Mlipuko wazua taharuki Tanga, mmoja ashikiiliwa

Tanga. Polisi Mkoani Tanga inamshikilia mmiliki wa banda la wazi la kuonyesha video, eneo la Amboni Kata ya Chumbageni jijini Tanga kwa mahojiano baada ya kutokea mlipuko wa kitu kinachodhaniwa ni bomu la kutengeneza kienyeji katika eneo lake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Frasser Kashai alisema kuwa tukio hilolilitokea jana usiku na mara baada ya kitu hicho kurushwa kilisababisha hofu kubwa kwa wakazi wa eneo hilo.
Alimtaja mmiliki wa banda hilo kuwa ni Evarost Kiangazi (82) ambaye anashikiliwa kwa mahojiano zaidi kwa lengo la kubaini chanzo cha tukio hilo.
Alisema mlipuko huo ulisababisha wakazi wa eneo hilo kuanza kukimbia ovyo na watu watano kati yao walijeruhiwa na kuwahishwa kwenye hospitali ya Mkoa wa Tanga ya Bombo kwa matibabu.
Aliwataja majeruhi hao Hassani Abdallah (72), Rashid Ally (45), Mrisho Abdi (29), Juma Mtoo (15) na Abdul Ismail (19), ambao wote ni wakazi wa Amboni wakiwa wamepata majeraha sehemu mbalimbali za miili yao.
Alisema kuwa baada ya majeruhi hao kupelekwa kwenye hospitali hiyo walipatiwa matibabu na kisha kuruhusiwa, isipokuwa mmoja aliyemtaja kwa jina la Hassani Abdallah (72) akiwa bado anaendelea na matibabu kwenye hospitali hiyo.
Mwingine anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo ni Ally Rashid (25) mkazi wa Amboni Mafurikio
Hata hivyo, alisema kuwa uchunguzi wa bomu hilo bado unaendelea ili kuweza kubaini ni la aina gani pamoja na kuwa lilikuwa na malengo gani kwenye eneohilo.
Polisi mkoani hapa Kijiji cha Maili Kumi wilayani Korogwe, iliwakamata watu saba kwa tuhuma za kuhusika kuweka mabomu.
yaliyokuwa yameandaliwa tayari kulipuka kwenye nyumba mbili tofauti za ibada.
Powered by Blogger.