uchambuzi


  1. 1. USIKU UTAKAPOKWISHA Na Mbunda Msokile M. Shekinyashi
  1. 2. Riwaya hii inahusu nini? • Kwa ujumla riwaya hii inahusu hali ngumu ya maisha inayowakabili watanzania wenye kipato kidogo. • Ujenzi wa wahusika, mandhari na matukio kwa ujumla vinafafanua umasikini uliokithiri. • Motifu kuu ya hadithi hii ni mahangaiko kila siku ya kutafuta kipato cha kujikimu, kupitia motifu hiyo masuala mengi yanajadiliwa; masuala ya kisiasa, kijamii, kiuchumi na hata ubinadamu.
  1. 3. Falsafa ya Mwandishi • Mwandishi wa riwaya hii anaamini kuwa hali ngumu inayowakuta wengi kwenye jamii ni zao la unyonyaji unaofanywa na wachache. Hili linajidhihirisha kupitia mhusika Goza katika fikra na mawazo yake. • Pia kwa upande mwingine mwandishi anaamini kuwa chanzo cha maovu katika jamii na mfumo mbaya wa kiuchumi unaotengeneza matabaka. Maovu kama wizi, rushwa, umalaya, utoaji wa mimba na ulevi uliokithiri. • Mwandishi pia anatumaini la maisha mazuri kwa wengi. Katika ukurasa wa 89 anamtumia mhusika Chioko na kusema: “Ulitakiwa uwe na subira na utulivu hadi pambazuko la umma ambalo lilikuwa likiingia kwa kasi kutokana na kwisha kwa usiku”
  1. 4. Msimamo wa Mwandishi • Msimamo wa mwandishi ni kwamba kuisha kwa matabaka kutajenga jamii isiyo na maovu yaliyokithiri. • Anamsimamo kwamba umma pekee ndio utakaoleta tumaini kwa watu wa kipato cha chini. • Hivyo msimamo wa mwandishi ni wa kimapinduzi.
  1. 5. Migogoro iliyojitokeza • Mgogoro wa kitabaka. Walionacho na wasionacho wameonekana kuwa katika mgogoro wa kimaslahi. • Mgogoro kati ya mgambo na walalahoi. Mgambo wametumika kama kiwakilishi cha tabaka tawala. Wamekuwa wakiwakandamiza wanyonge na kuwanyima haki ya msingi ya kujitafutia. • Mgogoro kati ya Chioko na mama yake alipokataa shule na kujichanganya katika jiji la Dar es Salaam.
  1. 6. • Mgogoro kati kondakta na abiria na miongoni mwa abilia pia: hii inadhihirisha ni kwa namna gani huduma duni za kijamii zinaweza zikawa chachu ya kukosekana kwa amani kwa watu wa tabaka la chini. • Mgogoro wa kimawzo baina ya Goza na Chioko: wawili hawa walikuwa wanapishana kimawazo juu ya namna ya kupambana na umasikini wao. Goza aliamini katika njia ya mkato lakini Chioko aliamini katika subira na nguvu ya umma. • Mgogoro wa kifikra: Chioko alikuwa na mgogoro wa kifikra. Alikwa ameshindwa kuamua juu ya ushauri wa kukimbilia Zambia alipowa na rafiki yake Goza. Alikuwa anawaza je, aende Zambia amuache Nelli au abaki na Nelli na umasikini wao?
  1. 7. Ujumbe, Nimejifunza kwamba… • Kujikwamua kiuchumi si lazima kupitia ajira. • Penzi ni kitovu cha uvivu na uzembe; Chioko ni mvivu kuingia mitaani kutafuta pesa na mzito kufanya maamuzi magumu kwa sababu ya mapenzi. • Kukosekana kwa mipango binafsi ya kimaendeleo hupelekea watu kukata tamaa. • Ujira wa dhambi ni mauti • Makundi ya marafiki wakati mwingine ni chachu ya uovu. • Kama jamii haiwezi kutambua kiini cha matatizo yetu si rahisi kuweza kutatua shida zetu. • Dhiki ikizidi sana mioyo ya binadamu huota kutu na huruma hupotea. Wewe umejifunza nini?
  1. 8. Dhamira
  1. 9. Umasikini • Ni hali ya kushindwa kujikimu katika mahitaji muhimu ya maisha ya kila siku. • Mwandishi anatumia wahusika, mandhari, matukio na matumizi ya lugha kali sana ya picha na kejeli kufafanua umasikini walionao wengi kwenye jamii yetu. • Wahusika wakuu; Goza na Chioko wanaishi kwenye mazingira magumu sana. Kupitia mahangaiko yao tunaona watu wengine wengi wanaoishi kwenye maisha magumu kadharika. • Katika ukurasa wa 29 mwandishi anapendekeza njia za kuondoa umasikini. Ni kwa njia gani unadhani umasikini unaweza ukapungua miongoni mwa watanzania wengi?
  1. 10. Kukosekana kwa makazi bora • Mandhari iliyotumiwa na mwandishi inadhihirisha kukosekana kwa makazi bora kwa wananchi. • Manzese kwa mujibu wa kitabu ni sehemu yenye makazi ya watu wa hali ya chini. Mwandishi ameyatumia maeneo hayo huku akifafanua kwa kina namna nyumba za maeneo hayo zilivyo duni. • Mhusika Chioko na Goza wanaishi katika kibanda kibovu kinachofananishwa na mbavu za mbwa. • Mhusika Nyundo naye kadhalika.
  1. 11. Tatizo la Ajira kwa Vijana • Vijana wengi hawana ajira. Mwandishi anawaangazia vijana wa kitanzania wenye nia ya kujikwamua kiuchumi lakini mfumo unawabana hata kushindwa kupata ajira ndogondogo. • Mhusika Goza na Chioko ni mfano wa vijana wengi wanaozurura mitaani kwa kukosa ajira. • Goza anazurura mitaani akipita ofisi hadi ofisi kuomba ajira lakini anaishia kukutana na vibao mlangoni vilivyoandikwa ‘HAKUNA KAZI’ • Mwandishi analijadili zaidi suala hili na kuonesha linavyopelekea ukandamizwaji wa kijinsia. Wasichana walihitajika kutoa rushwa ya ngono ili wapate ajira. Je, katika jamii yetu kuna tatizo la ajira? Wewe Umejiandaa vipi kupambana na tatizo la ajira?
  1. 12. Rushwa • Rushwa ni kitendo cha kuuza au kununua stahiki isiyo yako kwa wakati husika au isiyo yako kabisa. • Mwandishi anaijadili rushwa kupitia wahusika Goza na Chioko. Vijana hawa wanaamini kuwa ukiwa na pesa ya kuhonga hakuna kitu kitakachoshindika kwako. (uk 24) • Wanapokutana na Mgambo mitaani rushwa huwaokoa na hata wamekosa kazi kwa sababu hawana rushwa ya kuonga waajiri. Je, jamii yetu inaweza kupambana na rushwa?
  1. 13. Ukosefu wa huduma za Jamii • Huduma za jamii ni pamoja na hospitali, shule, usafiri, na nyinginezo. • Baada ya azimio la Arusha huduma za kijamii zilikuwa zikitolewa na serikali pekee. • Kwa sasa huduma hizo hutolewa na serikali kwa kusaidiana na watu au mashirika binafsi. • Katika riwaya hii mwandishi anaonesha uduni wa huduma za usafiri akiangazia zaidi baada ya azimio la Arusha. • Abiria wa UDA kutoka manzese wanakanyagana na kuumizaa kwa kugombea daladala. • Kwa upande mwingine mwandishi anaikumbusha serikali kuimarisha huduma za kijamii kwa walipakodi wao bila kubagua matabaka yao.
  1. 14. Uongozi Mbaya • Kiongozi katika jamii, taasisi, mashirika na serikali anapaswa kuwa kioo cha matendo mema kwa wale anaowaongoza na jamii kwa ujumla. • Tofauti na matarajio, viongozi wengi katika nchi yetu ni wabadhirifu, waonevu, madikteta na wafujaji wa mali za umma. • Dhana hii inasadifiwa na katibu mkuu wa kampuni ya mabomba. Kauli zake zinaashiria kiburi cha ulevi wa madaraka. • Alimwamuru dereva wake aendeshe gari kwa kasi huku akitumia mafuta ya umma.
  1. 15. Matabaka • Ni mgawanyiko wa wanajamii katika makundi kwa misingi ya kielimu, kipato na kiungozi. • Jamii yetu imegawanyika katika matabaka kadhaa. • Mwandishi amelijadili suala hili kwa kina. Anaonesha nchi moja yenye azimio moja lakini watu wake wanaishi katika dunia mbili tofauti. • Wachache wanaishi katika dunia ya raha na wengi wakiishi katika dimbwi la umasikini ,dhiki na karaha. • Katika ukurasa wa 43 mwandishi anaigawa mitaa kwa majina yanayoashiria utabaka: kuna mtaa wa SALAMA, WENYEWE, TUMAINI, MASHAKA na WASIWASI. Kwenu kuna matabaka?
  1. 16. Ulevi • Matumizi ya kileo huathiri vijana wengi. • Pombe inapendwa lakini inaathari nyingi kwa mtumiaji. Athali zinaweza kuwa za kijamii au kiafya. • Mwandishi analijadili swala hili kwa kina huku akigusa vijana kwa ukaribu. • Anamtumia Goza na Chioko kuonesha kuwa malengo mengi ya vijana hayafikiki kwa sababu ya ulevi uliokithiri. • Pombe mara nyingine hupelekea kifo. Mhusika Liteketa anakufa baada ya kunywa pombe ya Gongo. Nini athari za ulevi katika jamii yako?
  1. 17. Uhalifu • Uhalifu ni kitendo cha kuvunja sheria za nchi. • Mwandishi anaonesha uhalifu katika matukio mbalimbali. • Tukio la mwizi wa mifukoni aliyemchomolea abiria pesa yake katika UDA. • Pia tukio la Goza kuwapora watu pesa zao. • Tukio la Goza na Nyundo kuvamia nyumba ya meneja wa kampuni ya mabomba na kumuibia elfu sitini. Nafasi yako ni ipi katika kuzuia vitendo vya uharifu katika jamii yako?
  1. 18. Nafasi ya mwanamke katika jamii • Mtu anayedharaulika katika jamii. Mfano baada ya kifo cha baba yake Chioko hakumsikiliza mama yake tena. • Chombo cha starehe: uwepo wa wanawake wanaojiuza na pia vitendo vya rushwa za ngono. • Kama kitega uchumi: Goza anapomshauri Chioko kumuuza Nelle ili wapate ajira au wapate pesa za kujikimu. • kiumbe duni sana kwenye jamii; mama mwenye watoto watatu alipokuwa akinyanyasika na kondakta wa UDA. • Mshauri mzuri; alipowashauri Goza na Chioko kwenda kuanzisha miradi ya shamba. Mwanamke ananafasi gani katika jamii yako?
Powered by Blogger.