweza kutokea mara baada ya kitenzi kikuu au baada ya kishamirisho.
Mfano:-
Mama ansoma kitabu polepole
Ch
Mtoto anacheza vizuri sana
Ch
SIFA ZA CHAGIZO
i.                    Chagizo kwa kawaidahuwa ni kielezi au kirai kielezi au kirai kihusishi ambacho kinafanya kazi kama kielezi
Mfano
Mary anaonekana mnyonge mno
Ch
ii.                  Hutumika kufafanua kitenzi/kivumishi/kielezi.
Mfano.
Mbwa hukimbia  haraka sana
Ch
C.    SHAMIRISHO
Ni jina au kikundi jina kinachojaza nafasi ya mtendwa katika sentensi.
Shamilisho hutokea baada ya kitenzi kikuu au baada ya kitenzi kishirikishi
Mfano
Juma analima shamba letu
D.    UTOHOAJI
Ni kulichukua neno kulifanyia marekebisho Fulani na kulitumia ili liendane na kanuni na taratibu zilizoko katika lugha husika
Mfano.
Shirt - shati
Skirt – sketi
Cake – keki
E.     URUDUFISHAJI
Ni hali ya kurudia rudia neno ili kuunda neno linguine
Mfano
Pole – polepole
Kimya – kimyakimya

Moja ya sifa za sentensi za Kiswahili ni kuonyesha hali mbalimbali. Fafanua kwa hoja tano (5) ukitoa mifano kwa kila moja (mock 2014-dar swali la 5)
i.          Hali ya kuendelea kwa tendo.
Mfano
Alifika shuleni akilia.
ii.            Hali ya masharti
Mfano
Mwanafunzi akisoma atafaulu mtihani.
               iii.      Hali timilifu
                         Mfano
                   Neema amekula chakula
            iv.Hali ya kuamuru
             Mfano
             Nenda
Eleza njia zilizotumika kuunda kila moja ya maneno haya.(mock 2014 dar swali la )
a.      UDA
Ufipishaji au kufupisha kikundi cha maneno. Silabi kutoka katika baadhi ya maneno ya kikundi huchaguliwa ili kupata neno moja/jipya
Usafiri  Dar es salaam

b.      UGILIGILI
Kuchukua maneno. Maneno huchukuliwa kutoka makabila mbalimbali ya kibantu. Ugiligili (kimiminika) kinyakyusa.

c.       ASKARIKANZU
Miambatano au kuambatisha maneno. Ni kuweka pamoja maneno mawili au zaidi ili kupata neno jipya.
Askari + kanzu= askarikanzu.

d.      MAREHEMU
Utoaji au kutohoa maneno.
Ni kulichukua neno kutoka lugha nyingine (ya kigeni ) na kufanyiwa marekebisho ya kisarufi na kutumika katika lugha husika.
Marehemu – Almarhum (kiarabu)

e.       UMEME
Kutafsiri neno.
Ni kulipa maana neno kama linaloelezwa katika kamusi.
Electric – umeme.

Kwa kutumia tungo kati ya zifuatazo. Onyesha kivumishi kisha bainisha aina ya kivumishi husika (nectar 2011 swali la 4)
a.       Kikombe cha kaka kimevunjika
Cha kaka – kivumishi cha
A – unganifu
b.      Wachezaji wenu wanatafuta mpira.
Wenu – kivumishi kishirikishi
c.       Msichana mrembo amejikwatua
Mrembo – kivumishi cha sifa
d.      Viatu vyote vimechafuka
Vyote kivumishi cha pekee
e.       Wanafunzi wachache wamenunua vitabu
Wachache – kivumishi cha idadi

Bainisha kauli zinazowakilishwa na vitenzi vilivyotumika katika katika sentensi zifuatazo.(nectar 2013 swali la 5).
a.       Refa alichezesha mechi vizuri
Kauli ya kutendesha.
b.      Pili amevunjwa mguu
Kauli ya kutendwa
c.       Wanafunzi wanasomeana kitabu
Kauli ya kutendana
d.      Mafuta yamemwagika
Kauli ya kutendeka


Kwa kutumia mifano taja miundo mitano ya kirai nomino (KN) (nectar 2012 swali la 7)
Ni aina ya kirai ambacho hufanya kazi kama nomino. Neno kuu la kirai nomino ni nomino au kiwakilishi cha nomino kinaundwa na:-
i.                    Nomino peke yake
Mfano Chakula kinapikwa
KN
ii.                  Kiwakilishi peke yake
Mfano
Wao wataondoka kesho mchana
KN
Chako kimepotea kabisa
KN
iii.                Nomino, kiunganishi na nomino
Baba na mama wanapika
KN
Neema na Baraka wamesafiri
KN
iv.                Kiwakilishi na kivumishi
Mfano Vile vyao viliokotwa kule
KN
Wengi wao hawapendi ngoma za asili.
KN
v.                  Kivumishi na nomino
Kile kiti kinapendeza
KN
Maneno huweza kubadilika kutoka aina moja na kuwa nyingine” Dhihirisha kauli hii kwa kubadili maneno yafuatayo kwa kuzingatia maneno yalioko kwenye mabano (nectar 2012 swali la 4)
a.       Mkono (badili kuwa kielezi)
Mkononi
b.      Kwenda (badili kuwa nomino)
Mwendo
c.       Bora (badili kuwa kitenzi)
Ubora
d.      Ogopa (badili kuwa kivumishi)
Mwoga
e.       Mzazi (badili kuwa kitenzi)
Mlezi
f.       Bisha (badili kuwa kivumishi)
Mbishi
g.      Refu (badili kuwa kitenzi)
Ndefu/urefu
h.      Linda (badili kuwa nomino)
Lindo
i.        Kabati (badili kuwa kielezi)
Kabatini
j.        Uguza (badili kuwa nomino)
Muuguzi
Eleza maana ya dhana zifuatazo kama zinavyotumika katika kamusi.
i.                    Matini
Ni sehemu ya vidakizo vyote vya kamusi husika kuanzia herufi za alfabeti a – z
ii.                  Kidahizo
Ni neno lolote linaloingizwa katika kamusi na kupewa fasihi yake.
iii.                Sherehe
Ni taarifa ambazo huingizwa mwishoni mwa kitabu kama kiambatanisho.
iv.                Kitomeo
Ni aya ndogo katika kamusi zenye vidakizo na maana yake.
Wakilisha
Fanya kitu kwa niaba ya mtu mwingine.
Mfano
Yohana alimwakilisha baba yake kwenye harusi ya dada yake.
Wasilisha
Ni kitendo cha kupeleka kitu/vitu.
Mfano
Mwalimu wa zamu aliwasilisha Orodha ya mahudhulio ya wanafunzi.
Kodi
Ni kulipa ushuru au kitu ……………………
Mfano:-
Mamlaka ya mapato imekusanya kodi katika maduka ya mtaa wa wazo.
Kodisha
Ni kitendo cha kumpa mtu kitu atumie kwa malipo.
Mfano
Neema amekodisha ukumbi wa home boys.
Kula
Ni kitendo cha kuweka kitu mdomoni na kukimeza.
Mfano
Babu anakula chakula.

Kura
Ni kitendo cha kumchagua mtu ili ashike wadhifa Fulani (uongozi Fulani) kwa kuandika karatasi ya siri au kunyoosha mkono.
Mfano
Wanakijiji walipiga kura ili kumchagua mwenyekiti wao.
Baada
Ni kitendo kinachotarajiwa kufanyika (matarajio)
Mfano
Nitakuja baada ya kumaliza kula chakula cha mchana.
Badala
Niaba ya kitu Fulani.
Mfano
Nilienda arusini badala ya baba.
Onesha
Kueleza uelekeo Fulani
Mfano …………………
Onyesha ……………..

Kwa kutumia mifano. Fafanua dhana zifuatazo kama zinavyotumika katika fasihi (nectar 2013 swali la 11).
a.      Tashibiha
Ni tamathali inayounganisha vitu kwa kutumia viunganishi kama vile mfano wa, mithili ya, kana kwamba, sawa na, nk.
Mfano
Juma ni mweupe kama vyeta.
Saimon alifoka kwa hasira mithili ya samba.
b.      Takriri
Ni kurudiarudia maneno kwenye sentensi au kwenye usemi ambayo nia yake ni kusisitiza
Mfano
Neema ni mwembambamwembamba sana.
c.       Sitiari
Ni tamathali inatolinganisha matendo, vitu au tabia ya vitu vyenye maumbile tofauti bila viunganishi.
Mfano
Askari Yule ni samba
Nywele za mary ni chafu
d.      Tashihisi
Ni tamathali ambayo vitu visivyo na sifa walizonazo watu hupewa sifa hizo.
Mfano
Majani yote porini yalishangilia kwa vigelegele.
Manyunyu ya mvua hatimaye yaliimba wimbo kwa furaha.
e.       Tanakari sauti
Ni mbinu ya kuiga sauti ya milio mbalimbali. Milio hii ni ya wanyama, magari, vitu, nk.
Mfano
Alianguka chini pu!
Alitumbukia majini chubwi!
f.       Tafsida
Ni tamathali/mbinu ya kupunguza ukali wa maneno au matusi katika usemi.
Mfano
Naenda jikoni na wala si kupika.
Amejifungua badala ya amezaa

Vishazi tegemezi hufanya kazi ya vivumishi viwapo katika tungo. Onyesha ukweli wa kauli hito kwa kutumia mfano mine (4) ya sentensi.
Vishazi Tegemezi (K/TG)
Ni kishazi kinachotawaliwa na kitenzi kisaidizi, ambacho muundo wake hukifanya kutegemea kitenzi cha kishazi huru ili kuweza kutoa ujumbe uliokusudiwa kishazi tegemezi peke yake hakitoi ujumbe unaojitosheleza.
Mfano
Kitabu kilichopotea juzi
Mwanafunzi anayesoma sana.

Kishazi tegemezi cha weza kutoa maana kamili kinapoandamana na kishazi huru
Mfano
Kitabu kilichopotea juzi kimepatikana leo.
K/TG/V
Mwanafunzi anayesoma sana amefaulu.
K/TG/V
Hali hii tegemezi inakinyima kishazi tegemezi hadhi ya kuwa sentensi.
Vishazi tegemezi namana vinavyofanya kazi kama vivumishi.pale vinapotokea na nomino inayovumishwa
Mfano
a. Kiti kilichopotea jana kimeonekana
K/TG
b.Uzi ulionunuliwa jana haufai kabisa
K/TG

Pale visipotokea na nomino inayovumishwa
c. Uliyemwona jana anaondoka kesho asubuhi
K/TS
d.      Aliyekuwa katibu kata wetu amehama
K/TS
Huku ukitumia mfano mmoja mmoja, taja sifa nne za kishazi tegemezi.
Kishazi tegemezi, ni kishazi ambacho muundo wake hukifanya kutegemea kitenzi cha kishazi huru ili kuweza kutoa ujumbe uliokusudiwa.

Sifa za kishazi tegemezi.
i.                    Kishazi tegemezi hakiwezi kutoa maana kamili kama hakikuambatana na kishazi huru.
Mfano Mtoto aliyekuja jana.
ii.                  Kishazi tegemezi kinaweza kikafutwa katika sentensi bila kuharibu maana kamili ya sentensi.
Mfano. Mwalimu aliyefundisha jana ni mkarimu.
iii.                Kishazi tegemezi kinaweza kutanguliwa na kufuatwa na kishazi huru.
Mfano Nilimwona Tina nilipokuwa kanisani
Nilipokuwa kanisani nilimwona Tina
iv.                Kishazi tegemezi kinaweza kutambulika kwa kuwa na viambishi rejeshi vinavyoambatanishwa katika vitenzi.
Mfano Kitabu kilichopotea jana kimeonekana
v.                  Kishazi tegemezi kinaweza kutambulika kwa kuwepo vivumishi tegemezi kama vile ingawa, kwamba.
Mfano. Mwalimu amesema kwamba wanafunzi wengi hawana nidhamu.
Fafanua dhima ya viambishi vilivyopigiwa mstari katika vitenzi vifuatavyo.
a.       Anacheza
Kuonyesha njeo ya wakati uliopita.
b.      Tumelima
Kuonyesha kauli ya kutenda
c.       Aliyekukumbuka
Kuonyesha urejeshi
d.      Wangelisoma
Kuonyesha masharti

Kama mtaalamu wa lugha ya Kiswahili. Onyesha makosa ya kimantiki na ya kisarufi yanayosababishwa na wazungumzaji wa lugha hiyo,

i.                    Makosa ya kisarufi
a.      Matamshi
b.       
Watu wengi hushindwa kutamka baadhi ya sauti za Kiswahili.
Mfano. Wakurya hutumia ‘r’ badala ya ‘l
Naenda kurara badala ya kulala

ii.                  Makosa ya msamiati
Baadhi huchanganya msamiati wakati wa kuzungumza. Watu wengi huchanganya neno mazingira na mazingira
Mfano. Mazingira ya hapa ni machafu hii sio sahihi.
Mazingira ya hapa ni machafu hii ndio sahihi.
Jack amenenepa sana hii sio sahihi.
Jack amenenepa sana hii ndio sahihi.

iii.                Makosa ya kimuundo
Kwa kawaida sentensi za Kiswahili huanza na nomino ya mtenda au mtenda na kufuatiwa na kitenzi.
Mfano. Eva anaandika vizuri.
Mzungumzaji asiyefuata kanuni ya mpangilio wa                  maneno anaweza kusema. Vizuri anaandika Eva.

iv.                Makosa ya kuongeza vitamkwa
Mfano. Amekwendaga  - Amekwenda
Hapendagi – hapendi
Mtoto msafi – mtoto safi

v.               Makosa ya kimantiki
Mantiki ni utaratibu mzuri wa kufikiri. Makosa ya kimantiki ni yale yanayoonyeshwa kukosekana kwa utaratibu wa fikra. Makosa ya kimantiki yanatokana na upofu wa mawazo ya mzungumzaji.
Usimwage kuku kwenye mchele wengi
Usimwage mchele kwenye kuku wengi.
Mfupa hauna ulimi.
Ulimi hauna mfupa.
Kwa kutumia mifano ya lugha  ya Kiswahili,taja sababu 5 za Utata katika mawasiliano.(Necta 2012 swali 6)
AU
Maneno au tungo za Kiswahili zisipotumiwa kwa umakini zinaweza kueleweka hivi au vile na hivyo zinaweza kupotosha lengo la Mzungumzaji,Fafanua sababu tano(5) za kutoeleweka kwa maneno au tungo  kwa mifano dhahiri.

Utata ni hali ya neno au sentensi kuwa na maana zaidi ya moja.
Mfano
Neno “Barabara” lina maana zifuatazo,
Ø  Ni njia ipitawayo na magari na binadamu.
Ø  Sawasawa,au hakuna dosari.
Neno “Paa”lina maana zifuatazo;
Ø  Mnyama anayefanana na mbuzi
Mfano;Paa ni mnyama mwenye pembe ndefu
Ø  Enda juu au kwea angani
Mfano;Mwewe ni ndege anayepaa juu sana
Ø  Ni sehemu ya juu ya nyumba
Mfano;Paa la nyumba ya shule limeezuliwa.

Utata wa Sentensi ni hali ya sentensi kuwa na maana zaidi ya moja.
Mfano;
Ø    Mtoto anaendesha.
-Mtoto anaongoja chombo cha moto.
-Mtoto maradhi ya tumbo.
                      Chanzo cha utata katika sentensi hii ni neno ‘’Anaendesha’’
Ø  Musa amenunua mbuzi.
-Juma  amenunua kifaa cha kukunia nazi
-Juma amenunua mnyama afugwaye
Chanzo cha utata ni neno Mbuzi.

SABABU ZA UTATA KATIKA MANENO AU SENTENSI
Ø  Neno kuwa na maana zaidi ya moja
Mfano;
ü  Nileteeni nyanya
-Nileteeni kiungo/tunda
-Nileteeni mzazi wa kike wa baba au mama
ü  Sipendi buibui
-Sipendi mdudu anayejenga tandabui.
-Sipendi vazi linalovaliwa na wanawake wa kiislamu.
Ø  Utumiaji wa maneno yenye maana ya picha au  maana iliyofichika.
Mfano;
ü  Nina ua nyumbani kwangu.
-wigo
-kutoa uhai wa mtu au kiumbe
-Binti mzuri
-Mmea unaopendezesha.
Ø  Kutozingatia  taratibu za uandishi.
Mfano;
Tulimkuta Neema na rafiki yake,huruma.
Tulimkuta  Neema na rafiki yake  Huruma.
Sentensi ya kwanza ina maana kuwa tuliwakuta watu wawili  yaani Neema na rafiki wa Neema aitwaye Huruma.
-Alama ya mkato baada ya neno “yake” huonyesha kuwa taarifa imekamilika na neno “Huruma”ni Ufafanuzi tu wa “rafiki yake”
Sentensi ya pili ina maana kuwa tulimkuta Neema na mtumwingine ambaye ni rafiki wa Huruma.
ü  Kutumia neno bila kuzingatia mazingira au muktadha.
Mfano;Jeremia ametumwa na Rehema.
Katika sentensi hii ,msikilizaji na mzungumzaji wataelewana iwapo wote wanawajua Jeremia na Rehema na hali ya uwezekano wa yupi kumtuma mwingine.
ü  Kuwepo kwa mofimu za kauli ya kutendea /li/le/i/ na e/
Mfano;
Amempig-i-a ngoma.Sentensi ina maana zifuatazo;
                                                                         I.      Amepiga ngoma ili amfurahishe.
                                                                      II.      Amepiga ngoma kwa niaba yake.
                                                                   III.      Amempiga kwa kutumia ngoma.

Nyambua mzizi “lima” ili upate kauli zifuatazo za matendo (tahossa dar 2009)
a.       Kutenda
Lima
b.      Kutendeka
Limika
c.       Kutendwa
Limwa
d.      Kutendewa
Limiwa
e.       Kutendeka
Limika
f.       Kutendesha
Limisha

Eleza dhima za mofimu zilizopigiwa mistari (tahossa Dar 2009)
i.                    Kijana aliyewasili ni shupavu.
Inaonyesha urejeshi.
ii.                  Kiti kimevunjika
inaonyesha umoja (ngeli ya 4, ki-vi)
iii.                Akija nitafurahi
Inaonyesha masharti
iv.                Kijana hodari atoke mbele
Inaonyesha umoja katika nomino.
Sentensi zifuatazo zina makosa. Ziandike tena kwa kuepuka makosa hayo:-
a.       Ni budi kuoomba radhi kwa yaliyotokea
Sina budi kuomba radhi kwa yaliyotokea
b.      Maziwa ya motto yameingia nzi.
Nzi ameingia kwenye maziwa ya mtoto.
c.       Naomba uninunulie maembe kumi na mbili
Nakuomba uninunulie maembe kumi na mawili.
d.      Dhumuni la barua hii ni kutaka hali yako.
Dhumuni la kuandika barua hii ni kukujulia hali.

Nominisha vitenzi vifuatavyo kisha tunga sentensi moja kwa kila nomino.
a.       Hawili-Uhamisho
Baba aliamishwa kutoka Dar kwenda Mombasa.
b.      Ghadhibika – Ghadhabu
Ghadhabu yake haiwezi kuisha mpaka utubu.
c.       Afiki – Mafikiano
Mwalimu na mwanafunzi walifikiana kufanya masahihisho ya mtihani.
d.      Laumu – Lawama
Musa aliwalaumu sana watoto.
e.       Kumbuka – Kumbukumbu
Tarehe 14/10/ ni kumbukumbu ya Baba wa Taifa.
f.       Penya/Kipenyo/Mpenyo
Mwizi alipata mpenyo wa kupita akavunja duka.

Andika nomino tano (5) zinazoweza kuingia katika ngeli ya YU-A-WA, kasha tunga sentensi yenye Umoja, Wingi kwa kila nomino huku ukizingatia upatanisho wa kisarufi (mock Dar 2012 swali la 5)
NOMINO
i.                    Msichana
ii.                  Panzi
iii.                Nzi
iv.                Kiwete
v.                  Kiongozi

Umoja                                     Wingi
i.                    Msichana anaimba      Wasichana wanaimba
ii.                  Panzi anaruka              Panzi wanaruka
iii.                Nzi ananuka                Nzi wananuka
iv.                Kiwete anatembea      Viwete wanatembea
v.                  Kiongozi yu aja                       Viongozi wanakuja.

Fafanua dhima ya “na”  kama lilivyotumika katika sentensi zifuatazo;
(Eastern zone Education bord 2012)
(a)Ali na Japhet ni marafiki.
Imetumika Kuunganisha sentensi
(b)Tunafanya mitihani
Inaonyesha wakati uliopo
(c)Tangazo lilitolewa na mkuu wa shule.
Imetumika kama kihusishi
(d)   Nasi tumefurahi.
Inaonesha nafsi
(e)    Huyu anafanana na wewe.
Imetumika kuwianisha/kufananisha

Nini maana ya upatanisho wa kisarufi? kwa kutumia nomino zifuatazo taja ngeli zinazopatikana kutokana na kanuni ya Upatanishi.(Eastern zone Education board-EZEB 2012)
a.       Kijana
b.      Uovu
c.       Kiti
d.      Ufa

Upatanisho wa kisarufi
Ni uhusiano wa kisintaksia baina ya maneno ambapo neno moja hutawala umbo la kimofolojia la neno au maneno katika tungo.
Mfano;Watoto wadogo wanasoma.
Nomino
(a)    Kijana
Ngeli ya 4(ki-vi)
(b)Uovu
Ngeli ya 7(u-ya)
(c)    Kiti
Ngeli ya 4(ki-vi)
(d)   Ufa
Ngeli ya 6(u-zi)

“Kila Lugha ina tabia ya kuchukua maneno kutoka lugha nyingine ili kukidhi mahitaji yake kimsamiati”.fafanua kauli hii ukitumia maneno kumi (10) ya Kiswahili.(Necta 2011 swali la 4)

Msamiati wa lugha Kiswahili uliongezeka na kukua kwa njia ya kuchukua maneno kama yalivyo kutoka lugha nyingine kama ifuatavyo;
A. Kiingereza                                   Kiswahili
i. Tractor                                         Trekta
ii. Number                                        Namba

B. Kiarabu                                        Kiswahili
iii. Saalam                                                   salama
iv. Mahabusu                                              Mahabusu

C. Kireno                                                    Kiswahili
v.  Bibo                                                        Bibo
vi. Mesa                                                      Meza

D.    Kiajemi                                                   Kiswahili
vii.Randah                                                   Randa
vii.              Jamaadar                                              Jemedari

E.Kibantu                                                   kabila
ix. Ngeli                                                      kihaya
               x.Kitivo                                                     kipare

Yapange maneno yafuatayo kama yanavyoonekana katika kamusi ,kisha eleza maana ya kila neno kwa kutoa mfano mmoja(1) wa sentensi.
(a)  Falsafa  (b) Barizi  (c) Anuwai (d) Barubaru
(e)  Kinda     (f) Ajuza   (g) Fanusi  (h) Ghaibu
(i) Goigoi      (j) Kinanda.

Mpangilio wake;
(a) Ajuza
-Mwanamke mzee sana.
Mfano;
Ajuza Yule anatembea polepole sana.
(b) Anuwai
-Dhahiri
Mfano;
Wanafunzi walijibu maswali yote kwa mifano anuwai
(c) Barizi
-Punga pepo
-Kusanyika kwa watu kwaajili ya mazungumzo ya kawaida.
Mfano;
Baba na Mama wamekwenda baharini kubarizi.
(d) Barubaru.
-Kijana wa kiume aliyekwisha kubalehe.
-Samaki jamii ya papa.
Mfano;
Musa ni barubaru wa mzee kisonga.
(e) Falsafa
-Ni elimu ya asili, maana na sababu ya za mambo au vitu.
-Busara, hekima, mtazamo.
Mfano;
Falsafa ya baba wa Taifa ilihimiza Umoja na Mshikamano.
(f) Fanusi.
-Taa ya mkono; kandili
Mfano;
Fanusi ya Musa inachijiwa kwa siku moja.
(h)Ghaibu
-Mbali Mbali na macho
Mfano;
Nyumba ile ipo ghaibu yangu.
(i) Goigoi
-Mtu dhaifu
-Udhaifu
-Ngoma ya kupunga shetani: ngoma ya pungwa
-Mtu mvivu sana
Mfano;
Mtoto wa Neema ni goigoi sana
(j) Kinanda
-Chombo kinachotoa sauti kwa kupulizwa au misumari yake.
Mfano; Kinanda cha Musa ni kidogo kuliko cha Huruma.

Kwa kutumia mifano taja kazi za alama zifuatazo; (pre-necta kanda ya Dar 2011 swali la 8)
a.      Nukta
v  Hutumika kukamilisha sentensi.
Mfano; Baba yangu amefika
Hutumika kuonyesha ufupisho wa maneno
Mfano; k.v- kama vile
K.m – kwa mfano
S.L.P  - sanduku la posta.
v  Hutumika kuonyesha vipimo mbalimbali katika desimali.
Mfano:
Kilogramu 5.2
Mita 55:5
Saa 5:20
b.      Nukta pacha
v  Hutumika kutaja maneno yaliyo katika orodha
Mfano;
Nililetee vitu hivi: wino, karatasi, kalamu na kiti.
v  Hutumika kuashiria maneno ya msemaji
Mfano;
Alipomwona alimshambulia kwa maneno.
Wewe ni jambazi na mwizi kweli kweli.
v  Hutumika kutenganisha dakika na sekunde.
Mfano  saa 5:56
Saa 4:15
v  Hutumika kuonyesha uwiano baina ya namba
Mfano 5:7 8:10
c.       Mkato
v  Hutumika kuweka pumziko fupi katika sentensi
Mfano:
Tulipokuwa sokoni tulinunua samaki, mchele na ndizi.
v  Hutumika kutenga maneno yaliyo katika orodha
Mfano:
Ukifika nyumbani pika Ugali, Ndizi,samaki na wali.
v  Hutukika kabla ya alama za mitajo.
Mfano:
Musa alisema, “Nakupenda sana”
v  Hutumika kuonyesha vyeo, anuani au makazi baada ya jina la mtajwa
Mfano:
Hengapinge msambasa, Meya wa jiji la njombe
d.      Rutifaa (`)
v  Hutumika kutofautisha ng` na ng`
Mfano:
Ng`ambo, ng`ang`ania ng`arisha nk.
e.       Herufi kubwa
v  Hutumika kila mwanzo wa sentensi
v  Hutumika badala ya alama hizi (.), (?),(!) n.k
v  Hutumika kutaja majina ya pande za dira kama vile
Kusini, kaskazini, magharibi, mashariki.
v  Hutumika kutaja majina ya pekee.
Mfano:
Kutaja majina ya watu, mji, nchi, bara n.k.
Kama vile Nyaludzi, Gwivaha, Arusha, Tanzania n.k
Eleza dhima ya mofimu zilizopigiwa mstari katika maneno yafuatayo: (tahossa-zonal kidato cha 4 2010 swali la 6)
i.                    Ondokeni
Ni – kuonyesha wingi
ii.                  Ametoka
Me – inaonyesha wakati (njeo ya wakati timilifu)
iii.                Mkulima
M – inaonyesha umoja (mmoja katika nomino)
iv.                Cheza
Chez – mzizi wa neno
v.                  Amesomesha
Esh – inaonyesha kauli ya kutendesha.

“Moja ya hoja za kiisimu kuthibitisha ubantu wa lugha ya Kiswahili ni umbo la kitenzi”. Kwa hoja nne zenye mifano na fafanua namna ambayo kitenzi cha lugha ya Kiswahili kinavyofanana na lugha nyingine za kibantu (tahosa Dar zone 2013 swali la 10).

Vitenzi vya Kiswahili na kibantu.
Kuna uhusiano mkubwa kati ya vitenzi vya Kiswahili na kibantu.uhusiano huu upo katika viambishi, mnyambuliko, mwanzo na mwisho wa vitenzi.
a.      Viambiashi
Vitenzi vya lugha ya Kiswahili huundwa na viambishi awali mzizi na viambishi.
Mfano
Kiswahili-Analima-A-na-li-ma
Kikuyu-Ararema-A-ra-rem-a
Kindali-Akulim-A-ku-lim-a
1   2    3   4
b.      Mnyumbuliko wa vitenzi
Mnyumbuliko wa maneno ya Kiswahili na kibantu hufanana.
Mfano
Kiswahili – kucheka – kuchekesha – kuchekelea
Kindali – kuseka – kusekasha – kusekelela
Kibena – kuheka – kuhekesa – kuhekelela
Kikagulu – kuseka – kusekesha – kusekelela
c.       Mwanzo wa vitenzi
Vitenzi vya Kiswahili na kibantu huanza na kiambiashi awali cha nafsi.
Mfano
Kiswahili – Ni – nakwenda
Kibena – ndi – helela
Kindali – Ingubhuka
Kiyao – m - genda.
d.      Mwisho wa vitenzi
Vitenzi vya Kiswahili na kibantu huishia na Irabu a
Mfano
Kiswahili – kukimbia, kuwinda, kushika
Kindali – kukind-a kubhing-a, kukol-a
Hivyo mfano
Wa vitenzi vya Kiswahili na kibantu
a.      Uandaaji wa simu ya maandishi una utaratibu zake. Taja hatua zote unazopitia katika katika kuandaa simu ya maandishi (nectar 2010 swali la 9a).
Hatua za kuzingatia katika uandishi wa simu.
i.                    Anuani ya mpelekewa taarifa.
Anuani ya barua ya simu lazima iwe kamili na ya wazi wazi kuiwezesha barua hiyo kupelekwa kwa haraka.
Anuani ya mji ni lazima iwe na jina la mtu ikiwezekana na namba ya nyumba.
ii.                  Ujumbe au taarifa
Hiki ni kiini cha simu. Taarifa au ujumbe huelezwa kwa ufupi sana lakini hueleweke vizuri sana
iii.                Jina la mwandishi au mtuma simu
b.      Kwa kuzingatia hatua hizo andaa simu ya maandishi isiyozidi maneno kumi (10)juu ya taarifa yoyote.

RIZIKI JACKSON SLP 432 NJOMBE.
NJOO HARAKA BIBI ANAUMWA GODLOVE
Kwa kutumia mifano eleza maana ya:
(nectar 2011 swali la 7)
a.       Kamusi wahidiya
Ni kamusi inayoandikwa katika lugha moja tu, na inalengwa kwa wazungumzaji wazawa wa lugha hiyo mara nyingi huwafaa wanaojifunza lugha hiyo kama lugha ya pili au ya kigeni.
Vidakizo vya kamusi waliyo na maelezo ya maana huwa katika lugha moja.
b.      Rejesta
Ni mtindo wa lugha inayotumika mahali penye shughuli Fulani ambayo ni tofauti na lugha ya kawaida
Mfano
Lugha ya kivuvi ya kibiashara.
c.       Misemo
Ni fungu la maneno linalotumiwa na jamii ya watu kwa namna maalum ilikutoa maana Fulani
AU
Ni kauli yenye ukweli wa jumla inayotumiwa kusemea mambo mbalimbali yanayoafiki ukweli huo.
Mfano
·         Mtu kwao
·         Piga msasa
Misemo haina mana ya mafumbo bali inaeleza maana ya kauli moja moja.
d.      Lahaja
Ni tofauti ndogo ndogo zinazojitokeza katika lugha kuu yenye asili moja. Tofauti hozo zipo katika matamshi (lafudhi), maumbo au matumizi ya maneno.
e.       Lugha ya mazungumzo
Ni lugha inayotolewa kwa njia ya mazungumzo yam domo. Ni mawasiliano yanayohusisha msikilizaji na mzungumzaji.
Fafanua dhima ya “ji” katika maneno yafuatayo:
(nectar 2011 swali la 6)
a.       Jitu
Inaonyesha Ukubwaishaji
b.      Uzalishaji
Inaonyesha Unominishaji
c.       Anajikwatua
Inaonyesha urejeshi wa mtendwa
d.      Jicho
Inaonyesha umoja wa nomino.

Kwa kutumia mifano, eleza chanzo cha misimu na taja matumizi matatu 3 ya misimu.

Misimu
Ni maneno yasiyosanifu yanayozushwa na kikundi cha watu wachache wenye utamaduni moja ili kueleza mahusiano kama kikundi au kuhusu mahusiano ya kikundi au kuhusu jamii kubwa ambamo vikundi hivyo vinaishi katika kipindi Fulani cha wakati; maneno haya hupotea na yanayodumu husanifiwa na kuwa msamiati rasmi wa lugha inayohusika.

CHANZO CHA MISIMU
i.                    Huzuka kutokana na hali ya utani miongoni mwa watu mbalimbali. Mara nyingi misimu ya aina hii hubeba kebehi, dhihaka, kejeli, mabezo, dharau au kusifu kusiko kwa kawaida.
ii.                  Huzuka kutokana na vipindi mbalimbali vya kihistoria ambavyo huikumba jamii katika nyakati mbalimbali. Misingi ya kuzua misimu inakuwa ileile ya kutaka kukueleza dhna Fulani ambayo imejitokeza katika mfumo wa maisha ya mwana jamii.

MATUMIZI YA MISIMU
i.                    Hupamba lugha
Katika mazungumzo misimu ina mvuto na hupamba lugha, kwani misimu mara nyingi huwa imetiwa chumvi.
ii.                  Huibua hisia mbalimbali kwa wazungumzaji,misimu ina maneno yale yenye kubeba hisia, chuki, furaha, au karaha nk.
iii.                Huchekesha na hufurahisha
Maneno mengi ya misemo kuwa na mvuto na kutiwa chumvi nyingi,chuki, kejeli, mabezo, dharau au kujisifia kusiko kwa kawaida.

Muktadha wa utumizi wa lugha huwafanya wahusika kuibua maneno maalumu.
Jadili usemi huu kwa kutumia mifano ya sentensi tano (5) zionyeshazo miktadha tofauti. (nectar 2009 swali la 6)

MAJIBU
·         Mhudumu nipe chai mbili (hotelini)
·         Tusome somo ka kwanza (kanisani)
·         Kunywa mbili mara tatu kwa siku (hospitalini)
·         Andika kumbukumbu zote za kikao (ofisini)
·         Ambaye hakufanya mtihani apite mbele (shuleni).

i.                    Weka nomino zifuatazo katika ngeli za upatanisho wa kisarufi.

JIBU
a.       Kipofu
v  Kipofu yu mgonjwa
v  Vipofu wa wagonjwa
Ngeli ya 1 (yu-a-wa)

b.      Kiboko
v  Kiboko kimevunjika
v  Viboko vimevunjika
Ngeli ya 4 (ki-vi)

c.       Mkono
v  Mkono umevunjika
v  Mikono imevunjika
Ngeli ya 2 (u-i)

d.      Kalamu
v  Kalamu imevunjika
v  Kalamu zimevunjika
Ngeli ya 6 (u-zi)

ii.                  Kwa kutumia nomino hizo tunga sentensi moja yenye kiambishi cha O-rejeshi kwa kila nomino

a.       Kipofu aliyekuja jana ameondoka leo
b.      Viboko vilivyo vunjwa jana vimeisha
c.       Mkono uliovunjika juzi umepona
d.      Kalamu iliyopotea jana imeonekana

Kamusi ni muhimu kwa mtumiaji yeyote wa lugha. Taja hoja tano (5) zinazothibitisha umuhimu huu. (nectar 2012 swali la 5)

Kamusi ni kitabu cha marejesho chenye msamiati uliokusanywa kutoka kwa wazungumzaji wa jamii Fulani na kupangwa kwa utaratibu maalumu. Kasha kufafanuliwa kwa namna ambayo msomaji aweze kuelewa.

Kuna aina mbalimbali za kamusi kama vile kamusi wahidiya, thaniya na mahuruti.
UMUHIMU WA KAMUSI
i.                    Kamusi huonyesha tahajia (spellings) sahihi za maneno
ii.                  Kamusi hueleza maana (fasihi) mbalimbali za maneno
iii.                Kamusi hubainisha aina (kategoria) ya neno
iv.                Kamusi huonyesha alama ya vifupisha mbalimbali vinavyotumiwa katika lugha husika
v.                  Kamusi huongeza maarifa zaidi kuhusu lugha ya mzungumzaji.
vi.                Kamusi huonyesha Kamusi huonyesha misemo, semi, misimu, methali, mbalimbali katika lugha inayohusika.
vii.              Kamusi huonyesha matamshi sahihi ya maneno.

a.       Toa maana ya Hotuba
Hotuba ni mazungumzo yanayofanywa na mtu
Eleza ubora na dhaifu wa kuhifadhi fasihi simulizi kwa njia ya maandishi (pre form iv Dar 2011 swali la 11)

Maandishi
Uhifadhi kwa kutumia maandishi una matatizo yafuatayo
·   Fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi kuna mambo ya msingi ambayo hayawezi kuhifadhiwa katika maandishi. Mambo hayo ni yale yanayohusiana na utendaji, sauti, vitendo, kuimba na vitabia. Matokeo ya kukosekana kwa vitu hivi ni kwamba radha au athari ya kazi inayowasilishwa kupungua kabisa .
·   Katika maandishi, fasihi simulizi haina sauti. Kwa hiyo, msomaji inambidi atie sauti na mahadhi yake mwenyewe. Shuguli hii inaweza kuharibu au kufifisha ubora wa kazi hiyo.
·   Kuhifadhi fasihi simulizi katika maandishi uhusiano wa ana kwa ana kati ya fanani na hadhira hupotea. Kwa hiyo, hadhira inashiriki kwa kuona maandishi.
·   Fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi haitabadilika kulingana na wakati na mazingira. Hivyo huweza kudumu katika hali ileile kwa muda mrefu kama ilivyo fasihi andishi.
·   Fasihi simulizi ikihifadhiwa katika maandishi itakuwa na watu wachache tu yaani wale wanaojua kusoma na kuandika. Wale wasiojua kusoma na kuandika itawawia vigumu kuielewa fasihi hiyo iliyoko kwenye maandishi.
·   Ni gharama kubwa kuhifadhi masimulizi katika maandishi. Hii ni kwa sababu uandishi hutumia kalamu na karatasi. Hivyo, hapa zinahitajika pesa za kununulia kalamu na karatasi na gharama za uchapishaji.

Fafanua aina ya tungo kwa kutoa mfano mmoja kw kila tungo.
Hii ni sentensi ya kishazi huru. Kishazi hicho kinaweza kuwa na kifungu tenzi kimoja. Kifungu tenzi hicho kinaweza kuwa kitenzi kikuu au kitenzi kuu na kitenzi kisaidizi au kitenzi kisaidizi.
Mfano
Ali analima shamba
T
Musa ni mzembe
T
Mama alikuwa anapika chakula
Ts           T
Mzee alikuwa anataka kwenda kuona mpira.
Ts          Ts        Ts          T

Taja aina nne za virai na kwa kila aina tolea mfano mmoja
Kirai nomino (KN)
Kirai nomino ni kirai kinachotawaliwa na nomino au mahusiano ya nomino na neno au mafungu ya maneno. Kirai nomino huundwa na maneno yafuatayo:

-      Nomino peke yake. Mfano
Juma anasoma
Baba analima
KN

-      Nomino mbili au zaidi zinazounganishwa. Mfano:
Baba na mama wanalima
Juma na ally wanacheza mpira
KN

-      Nomino na kivumishi (N+V). mfano
Watu wawili wanalima
Mtoto Yule ni mpole
Mtu mnene ameanguka
KN

-      Kivumishi na nomino (V+N). mfano
Yule mtu anapika
Kile kiti kimevunjika
Hawa watoto ni watundu
KN

Kiwakilishi peke yake (W). Mfano
Wewe unaumwa kichwa.
Mimi ninapika chakula
Yeye anacheza mpira
KN

Eleza shughuli tano za utawala wa waingereza kabla ya uhuru zilizokuza na kueneza Kiswahili nchini Tanzania.

·         Elimu
Wakati wa Waingeleza, Kiswahili kilitumika kufundishia shule za msingi darasa la kwanza hadi la nne, na lilikuwa mojawapo hadi darasa la 12 katika shule za waafrika.

·         Vyombo vya habari
Vyombo vya habari vilivyo jishughulisha sana na kukuza na kueneza Kiswahili ni magazeti, redio nk.
Magazeti yaliyo jishughulisha sana kukuza na kueneza ni Habari za leo (1954), sauti ya pwani (1940), mwangaza (1923), kiongozi (1950), mamboleo (1923) nk.
Chombo kingine cha habari ni redio Tanganyika ilianza na matangazo kwa lugha ya Kiswahili mwaka (1950). Kwanza kama sauti ya Dar es salaam halafu baadaye kama sauti ya Tanganyika.

·         Suala la manamba
Utaratibu wa serikali za kikoloni ulikuwa ni kuzitenga sehemu Fulani kwa ajili ya vibarua wa kufanya kazi katika mashamba yao. Mawasiliano yote yalifanywa kwa Kiswahili. Kwa njia hii, Kiswahili kilikua na kueneakwa urahisi zaidi hapa nchini.

·         Suala la jeshi (KAR)
Wanajeshi walipigana katika vita mbalimbali walikuwa na nafasi ya kusafiri sehemu mbali mbali. Kwa kuwa lugha yao ya kiswahili ilikuwa ni Kiswahili, lugha hiyo iliweza kuenea kwa urahisi nchini.

·         Suala la utawala
Kama ilivyokuwa kwa wajerumani, waingereza nao katika shughuli za utawala walisisitiza matumizi ya Kiswahili. Waingereza walilazimisha kila chifu afahamu Kiswahili ili atumike katika shughuli za utawala. Vilevile wafanyakazi wote wa serikali wa ngazi za chini walilazimishwa kufahamu Kiswahili ili wapate ajira za chini serikalini.


Kwa kutumia hoja tano zenye mifano eleza kwa kifupi mchango wa wamisionar wa kikristo katika kueneza lugha ya Kiswahili nchini Tanganyika kabla ya uhuru (nectar 2013 PC swali la 10)
Wamisionari
Wamisionari walifika Pwani ya afrika mashariki kabla ya utawala wa wakoloni mashirika mbali mbali ya kidini liingia Afrika Mashariki katika nyakati tofauti.
Baadhi ya mashirika ya kidini ni :-

ü  Roho matakatifu toka ufaransa mwaka 1868
ü  White father toka ufaransa mwaka 1878
ü  Church missionary society (C.M.S) iliyoongozwa na J.C krapf.

Mchango wa missionary
a-      Waliandika sarufi ya kwanza ya Kiswahili cha kimvita katika kitabu kilichoitwa “Ouline of the Elements of Kiswahili language with specific reference to the kinika Dialect”.
b-      Walitafsiri Injili ya luka na yohana ili kuwasaidia wamisionar wengine ambao walikuwa wakiletwa Afrika mashariki.
c-      Mwaka 1905 Misheni Magila (tanga) walitoa kitabu cha historia ya wasambaa kilichoitwa “Habari za Wakilindi” na makao makuu ya shirika hili yalikuwa Mombasa.
d-     Walichapisha kitabu cha kwanza cha sarufi ya Kiswahili cha Unguja kilichoitwa “A Hand book of the Swahili language as a spoken at Zanzibar” (1870- Askof Edwrd steere)
e-      Walichapisha vitatabu vya nyimbo na kamusi za Kiswahili-kiingereza na kingereza – Kiswahili kazi ya mwanzo ya kuandaa kamusi hizo zilifanywa na Askofu Edrard Steer na kurudiwa na A. Madam na kurudiwa na F. Johnson
f-       Walichapisha magazeti, Magazeti hayo ni masimulizi (1888). Habari za  mwezi (1976) Pwani na bara (1910).
g-      Walichapisha kamusi ya “A Standrd English-swahili Dictionary na Swahili-English Dictionary ambazo zili tolewa mwaka (1939).
Vishazi tegemezi hufanya kazi ya vivumishi viwapo katika tungo. Ukweli wa kauli hiyo kwa kutumia mifano mine ya sentensi. (nectar Pc 2013 swali la 6).
Jibu
i.        Kishazi tegemezi (K/Tg)
Ni kishazi kinachotawaliwa na  kitenzi kisaidizi ambacho muundo wake hukifanya kutegemea kitenzi cha kishazi huru ili kuweza kutoa ujumbe ulio kusudiwa. Kishazi tegemezi peke yake hakitoi ujumbe unaojitosheleza.
Mfano
Mwalimu aliyefundisha darasani.
Kitabu kilichopotea juzi.

SIFA ZA KISHAZI TEGEMEZI.
a.       Kishazi tegemezi hakiwezi kutoa maana kamili ikiwa  haijafuatana na kishazi huru
Mfano
Kisichana anayecheza uwanjani
Mbwa aliyekamata paka.
b.      Kishazi tegemezi kinaweza kuondolewa katika sentensi bila kuharibu maana ya sentensi
Mfano
Mbwa aliyekichaa mwogope
Sentensi hii inaweza kuondolewa kishazi tegemezi tegemezi “Aliyepata kichaa” ikawa mbwa mwogope”
c.       Vishazi tegemezi huweza kutambuliwa kwa kuwepo vishazi kama vile “Ingawa, kwamba, ili, kwa sababu, ambate, ambacho nk.
Mfano
Kijana ambaye anasoma atakuja
Dada huyu hapiki kwakuwa ameshiba.

NAMNA VISHAZI TEGEMEZI VINAVYOFANYA KAZI KAMA VIVUMISHI VIWAPO KATIKA TUNGO
i.                    Soko lililoungua jana limesafishwa.
K/Tg (v)
ii.                  Kisu kilichonunuliwa jana kimepotea
K/Tg (v)
iii.                Aliyekuwa mwalimu mkuu wetu amesafiri.
K/Tg (v)
iv.                Walioandamana barabarani wamefukuzwa na mlinzi.
K/Tg (v)

Kwa kutumia mifano, Onyesha jinsi shughuli za dini, utawala, biashara na elimu zinazokuza na kueneza lugha ya Kiswahili nchini Tanzania (nectar 2012 swali la 10)
Utawala
Shughuli zote za utawala hapa nchini Tanzania kama vile ofisini, bungeni, mahakamani, shuleni nk. Hutumia lugha ya Kiswahili kama lugha ya mawasiliano. Hivyo shughuli za utawala zinasaidia sana katika ukuaji na uenezaji wa Kiswahili hapa nchini.
Dini
Dini zote yaani ukristo na uislam zimesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza na kueneza Kiswahili kwa kiasi kikubwa Tanzania tangu kipindi cha uhuru mpaka sasa. Ukristo na uislam huendesha shughuli na mahubili yake kwa lugha ya Kiswahili hivyo huchangia sana kuku na kueneza Kiswahili hapa nchini.
Biashara
Shughuli na misafara mbalimbali ya kibiashara katika sehemu mbalimbali hapa nchini husaidia sana kukuza na kueneza Kiswahili katika sehemu mbalimbali za ndani ya Tanzania.
Elimu
Nchini Tanzania Kiswahili hutumika kufundishia Elimu ya msingi yaani darasa la wanza mpaka la saba na secondary Kiswahili wanasoma kama somo. Hali hii imesaidia kukuza na kueneza Kiswahili nchini Tanzania.
Kwa ujumla dini, utawala, biashara, elimu zimesaidia sana kukuza Kiswahili nchini Tanzania.
Eleza tofauti za msingi mbili zilizopo kati ya kirai na kishazi. Toa mifano miwili kwa kila tofauti. (nectar 2010 swali la 10)
Tofauti
*      Maana, kirai ni kipashio cha kimuundo chenye neno moja au zaidi ambacho hakina muundo wa kiima kiarifu. Lakini kishazi ni tungo yenye kitenzi ambacho chaweza kujitosheleza na kukamilisha ujumbe uliokusudiwa na mzungumzaji au kuwa na kitenzi kisichoweza kujitegemea mwenyewe.
Mfano    Mwanafunzi anacheza mpira” (kishazi) hiki kinajitosheleza kwani kinakamisha ujumbe uliokusudiwa na mzungumzaji.
“mwanafunzi anayecheza mpira” (kishazi) hiki hakijitoshelezi kwani hakikamiliki ujumbe)
*      Aina, Kirai kimegawanyika katika aina nne ambazo ni kirai nomino, kirai kielezi, kirai kivumishi, na kirai kitenzi. Lakini kishazi kimegawanyika katika aina mbili ambazo ni kishazi huru (K/Hr) na kishazi tegemezi (K/Tg).
18.Eleza tofauti kati ya hotuba na risara. Andika Risala huhusu maji ni uhai.
a.      Toa hotuba ya maana
Hotuba ni mazungumzo yanayofanywa na mtu au watu kuhusu. Hotuba inaweza kutolewa kutolewa na waalimu kwa wanafunzi, wanasiasa kwa raia, ama wahuburi kwa waumini.

b.      Eleza kwa ufasaha sifa nne hotuba nzuri.
i.                    Hotuba nzuri lazima iwe na sehemu kuu tatu yaani Mwanzo, kati na mwisho.
ii.                  Hotuba nzuri ni lazima izungumzie ukweli wa jambo.
iii.                Hotuba nzuri ni lazima iendane na Muktadha maalum.
iv.                Mzungumzaji wa hotuba nzuri ni lazima azungumze kwa nidhamu.

Hotuba ni maelezo ambayo huolewa mbele za watu. Hotuba hutolewa kama vile kutaka kuhimiza kazi, kufanya kampeni, au kutoa taarifa kwa watu.
Risala ni hotuba fupi inayosomwa mbele ya kiongozi kwa niaba ya kundi Fulani la watu ili kutoa maelezo kuhusu kundi hilo kwa kiongozi. Mfano risala inaweza kusomwa na wahitimu mbela ya mgeni rasmi.
RISALA
Ndugu wananchi mabibii na mabwana. Ninayo furaha kubwa kuzungumza nanyi  siku hii ya leo, kwa kifupi ni lengo la ujio wangu na kuwaita hapa ni kutoa taarifa ya matumizi ya maji kwani “Maji ni uhai”
Ndugu wananchi,nimepata taarifa kutoka kwa viongozi wenu na watu mbalimbali kuhusu watu kutumia maji vibaya pasipo sababu maalum na kuharibu vyanzo vya maji.Mfano, baadhi yetu wanalima kandokando yam to, wanakata miti ovyo hivyo husababisha mvua kuwa kidogo katika kijiji chetu. Mvua ikikosekana je, Mazao yetu yatastawi vipi mashambani? Na mazao yakikauka shambani tunaweza kukumbwa na jangwa la njaa katika kijiji chetu.
Ndugu wananchi katika mkutano huu napenda kuwakumbusha kuwa serikali yetu immekwishaonyesha mfano kwa vitendo umuhimu wa maji.
Vijiji vingi vimekwisha pewa fedha za kuendeshea miradi mbalimbali ya maji kama vile kutengeneza mabomba, kuchimba visima vilivyojengewa na vinatoa maji safi kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya nyumbani kama vile kupikia,kuoga,kufua na mengine kadha wa kadha.
Hivyo basi ili kutunza vyanzo vyetu vya maji hatuna budi kuacha kulima kandokando ya mito na tunatakiwa kupanda miti kwa wingi hasa tukifuata sera ya ‘Panda mti Kata mti’ ili tuweze kupata mvua za kutosha.
Nina matumaini kuanzia sasa mtatekeleza haya niliyoyasema, kuanzisha miradi mbalimbali ya maji na hakika tutatunza vyanzo vyetu vya maji. Mkifanya hivyo kijiji chetu hakitakuwa na ukosefu wa maji tutakuwa na maji ya kutosha na mvua nyingi za kutosha.
Nawatakia utekelezaji mwema
Asanteni sana kwa kunisikiliza
Eleza mchango wa waarabu katika kukikuza,kukieneza na kukidumaza Kiswahili nchini Tanzania kabla ya uhuru. (nectar 2005 swali la 1).
AU
Fafanua Athari ya Waarabu katika Lugha ya Kiswahili kwa kutoa hoja nne(Necta 2011 swali 10)
Kukua kwa lugha ni hali ya kuongezeka kwa msamiati katika lugha na Kuenea kwa lugha ni jinsi lugha inavyoenea kwa watumiaji ndani na nje ya nchi au eneo husika na kufanya lugha kuwa na eneo pana.Kudumaa kwa lugha ni hali au tendo la kuifanya lugha isikue hivyo hupelekea kutokutumiwa mara kwa mara na kushuka kiwango kutoka ilichokuwa nacho (juu) hadi chini.
Kukikuza Kiswahili; Waarabu walipoingia nchini Tanzania maeneo ya Pwani ya Afrika mashariki karne ya 8, walikuta tayari wenyeji wana lugha zao za ambazo walizitumia katika mawasiliano zilijulikana kama lugha za kibantu ukijumuisha na Kiswahili.
Waarabu walichangia baadhi ya maneno katika lugha ya Kiswahili, mfano maneno kama; shikamoo, Laki, Abadi n.k hivyo kama ilivyo tabia ya lugha yeyote kukopa maneno kutoka kwenye lugha nyingine ili iwe na msamiati yakujitosheleza, hivyo kukua kwa lugha ya Kiswahili kumetokana na kukopa maneno kutoka katika lugha ya kiarabu na lugha nyingine.
Neno lenyewe Kiswahili limetokana na kiarabu ‘sahil’ (umoja) na   ‘swahil’ (wingi) lenye maana ya Pwani au Upwa.
Kukieneza Kiswahili; waarabu walitumia njia tatu katika kukieneza Kiswahili kama ifutavyo;
Biashara, waarabu  walipofika pwani ya afrika mashariki walilazimika kutumia lugha ya Kiswahili katika biashara zao kama vile, Biashara ya pembe za ndovu na biashara ya watumwa. Walitumia Kiswahili katika mawasiliano katika biashara zao na biashara hiyo ilikuwa baina ya watu wa pwani na bara, watu wa pwani walikipeleka Kiswahili bara kupitia misafara ya kibiashara na katika misafara hiyo wenyeji waliwaongoza waarabu na kuwabebea mizigo.
Dini, waarabu walilazika kutumia Kiswahili kwa sababu kilikuwa tayari kinatumiwa na wenyeji wa pwani, waarabu walijenga madrasa ambayo yalitoa mafundisho ya dini ya kiislamu kwa kutumia lugha ya Kiswahili ili waweze kueneza mahubiri yao kwakiurahisi na hivyo wakajikuta wanakisaidia kiswahili kuenea.
Kuoana, waarabu walipoingia pwani ya afrika mashariki waliwakuta wenyeji wao wakitumia lugha ya Kiswahili na kibantu kadri wavyozidi kuishi pamoja walioana na wenyeji wa pwani na iliyotumika katika mazungumzo yao ya kila siku ilikuwa ni Kiswahili.

Athari au Namna waarabu  walivyodumaza  lugha ya kiswahili
Waliingiza msamiati na istilahi nyingi za kiarabu kuliko Kiswahili hivyo waliaribu lugha
Mfano; abudu, samehe, fariji nk.
Katika mafundisho ya kidini walitumia walitumia zaidi kiarabu                                     kuliko Kiswahili mfano; Madrasa na swala kwa ujumla walitumia walitumia kiarabu
Hawakutafsiri vitabu vya kidini kwa lugha ya Kiswahili
Waarabu walidharau lugha ya Kiswahili na kuiona kama lugha ya makabwela
Waarabu walieneza Kiswahili sehemu chache tu ambazo walikuwa na malengo nazo. Walieneza Kiswahili katika vituo vya biashara tu kama Tabora na ujiji tu.

Fafanua mambo matano (5) yanayomtambulisha mtu kuwa ni mjuzi wa lugha.(Necta 2010 swali la 4)

Ujuzi wa lugha unatazamwa katika stadi kuu nne yaani kusoma,kuzungumza,kusikiliza na kuandika
Mtu anayeweza kuzungumza  na kuielewa lugha na kukidhi vema mawasiliano huitwa mjuzi wa lugha.
Mambo yanayomtambulisha mtu kuwa mjuzi wa lugha
a.      Kutambua kwa urahisi sentensi amabazo ni tata na       namna/jinsi ya kuondoa utata huo
Sentensi zifuatazo ni ni sentensi rahisi sana  na  za kawaida sana katika Kiswahili,
Ally anampenda dada  yake
Mkewe anampenda Ally.
Ikiwa Sentensi hizi zitasikika bila kuwekewa mazingira yanayopasa ,Mjuzi wa Kiswahili yeyote  atatambua kuwa kila mojawapo ya sentensi hizi inaweza kueleweka kwa namna zaidi ya moja.Katika sentensi ya kwanza kuna wahusika wawili au watatu.
-Ally anampenda dada yake(wahusika 2)
-Mtu fulani ana dada,Ally anampenda dada wa mtu huyo      (wahusika 3)
Sentensi ya pili inaweza kuelewekahivi;
-Mtu Fulani ana mke,mke huyo anampenda sana Ally.(wahusika 3)
-Mtu Fulani ana mke na anampenda sana mke wake.
Utata wa sentensi hizi hautokani na tofauti za kimuundo katika sentensi hizo,kwani miundo yake inafanana na  zote zina S  K+A,yaani kiima na Kiarifu.
Hivyo mjuzi wa Lugha lazima atambua Utata uliomo katika tungo na namna ya kuondoa utata huo.
b.      Kutambua ni sauti zipi zinatumika kuunda maneno ya lugha yake na mfuatano upi unakubalika na upi haukubaliki.
Kwa mfano, ikiwa ni mmahiri wa Kiswahili atapewa neno “baba” na akaambiwa aweke sauti nyingine badala ya ile ya kwanza, haya ni baadhi ya maneno ya Kiswahili anayoweza kuunda: kaba, saba na shaba. Ikiwa itabadili sauti ya pili anaweza kupata beba na buba. Katika kuunda maneno, kuna kanuni maalum ambazo ni mmahiri wa lugha anazifahamu na anajua kuwa mifuatano Fulani inakubalika, na mengine haikubaliki kwa sababu haiwezi kuunda maneno ya Kiswahili. Hivyo, kutokana na “baba” huweza kuunda, Abba, bbaa, aabb au baab. Maarifa haya ya lugha yanamwezesha mmahiri kutambua kuwa, ingawa anaweza kufananisha sauti katika maneno tofauti ya lugha yake, si kila mahali anaweza kuzibadilisha kama tulivyofanya hapo juu katika “baba”.
c.       Kwa kutambua mfuatano sahihi wa vipashio katika maneno au sentensi za lugha yake.
Katika Kiswahili kwa mfano, sentensi zake kwa kawaida huanza na nomino ya mtenda au mtendwa na huwa na kitenzi.
Mfano
Ng’ombe anakula majani porini.
Mmahiri wa Kiswahili anayefuata kanuni ya mpangilio wa maneno anaweza kukataa sentensi hii: “mnene ng’ombe anakula majani” kwa sababu haijapa mpangilio sahihi wa maneno wa maneno katika sentensi hiyo.
d.      Kutambua tungo ambazo zinavunja/hazivunji kanuni za sarufi ya (upatanisho wa kisarufi)
Mmahiri wa kiswahili atakuwa na matatizo ya tungo zifuatazo,yaani atakuwa na wasiwasi kuwa kanuni Fulani za lugha hii imevunjwa na pia atatambua zimrvunjwa kwa namna gani.
-      Ile motto imechana kitabu chake
-      Watoto yao na baba yao wamekuja
Katika sentensi ya kwanza mmahiri wa lugha ya Kiswahili atatambua kuwa tungo hiyo inaweza kutolewa na mtu anayejifunza Kiswahili kabla hajajizatiti sawasawa katika upatamsho wa makundi tofauti ya maneno ya lugha hii.anaweza kuisahihisha sentensi hiyo hivi.
“Yule mtoto amechana kitabu chake”. Sentensi ya pili inaonekana imevujwa kanuni za juu za za lugha na mmahiri wa Kiswahili itaikataa moja kwa moja tungo hiyo, ingawaje anaweza kujaribu kuirekebisha isomeke kama:
Watoto wamekuja na baba yao
e.       Kutambua kwa urahisi kusudio la sentensi
Mmahiri wa lugha yoyote anayo maarifa yanayomwezesha kutofautisha kati ya aina ya sentensi katika lugha yake kutegemea kusudio la sentensi hiyo. Anajua, kwa mfano,ni tungo zipi za kuuliza,  aaina za maswali yanayoweza kuulizwa,pamoja na majibu yanayotegemewa. Atajua zipi ni za taarifa, za kebehi au utani. Kwa mfano, ikiwa mmahiri wa Kiswahili ataulizwa “mtoto yuko wapi?” atatambua kwa urahisi kuwa jibu lake linaweza kuwa “Amelala” ma sio “ndio”.
Lakini akiulizwa “mtoto amekwisha kula?”. Atatambua kuwa “amelala” haliwezi kuwa jibu ambapo “ndio” linaweza kuwa mojawapo ya majibu ya swali hilo.
Mmahiri wa Kiswahili pia anayo maarifa yanayompa utambuzi kuwa tungo zifuatazo hazihitaji kujibiwa kwa maneno, ila pengine kwa vitendo,kwa sababu ni tungo za utendaji” yaani zinamtaka mzungumziwa kutekeleza kusudio la tamko.
-      Tafadhali nipatie maji ya kunywa
-      Samba huyu anaunguruma, tukimbie.
Mambo (5) yanayosababisha kutokea kwa lahaja (mock 2012 Dar swali la 10)
Chanzo cha lahaja

i.                    Utengano wa watu kijografia
Msukumo wa kimazingira ndiyo chanzo cha jamii katika eneo pana zaidi. Kuna mambo mbalimbali yanayotokea na kusababisha watu wanaosema lugha moja kutengana kimahali na kimielekeo. Mambo haya ni kama vile kuongezeka kwa idadi ya watu, ukame na vita mambo haya yanalazimisha watu walioishi pamoja kuachana ili kutafuta makazi mapya yenye kuwapatia nafuu. Matokeo ya mwachano huu ni kwamba, mawasiliano ya mara kwa mara yatapungua. Kwa kuwa mawasiliano ni haba, kuna uwezekano mpano wa watu walioachana kukuza upekee wa namna Fulani katika usemaji wao. Kwa hiyo, msingi wa pekee wa usemaji au kuzuka kwa lahaja ni utengano, ama wa kijamii (kitamaduni) au wa kijografia (kimazingira).

ii.                  Utengano wa watu kitabaka
Katika jumuiya moja kunaweza kumea tabaka mbambali za watu.kila tabaka hujihisi na kujitambulisha kwa namna ya pekee japokuwa matabaka hayo huishi katika eneo moja la kijografia. Msingi wa mwachano wa kitabaka unaweza kuwa uchumi, dini, elimu au siasa. Kwa sababu ya mwachano wa kitabaka, mawasiliano ya mara kwa mara baina ya watu na tabaka mbalimbali hupungua. Mawasiliano ya mara kwa mara yakipungua, nafasi ya kuchipuza upekee hata katika usemaji hupanuka. Hivi ndivyo vianavyo vipengele vya upekee wa usemi vifungamanavyo na tabaka. Vipengele hivi havionekani au havipatikani kwa urahisi hata kama ni jumuia zilizoendelea sana kiuchumi. Ndio mana vigumu kusema kwamba, katika jumuia hasa za zamani za wasema-kiswahili kilikuwa na lahaja za kitabaka. Miongoni mwa wasema-kiswahili wasasa bila shaka inawezekana kuona vidokezo vya kuinukia vya lahaja ya kitabaka.
iii.                Kupita kwa wakati
iv.                 Utengano wa kiwakati ni kipengele muhimu katika kusababisha kuzuka kwa lahaja. Umbali tu hautoshi-uwe wa kijografia au kijamii au kijamii.hata baada ya wasemaji wa lugha moja kutengana kwa sababu ya hiki au kile, upekee katika usemaji hauzuki mara moja. Hutokea taratibu kadri wakati unavyopita. Kipengele cha wakati ni muhimu vilevile katika ukuzaji wa lahaja za kijamii au za kitabaka.
v.                   Kwa ujumla uzito mkubwa zaidi ya kustawi kwa lahaja unabebwa na upitaji wa wakati hasa lahaja za kijografia. Kwa mfano, tuseme kuna wana jamii lugha A. Kutoka jamii hii kikachipuka kikundi-jamii B kwa kuhama. Wakati wa kuhama na hata miezi au miaka michache baada ya kuhama wakazi wa B na A hawatakuwa tofauti. Wakazi wa B wataongea sawa na wakazi wa A. Lakini kadri wakati unavyopita ndivyo wakazi wa B watakavyochomoza na kusha tofauti za kilugha za kuwatofautisha na wa A. Kwa hiyo umbali pekee hautoshi kuelezea umeaji wa tofauti za kudumu bali lazima umbali huo upatiwe wakati. Kama wakazi wa B wasingekuwa mbali na wale wa A, tofauti ambazo zingetokea ama zingesawazishwa na mvuto wa umoja wa umoja wao na A, au zingefuata mkondo mwingine wa mabadiliko ya kiwakati. Ikumbukwe kuwa wakati tofauti zinatokea kwa wakazi wa B, tofauti nyingine hutokea hata miongoni mwa wakazi wa A. ingawa kijografia eneo la A halikugeuka, kiwakati na kimahitaji wakazi wa eneo hilo hubadilika. Kwa hiyo, hata namna yao ya kusema hubadilika.












Mpaka wakazi wa eneo B waunde jamii pekee ya kilugha, mambo huku shinani walikotoka huwa yamebadilika pia kutokana na mwachano wa wakati. Japokuwa A2 itahifadhi jina la A, na pia inawezekana, iwapo hakutatokeavurugu ya ghafla, A2 itakuwa jirani na A; hatuna budi kukiri kuwa, kuna lahaja mbili; A2 na B zilizotokana na A. ni muhimu kusisitiza jambo hili kwa sababu mara nyingi tunapata kufikiri kuwa B ni lahaja ya A bila kufikiri ni A gani inayohusika.
Kipengele cha wakati kinapaswa kushirikishwa pia katika umeaji wa lahaja za kitabaka. Tabaka haziundwi ghafla bali kwa hatua za kiwakati. Hakuna jumuiya iliyozaliwa ikiwa na wanajumuiya hujigawa vikundi vikundi kwa kadri ya kiwango cha ufanisi wa kiuchumi au kitawala, kisiasa hata kielimu. Kwa hiyo, wakati pia ni kipengele muhimu katika kueleza umeaji wa lahaja-tabaka.

Powered by Blogger.