,MABOMU YATAWALA MBAGALA,PROFESA LIPUMBA AKAMATWA,NI MAANDAMO YA CUF SOMA HAPA KUJUA




HABARI zilizotufikia mda huu zinasema Jeshi la Polisi Mkoani Dar es Salaam limetumia nguvu kwa  kurusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya wananchama cha Wananchi CUF waliokuwa kwenye maandamo wilaya ya Temeke .
Na kufanikiwa kuwatia nguvuni viongozi waandamizi wa chama cha Wananchi CUF,wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa Ibrahimu Lipumba,huku wananchi wa maeneo hayo wakiishi kwa hofu kubwa sana.
Akithibitisha kukamatwa viongozi hao pamoja na kuvunjwa kwa maandamano .Afisa Habari wa chama cha Cuf ,Bwana Silas  alipoongea na mtandao huu mda huu ambapo amesema waalianza maandamano ya Amani katika Viwanja vya temeke na kwenda mbagala , ambapo maandamano hayo yaliokuwa na lengo la kumbukumbu ya mauaji ya wanachama wao yaliofanyika  TAREHE 26 januari mwaka  2001 huko Zanzibari na Tanzania Bara,
        Bwana Silas alisema wakati wapo kwenye maandamo hayo walipofika maeneo ya Mtongani iliyopo wilaya ya Temeke ndipo Jeshi la polisi likafika na kurusha mabomu na kuwapiga wanachama wa chama hicho na kufanikiwa kuwakamata viongozi wa chama hicho,na kuwapeleke kituo kikuu cha polisi.kwa madai maandamano hayo hayana ruhusa.
Powered by Blogger.