Fasihi simulizi


Fasihi simulizi ni kazi ya sanaa inayotumia mdomo (tofauti na maandishi kama kwenye fasihi andishi) kama njia kuu maalum ya kufikisha ujumbe. Ni sehemu ya msingi ya utamaduni, na vipengele vyake vingi vinafanya kazi kama katika fasihi kwa jumla.
Katika jamii isiyo na uandishi ni wazi kuwa hakuna fasihi andishi. Hata hivyo kila jamii ina hazina ya mapokeo yapokelewayo mdomo kwa mdomo—kwa mfano utenzi, ngano au nyimbo za jadi—hivyo vyote ni sehemu za fasihi simulizi.
Hata jamii ijuayo kusoma na kuandika inaendelea kuwa na fasihi simulizi, hasa nyumbani, k.m. katika kuwasimulia watoto hadithi. Lakini mara nyingi fasihi simulizi ya jamii ijuayo kusoma na kuandika ni tofauti sana na fasihi simulizi ya jamii isiyo na uandishi, kwa vile imeathiriwa na ujuzi wa kusoma na kuandika, na mitindo ya masimulizi yake haiendi sambamba na mitindo ya masimulizi yasiyoathiriwa na uandishi.
Tanzu na vipera vya Fasihi Simulizi
Hadithi Ushairi Semi Maigizo
Ngano Mashairi Methali Matambiko
Vigano Tenzi Nahau Majigambo
Soga Tendi Misemo Mivigha
Visakale Ngonjera Mafumbo Utani
Visasili Nyimbo Vitendawili Vichekesho
Hekaya Maghani Mizungu Ngoma
Arafa

Michezo ya jukwaani



Michezo ya watoto



Ngonjera




Semi

Semi ni tungo fupi za kisanaa zitumiazo picha na tamathali kuelezea maudhui yanayobeba mafunzo ya kijamii.

Tanzu za semi

Semi ina vipera au tanzu sita ambazo ni:
  • Methali
  • Vitendawili
  • Nahau
  • Misemo
  • Mafumbo
  • Mizungu

Methali

Methali ni semi fupi zenye mpangilio maalumu wa maneno ambazo huelezea kwa muhtasari mafumbo na mawazo mazito yanayotokana na uzoefu wa kijamii.
Methali huundwa na vipande viwili vya maneno vyenye fikra yurani.Kipande cha kwanza huashilia tendo au sharti na kipannde cha pili huashilia matokeo ya tendo au sharti hilo.

Mifano ya methali

  • Mcheka kilema,hali hakija mfika.
  • Kupotea njia, ndiko kujua njia.
  • Mchelea mwana kulia, utalia wewe.
Maana ya methali hutegemea muktadha au wakati maalumu kati jamii.

Kazi za methali

Methali zina kazi nyingi katika jamii yoyote ile kama vile:
  • Kuionya jamii inayohusika au inayopewa methali hiyo.
  • Kuishauri jamii inayopewa au kutamkiwa methali hiyo.
  • Kuihiza jamii inayohusika.
  • Kukejeli mambio mbalimbali yanayofanyika ndani ya jamii husika.
Powered by Blogger.