Siku chache baada vyombo vya habari kukaririwa kuwa Ikulu inautambua mgogoro wa magereji Tegeta.


 
Siku chache baada vyombo vya habari kukaririwa kuwa Ikulu inautambua mgogoro wa magereji Tegeta.
Siku chache baada vyombo vya habari kukaririwa kuwa ikulu inautambua mgogoro wa magereji Tegeta ikieleza kushughulikiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam huku chama cha demokrasia na maendeleo Chadema kuingilia kati kupitia kurugenzi yake ya sheria mkuu wa mkoa ameeleza kujiingiza katika masuala ambayo tayari yameamriwa na mahakama zaidi ya kusimamia utekelezaji wake.
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Bw. Saidi Meck Sadiki ambaye pamoja na kueleza nia yake ya kutotaka kuongelea suala hilo katika vyombo vya habari kwa njia ya simu amesema yeye kama kiongozi lazima asimamie utekelezaji wa sheria huku viongozi wa magereji hayo wakieleza kuwa hatua hiyo inalenga kupora haki yao ya uwekezaiji uliofikia zadi ya shilingi billion 30.
 
Hata hivyo ITV ambayo imekuwa ikifuatilia sakata hilo kwa kipindi chote imafanikiwa kupata nyaraka za manispaa kubariki zoezi hilo pamoja na kuomba kubadilisha matumizi ya ardhi ya kiwanja tajwa no. 29971 kupitia mamlaka husika huku viongozi wa manispaa ya Kinondoni mara zote wakionyesha kutetea uamuzi wao tangu ilipofanya opereshenmi ya kuondoa gereji bubu mitaani kwa kuwabomolea mapema mwaka 2006 tofauti na msimamo wa ofisi ya mkuu wa mkoa.
 
Hata hivyo katika uamuzi wa kuwakabidhi eneo hilo pia ITV ilishuhudia uzinduzi rasmi wa magereji hayo uliofanywa mwaka 2010 chini ya uratibu wa ofisi ya mkoa kupitia mkuu wa wilaya Jordan Rugimbana akiwa mrithi wa ulezi wa mafundia hao zaidi elfu nne kutoka kwa muasisi wa taifa na waziri mkuu mataafu mzee Rashd Mfaume Kawawa mara bada ya afya yake kudhoofu kabla ya kupatwa na umauti.
 
Powered by Blogger.