Mtalaa wa isimu fonetiki,Fonolojia na mofolojia ya kiswahili


Mtalaa wa Isimu kinachambua kwa undani mada muhimu katika nyanja za isimu kwa jumla, fonetiki, fonelojia, na mofolojia ya Kiswahili. Dhana muhimu ambazo zimefafanuliwa ni pamoja na isimu, lugha, umilisi,foni,fonimu, alofoni, alomofu, mofimu, miongoni mwa nyingine. Dhana hizi zimefafanuliwa kwa kuzingatia kunga mahususi zilizopo katika nadharia ya Sarufi Zalishi.Bila shaka kitabu hiki kitawaf aa sana walimu na wanaf unzi wa somo la Kiswahili katika shule za sekondari, vyuo vya walimu na vyuo vikuu, ambao wamekuwa wakipata taabu sana kuyasoma masomo haya katika vitabu ambavyo havikuandikwa kwa lugha ya Kiswahili. Aidha kitabu hiki kitawanufaisha pia wapenzi wengine wa lugha ya Kiswahili ambao wanapenda kujifunza na kuielewa vizuri zaidi lugha ya Kiswahili.Kwa mantiki hii, kitabu hiki kinashiriki kutoa mchango mkubwa katika harakati za kuikuza na kuiendeleza lugha ya Kiswahili hadi ipate uwezo kamili wa kuweza kutumika si kama lugha ya mawasiliano tu bali pia kama lugha ya kufundishia katika viwango mbalimbali hadi vyuo vikuu.
Powered by Blogger.