Historia ya Riwaya ya Kiswahili

Historia ya riwaya ulimwenguni haina muda mrefu sana hasa inapolinganishwa na historia ya tanzu nyingine za fasihi kama vile ushairi, tamthiliya, na fasihi simulizi. Riwaya ya Kiingereza kwa mfano, irnejitokeza hasa mnamo karne ya 18 ingawa riwaya ya kwanza inasemekana kuwa ni ya Don Quixote iliyoandikwa 1605-15. Riwaya za mwanzo kuandikwa ziliongozwa na Fielding aliyeandika vitabu vya Joseph Andrews (1742) na Tom Jones (1749); vile vile mwandishi kama Richardson alijitokeza na kuwa maarufu kwa kitabu chake cha Pamela (1749). Riwaya ya Kirusi nayo ilijitokeza zaidi wakati huo huo.
Historia ya riwaya ya Kiswahili nayo haikupishana sana na hali hiyo ya kutanguliwa na tanzu nyingine za fasihi, ingawa kwa hakika imejitokeza mapema zaidi kabla ya tamthiliya za Kiswahili. Tofauti kubwa kati ya riwaya ya Kiswahili na riwaya za Ulaya ni kwamba yenyewe imeanza kujitokeza mwishoni mwa karne ya kumi na tisa. Zaidi ya hilo, riwaya ya Kiswahili imekuwa na maendeleo tofauti kabisa hasa kwa vile imeanza kukua kutokana na hadithi zilizotokana na fasihi simulizi.
Pamoja na kutanguliwa na tanzu nyingine kama vile ushairi, ambao historia yake ni ndefu sana, historia ya riwaya, kwa haraka mno imepitia hatua tofauti nakukua kiasi ambacho hivi sasa umaarufu wake umezidi ule wa tanzu nyingine kwa klwango kikubwa sana. Ikiangaliwa katika wakati wake wa sasa, riwaya ya Kiswahili inaonckana kuwa imetajirika sana upandc wa dhamira, muundo, ujenzi wa wahusika na hata kwa idadi. Ni utanzu ambao kwa upana na undani zaidi umeweza kuzingatia nyanja tofauti za maisha kama vile uchumi, siasa, utawala na maisha ya jamii kwa jumla. Riwaya ya Kiswahili imeweza kuvuka mipaka ya nchi na hata kwenda nje ya Afrika Mashariki. Sababu za maendeleo kama hayo zitajitokeza wakati wa kujadili vipindi tofauti vya historia ya riwaya ya Kiswahili. Mojawapo ya sababu kubwa ambayo inaweza kutajwa hapa ni ongczeko la watu wanaoweza kusoma na kuandika.
Historia ya riwaya ya Kiswahili imeangaliwa katika sura tofaati na wataalamu na watafiti mbalimbali. Wapo wale ambao wameiangalia pamoja na historia ya fasihi ya Kiswahili kama vile Rollins (1983), na wapo ambao wamegusia uandishi wa hadithi za Kiswahili kama vile Balisidya N (1976), Rollins (1985), Ohly (1981), Senkoro (1977), (1989) na wengine. Kuhusu historia ya riwaya wapo wataalamu tofauti ambao wameiangalia historia hiyo katika sura tofauti. Baadhi wanaiangalia historia hiyo kuanzia mwishoni mwa karne ya kumi na tisa. Wataalamu hawa, ikiwa ni pamoja na Rajmund Ohly (1981) wanaiangalia historia ya riwaya ya Kiswahili kuanzia wakati wa Edward Steere, ambaye mwaka 1870 alikusanya simulizi za wenyeji wa Zanzibar na kuzihariri. Hadithi hizi zilikusanywa na kuandikwa kwa lugha ya Kiingereza. Wataalamu kama hawa wanaiangalia historia ya riwaya kuanzia kwenye chanzo chake na vilevile kuanzia kwenye hatua za mwanzo katika maendeleo yake. Wapo wataalamu wengine ambao wanaona kuwa historia ya riwaya ya Kiswahili ilianzia robo ya kwanza ya karne hii ambapo vitabu kama vile Mwaka katika Minyororo (Mary Sehoza: 1921) viliandikwa. Ni wakati huu ambapo wataalamu kama akina Senkoro (1976) walichangia katika hoja hiyo wakiwa wametanguliza kitabu cha James Mbotela (1934) cha Uhuru wa Watumwa kuwa ndicho kinachoweza kuchukuliwa kama mwanzo wa historia ya riwaya ya Kiswahili. Senkoro (1976:75) anadai kuwa:
... riwaya ya Kiswahili ndipo hasa ilipoanza wakati James Mbotela alipoandika Uhuru wa Watumwa. Hii ndiyo iliyokuwa riwaya ya kwanza ya Kiswahili nayo ilikuwa na mandhari ya huku huku Afrika Mashariki, wahusika walikuwa Waswahili, na maudhui yake yaliwahusu Waswahili kwa jumla, na mwandishi mwenyewe alikuwa Mswahili.
Dai hili linaweza kupambana na dai la Kezilahabi (1980) kuwa waandishi wa Kiswahili sio lazima wawe Waswahili na pia suala la Mswahili ni nani. Dai hilo kuhusu Mbotela limepingwa na Shariff (1988:18-19) ambaye haamini kuwa kazi hiyo imeandikwa hasa na Mbotela na kuwa mawazo mengi hapo sio ya Mswahili. Shariff anasema:
... lakini ukisoma kitabu hicho chenye jina lake, ni mara tu utagundua kuwa mara kwa mara maelezo yaliyokuwemo hayakuelezwa na mtu anayesema Kiswahili kuwa ni lugha yake. Utaona dhahiri kuwa mara nyingi mawazo ni ya Kiingereza ... ingawa wafasiri walichukua hadhari sana wasitambuliwe kuwa hadithi ni ya kubuni na fikira, kwanza zilipangwa kwa Kiingereza.
Wakati mawazo ya Senkoro yanaweza kuwa yamekitwa kwenye ufafanuzi wake wa riwaya ya Kiswahili, uchunguzi wa Shariffunaonyesha kuwa kufuatana na vigezo tunavyoviona kwa Senkoro riwaya ya Mbotela inaweza isistahili sifa hiyo ya kuwa riwaya ya Kiswahili. Hata hivyo Shariff hakukiri waziwazi kwamba hiyo si riwaya ya Kiswahili. Ufafanuzi wetu wa baadaye kuhusu riwaya ya Kiswahili utaweza kutoa mwanga zaidi kuhusu suala hili. Ni muhimu kufafanua riwaya ya Kiswahili ni ipi na ni nini.
Pamoja na wataalamu hao waliotajwa wa makundi hayo mawili, wapo wataalamu wengine ambao wanadai kuwa histoha ya Kiswahili imefunguliwa mlango na Shaaban Robert. Hawa ni akina Elena Bertoncini (1980:85) na Shegov (1976). Pamoja nao wachunguzi kama akina Rollins (1983) wanachangia zaidi. Hawa wameichukulia riwaya ya Kiswahili katika hatua yake ya juu kimaendeleo na kuacha pengo kubwa ambalo ndilo hasa lililoweka msingi wa kukua kwa riwaya ya Kiswahili. Na wapo wataalamu ambao wameiangalia riwaya ya Kiswahili na kuilinganisha na liwaya zmgine za Ulaya kama vile Ohly (1981:16) anavyoona kuwa riwaya ya Kiswahili ilianzia mwaka 1974 wakati Kezilahabi alipoandika Kichwamaji.
Ili kuielewa historia ya riwaya ya Kiswahili kwa upana zaidi ni muhimu kutoa ufafanuzi wa riwaya kama tutakavyoiangalia katika kazi hii na kama ambavyo ufafanuzi huo unavyokubalika na wataalamu wengine. Tofauti yake na tanzu nyingine za fasihi na uhusiano baina yake na tanzu kadhaa ni mambo muhimu ya kuzingatia.
Ili kufafanua riwaya ya Kiswahili ni nini itakuwa ni muhimu kutambua hadithi au masimulizi ni vitu gani na kuweza kuonyesha uhusiano baina ya tanzu hizi za fasihi ambazo hushabihiana sana. Tanzu hizi za fasihi zinaweza kuwa na hali ya kuchanganywa sana. Ushairi na tamthiliya ni tanzu ambazo zimetofautiana vya kutosha na hivyo hazitakuwa na umuhimu wa kujadiliwa hapa.
Riwaya ni hadithi ambayo imekitwa kwenye dhamira moja kuu. Dhamira hiyo inaweza kuwa imejengwa na dhamira kadhaa ndogo pamoja na visa tofauti. Dhamira hizo ndogo, kama vile visa, huwa vinahusiana katika kuijenga riwaya nzima. Pamoja na hayo, riwaya huwa inakuwa na wahusika ambao aghalabu ni watu wanaowakilisha matendo na maisha ya binadamu kwenye maandishi. Riwaya sio maelezo halisi ya maisha ya binadamu bali ni maelezo ya mtunzi kuhusu anavyoyaona maisha hayo, ambavyo angetaka yawe au hata ambavyo angependa yasiwe. Kwa hivyo basi, riwaya ni mchanganyiko wa ukweli wa maisha na ubunifu wa mwandishi uliojengwa kiasi cha kumfanya msomaji ahusishe hadithi hiyo na maisha halisi ya binadamu.
Ingawa riwaya na hadithi zinazotokana na simulizi zote ni hadithi, liwaya inazmgatia maisha yajamii wakati huo. Hadithi zingine zinakuwa ni mapokezi ambayo huwa na nafasi ya msimuliaji kuongeza, kubadili au kupunguza kile kilichokuwemo kwenye masimulizi ya awali. Ni hadithi ambazo zinazingatia sifa za wahusika na maadili yaliyosimuliwa kuliko dhanura zilivyojengwa au uhusiano wa visa, dhamira, lugha na wahusika wenyewe. Haya yatajitokeza kwa upana zaidi katika kuielezea riwaya ya Kiswahili. Aidha ni muhimu kutambua kuwa riwaya ni tokeo la maendeleo ya kiteknolojia ya uchapishaji, uchapaji na uandishi. Hivyo basi, mwandishi wa riwaya hana ulazima wa kuweka kumbukumbu ya hadithi yake kiwawani kama vile msimuliaji. Vile vile mwandishi anakuwa na uwezo wa kupanga na kupangua hadithiyake. La muhimu hapa ni kuzingatia pia kuwa tunapozungumzia riwaya ya Kiswahili tunamaanisha riwaya zilizoandikwa kwa lugha ya Kiswahili. Hivyo riwaya zilizotafsiriwa kwa Kiswahili zitaangaliwa tofauti katika mchango wake wa kuiendeleza riwaya ya Kiswahili na vile vile nafasi yake katika historia ya riwaya ya Kiswahili.
Mawanda ya riwaya ni mapana zaidi kuliko yale ya tanzu nyingine za fasihi. Ni utanzu ambao unaweza kujumuisha hadithi zaidi ya moja ambazo zimeunganishwa kama visa. Vile vile unaweza kuingiza masimulizi ambayo yamekitwa na kujengwa na dhamira moja kuu ndani yake zikiwemo dhamira ndogo ndogo. Riwaya huundwa kwenye hali ya mkufu utokanao na visa. Riwaya, tofauti na tanzu nyingine, inakuwa na wahusika ambao hujengwa kutokana na hali ya kimaisha ya binadamu ili kumwakilisha binadamu katika kuufikisha ujumbe wa msanii. Hata hivyo, haimaanishi kwamba hii ni aina nzuri zaidi ya kujieleza ingawa ni utanzu unaowaelezea watu kwa undani zaidi na jinsi wanavyoishi. Ikiwa na mchanganyiko wa matukio, hali, mazungumzo na majadiliano, maelezo na kauli za msanii, riwaya imejizatiti kwenye kuelezea nyanja nyingi zaidi za maisha kuliko tanzu nyingine za fasihi. Hii ni pamoja na kuonyesha hisia na maono yao, mawazo yao, nyendo na tabia zao. Iwe imekitwa kwenye matukio halisi ya kudhaniwa au ya Kutungwa. Riwaya kama kazi zote nzuri za fasihi, inaweza kusaidia Kufafanua na kutoa mambo yaliyojificha au yasiyoonekana katika maisha ya kila siku. Tofauti nyingine kati ya utanzu huu na tanzu nyingine za fasihi ni kuwa riwaya huyatoa matendo ya binadamu kwa uwazi na ukamilifu wa kutosha kuweza kumfanya binadamu ajione, ajifunze na kujikosoa. Ni utanzu ambao huweza kumsogeza zaidi msomaji kwenye chanzo cha uhalisi au ukweli wa jambo na kumpa njia ya kuwazia au kujadili jambo kwa upana zaidi. Kwa hali hiyo, utanzu huu hukidhi lengo la kumfunza binadamu mambo mengi na kwa njia nyepesi, hasa kuliko ushairi.
Tofauti na simulizi, riwaya ni hadithi zenye matukio yaliyopangwa kufuatana na muda wake kimantiki. Hadithi ambazo zinahusu maisha ya watu wanaoishi katika wakati fulani. Tukio moja linafuatiwa na tukio jingine na vilevile kuhusishwa nalo kwenye hali ambayo inakubalika kwa kuzingatia maisha na tathmini ya maisha ya wakati huo. Ili kufanikisha hayo, muundo wa riwaya unahitaji kutumia nyenzo maalum kama vile wahusika, lugha yao, visa vinavyooana na msuko wa matukio yanayolingana na kuijenga dhamira. Vyote hivi, kwa pamoja na kwa kuhusiana, vinatanda kwenye hadithi nzima ambayo inakuwa imejengwa na dhamira ndogo ndogo. Hivyo, mwandishi wa riwaya hawezi kuukana wakati maalum katika historia ya maisha anayoy- azungumzia katika msuko wake wa riwaya kama vile ambavyo fasihi simulizi inavyoweza kuukana wakati maalum na hata kutoa nafasi ya wahusika wa aina tofauti, wanyama, binadamu, miti n.k. Riwaya, pamoja na kuweza kutumia wahusika wa aina zote, inazingatia historia ya jamii ya wakati maalum.
Tukianza kuzungumzia historia ya riwaya ya Kiswahili ni muhimu kuihusisha sana na fasihi simulizi. Vhusiano huu sio wa kimuundo, ingawa muundo wa masimulizi ulichangia kwa kiasi fulani katika riwaya nyingi za mwanzo, lakini zaidi ni uhusiano uliotokana na uandikaji wa hadithi za Kiswahili. Edward Steere alipokusanya na kuhariri hadithi alizozipata kutoka kwa wakazi wa Zanzibar unaweza kuwa ndio wakati wa kwanza kuiangalia historia ya riwaya yetu. Hadithi hizi zilikuwa sio za kiriwaya bali hadithi fupi ambazo zilitokana na simulizi tofauti za jamii hiyo. Katika mkusanyiko huo hadithi maarufu kama vile “Sultan Majinuni” na 'Sultan Darai' zilikuwepo. hadithi hizi zilikuwa maarufu sana na kuwa ni njia mojawapo ya kuwahamasisha watu wengine waliojua kusoma na kuandika kuweza kupata picha ya uandishi wa hadithi. Baadaye hadithi zingine zilikusanywa na kuhaririwa na Velten. Kati ya hadithi hizo zilikuwepo hadithi ndefu kama zile za Mtoro bin Mwenyi Bakari ambazo zilijumuisha maelezo marefu kuhusu watu ambao Mwenyi Bakari alikutana nao katika safari zake, mila na desturi zao, vyakula na maisha yao. Nyingi ya hadithi hizi zilikuwa hazikuzingatia au kuyahusisha maisha ya watu wa Afrika Mashariki. Hadithi nyingi zilikuwa na ubunifu wa kinjozi usio wa dhati kwa maisha halisi ya wenyeji. Kwa hali hiyo, maadili mengi ambayo yangewafaa wanajamii yalielekea kuwa yangepokelewa kirahisi zaidi kwenye hali ya kisimulizi kuliko kimaandishi. Hivyo lengo la kuielimisha jamii lilikuwa finyu zaidi. Ni hadithi ambazo ingawa Mbughuni (1980:93) anadai kuwa serikali za kikoloni zilizichapisha kwa madhumuni ya kielimu, tukichukulia kuwa waliokuwa na uwezo wa kusoma na kuandika wakati huo hawakuwa wale wenye amali hiyo bali wageni, zilinuiwa kuwasaidia wageni hao zaidi kujua maisha ya Mwafrika. Ndio maana hadithi nyingi kati ya hizo zilipatiwa tafsiri za Kijerumani na ufafanuzi pamoja na maelezo ya ziada. Maudhui ya hadithi hizi yalikuwa ya kigeni mno kiasi ambacho yangeweza kuwaelimisha wenyeji mambo ya Uarabuni, kwani nyingi ya hadithi hizo zilikuwa na misingi ya Kiarabu. Wasomaji wachache waliokuwepo walikuwa na elimu yenye misingi ya Kiarabu au ile ya Kizungu. Kwa mfano tukiangalia hadithi ya 'Sultan Majinuni', hadithi hii ilikuwa na habari zinazohusu uvunaji wa tende, uchezaji karata n.k., vitu ambavyo havikuwa vinahusiana na maisha ya Waafrika.
Hadithi hizo fupi ziliendelea kuwepo chini ya misingi hiyo ya simulizi hadi kitabu kikubwa cha Habari za Wakilindi kilipochapishwa (1905-1907). Kitabu hiki kilikuwa na wahusika ambao walikuwa kwenye maisha na mazingira yanayolingana na yale ya riwaya ya kisasa. Muundo wake na maelezo ya hadithi hii yalizingatia watu wa mbari za Kisambaa, Kizigua na Kibondei na kama alivyoeleza zaidi Ohly (1981), ni kitabu kilichoelezea mila na desturi za watu hawa. Hatua iliyokuwa imepigwa kutoka kwenye mkusanyiko wa hadithi za Steere, na Velten hadi kufikia kwenye kitabu cha Abdallah Hemed L'Ajjemiy ni kubwa mno kwa kipindi kifupi hivyo kutoka kwenye mikusanyo ya hadithi fupi hadi kuandika riwaya hiyo. Kama hatua za namna hiyo zingeendelezwa kwa kasi hiyohiyo huenda historia ya riwaya ya Kiswahili ingekuwa na sura tofauti na vile tunavyozungumzia hapa. Hata hivyo, kwa bahati mbaya, wakoloni wa Kijerumani na hata baadaye Waingereza, hawakuipa msukumo zaidi historia ya riwaya ya Kiswahili kwa kipindi cha zaidi ya miaka kumi. Sababu mojawapo inayojitokeza ni ile ya Vita Kuu vya Kwanza vya Dunia ambavyo vilizihusisha nchi hizi mbili. Makoloni yote yalizingatia kupigana na kutetea nchi zao. Sababu nyingine, ambayo pia inahusiana na hiyo iliyotajwa ni kwamba baada ya vita, Afrika Mashariki ilitawaliwa na Waingereza. Jitihada na malengo ya Wajerumani kuhusu lugha na fasihi ya Kiswahili yalifika ukingoni baada ya kuondolewa Tanganyika. Waingereza walianza kuangalia swala hili kwa upana zaidi, yaani nje ya Tanganyika. Kwa vile waliitawala Kenya, nchi hizi mbili zilihusishwa zaidi katika uendelezaji wa Kiswahili.
Katika jitihada za kuendeleza Kiswahili, na kuhusiana na mada yetu hii, katika kuendeleza riwaya ya Kiswahili, Waingereza walitilia mkazo hadithi fupi na simulizi nyingine. Hali hii, ambayo ilikuwepo kabla ya kuandikwa Habari za Wakilindi iliendelea kwa muda mrefu hadi mwaka 1934 kama tutakavyoona mbele. Jambo la muhimu hapa ni kuwa, pamoja na kipindi hicho cha kusimama na kurudi nyuma, historia ya riwaya ya Kiswahili ilikuwa imekwishavuka kiwango cha simulizi za kinjozi na uundaji wa riwaya ulikwisha kamilika mnamo mwanzoni mwa karne ya ishirini. Hivyo, wakati kipindi cha kwanza katika historia ya riwaya ya Kiswahili kinaishia mwaka 1910, kipindi cha pili (1910-1920) ni kipindi ambacho kimeiweka historia hiyo katika hali ya kutosogea. Kipindi cha tatu, ambacho tutakianzia mwaka 1929 ni kipindi cha kurudinyuma na kusonga mbele.
Baada ya mwaka 1920 Hellier A.B. na wenzake walianzisha vijigazeti ambavyo viliandika hadithi tofauti. Hadithi hizi ziliweza kuwafikia wenyeji wachache ambao walikuwa na ujuzi wa kusoma. Wahariri wa magezeti kama vile Mambo Leo, mwalimwengu, na mengine machache walitoa hadithi kama vile 'Kibaraka', 'Sultan Zuwera', 'Asha Binfi Fulani' na nyingine nyingi. Hadithi hizi ni muhimu sana katika historia ya riwaya ya Kiswahili. Ni hadithi ambazo ziliwapa waandishi wenyeji nafasi ya kujitokeza katika uandishi wa hadithi na kujifunza kujieleza kifasihi na kifasaha. Mnamo mwaka 1921 hadithi kama vile Mwaka katika Minyororo na Tulivyoona na Tulivyofanya Uingereza viliandikwa na waandishi wenyeji wa mwanzo kama vile Sehoza na Kayamba. Mnamo mwaka 1934 ndipo James Mbotela alipojitokeza na riwaya yake maarufu ya Uhuru wa Watumwa. Riwaya hii imekuwa ndio chanzo kilichojitokeza zaidi cha kukua kwa riwaya ya Kiswahili. Hata hivyo, riwaya hii haitofautiani sana na kazi za Sehoza na Kayamba kwa upande wa hadhi ya kiriwaya na muundo wake, licha ya kwamba wahakiki wengine kama vile Shariff (1988) wanaona kwamba msaada wa wamisionari ulijitokeza sana. Tofauti yake na kazi nyingine za awali ni kwamba kitabu hiki kilikuzwa sana na wakoloni hasa kwa sababu mbili. Sababu ya kwanza ambayo inajitokeza kwenye uchunguzi ni kwamba kilikuwa kitabu ambacho kilionyesha kuwa Mwafrika alikuwa mtu duni na mtumwa ambaye maisha yake na maendeleo yake yalimtegemea sana mtu mweupe. Ni kitabu ambacho kimeonyesha jicho la Mwafrika kwa wakati huo kuhusu kutawaliwa na mawazo yake kuhusu utumwa. Mawazo haya ya mtumwa aliyeachwa huru na kupelekwa Uingereza, mawazo ambayo kwa kweli yalimdhalilisha Mwafrika na hayaridhishi yakilinganishwa na historia ya utumwa, yalionyesha zaidi ujinga wa Mwafrika kwa upande mmoja na kwa upande mwingine shukrani na kujipendekeza kwa mwandishi kwa Wazungu. Sababu ya pili ni kuwa James Mbotela mwenyewe alikuwa mchungaji wa dini aliyepata masomo yake chini ya chama cha kanisa la Kikristo. Sababu hizi zinasaidia kuelewa kwa nini riwaya hii, pamoja na kuwa haikupevuka kisanii, ilipigiwa parapanda kubwa.
Mnamo mwaka 1929 iliundwa Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki. Kamati hii, pamoja na umuhimu wake katika kuiendeleza lugha ya Kiswahili, ilikuwa na nafasi kubwa mno katika kuendeleza fasihi ya Kiswahili. Katika kamati hii aliwahi kuwemo mwanafasihi na mwandishi maarufu, hayati Shaaban Robert, lakini pamoja na hayo, ripoti ya magavana ambayo ilionyesha umuhimu wa kuwa na Kiswahili katika mashule na kuwa na lugha sanifu ambayo ingetumika katika kujieleza kifasaha na kifasihi ilikuwa ni ripoti muhimu katika maendeleo na historia ya riwaya ya Kiswahili. Mojawapo ya mafanikio ya Kamati hii ni kuanzishwa Shirika la uchapishaji wa riwaya fupi za Kiswahili na kitabu chake cha mwanzo kilikuwa mwaka 1950, kitabu kilichoitwa Mwarabu na Binti yake. Waandishi maarufu kama vile Shaaban Robert walijitokeza na kupata msukumo zaidi baada ya kuanzishwa kamati hii. Mchango wa wachapishaji kama vile Nelson na Evans Brothers ulichangia sehemu kubwa sana katika kuikuza na kuikomaza riwaya ya Kiswahili katika kipindi hiki.
Aina ya tatu ni ya Simbamwene. Aina hii ina waandishi wengi zaidi. Vijitabu vyao ni vidogovidogo, vinavyoonyesha usanii ulioharakishwa, unaoonyesha mianya ya upungufu wao, hususan wa kisanii hapa na pale na ambavyo aghalabu maudhui yao yamezibwa kwa wingu la fani kwa kutumia uhodari wa mhusika mkwezwa katika kutenda yasiyosadikika. Mifano rnizuri ya kuipitia ni Mpango (1982), Je Kisasi? (1982), Kitanzi (1984), Kivumbi Uwanjani (1978), n.k. Ni aina hii ya waandishi ambayo imeanzisha vituo vya kwao (binafsi) vya uchapishaji ili kuchapisha kazi zao ambazo, kwa kawaida, hazikuwa zikipokelewa na mashirika ya uchapishaji yenye mashiko kutokana na masuala ya kimaadili na kupwaya kwa fani na maudhui.
Hitimisho
Katika sura hii tumejaribu kuiweka riwaya ya Kiswahili katika aina kadhaa kadiri ilivyojibainisha katika maendeleo yake hadi kufikia miaka ya themanini. Hatudai kwamba kujitokeza kwa aina hizo kumekuja kwa kuandamana, yaani kwa mfuatano maalum. La hasha. Bali kujitokeza huko kumekuja kwa mchangamano na mwingiliano; ndiyo maana aina moja ya riwaya inaweza kubainisha baadhi ya sifa za aina nyingine. Hali kadhalika, aina zilizotajwa si Alfa na Omega (A na Z) ya aina ya riwaya zinazojitokeza katika fasihi ya Kiswahili, bali haya ni matokeo ya uchunguzi wa maktabani uliofanywa na mtu mmoja. Jaribio jingine la namna hiyo lingeweza kuonyesha matokeo tofauti, kidogo au sana, kutegemeana na mkabala wa mchunguzi. Hata hivyo, matokeo yaliyojitokeza katika sura hii ni kichocheo cha kuweza kuyafikia matokeo mengine, kama vile Kezilahabi anavyodokeza “....ukweli ukipambanuliwa mwanafalsafa huendelea kudadisi hadi ule ukweli ukajitanua na kufunua ukweli mwingine”. Aidha haina maana kuwa mwandishi aliyetokea kuandikia mkondo fulani atabaki kuutumikia mkondo huo wakati wote. Inawezekana kabisa pakawa na tofauti kama ile inayojibainisha kwa Abdulla alipouacha kidogo mkondo wa riwaya-pendwa yenye mawanda ya uhalifu-upelelezi akaandika Mke Mmoja Waume Watatu. Aidha katika baina ya mikondo iliyojadiliwa imejibainisha kuwa kuna 'kipindi cha mpito' ambapo mabadiliko ya kifani, kimaudhui na zaidi ya yote, kisanaa, hujitokeza wakati wote wa maendeleo ya maisha.
to previous section
Powered by Blogger.