Kikwete: Tumedhamiria kusambaratisha uasi DRC

Alitoa kauli hiyo jana alipokutana na Mjumbe Maalumu wa Rais wa Afrika Kusini na Waziri wa nchi hiyo, Mapisa-Nqakula, Ikulu mjini Zanzibar.PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amesisitiza kuwa Tanzania inayo nia ya dhati ya kukabiliana na vikundi vya uasi vinavyo vuruga amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Rais Kikwete amesema kuna watu wanaojidai kuwa na uwezo wa kusoma na kuelewa maoni na mtazamo wa Tanzania kuliko hata Tanzania yenyewe.
Alitoa kauli hiyo jana alipokutana na Mjumbe Maalumu wa Rais wa Afrika Kusini na Waziri wa nchi hiyo, Mapisa-Nqakula, Ikulu mjini Zanzibar.
“Wanadai eti Tanzania haina nia ya kukabiliana na vikundi vya uasi. Ni watu wa ajabu kabisa hawa kwa sababu Tanzania kama zilivyo, Afrika Kusini na Malawi, zina askari wake DRC chini ya Umoja wa Mataifa,” alisema Rais Kikwete.
Alisema askari wa Tanzania walianza kazi kwa kukisambaratisha kikundi cha M-23 na wako tayari kukabiliana na kikundi cha uasi cha FDLR. Alisisitiza kuwa Tanzania iko tayari kwa sababu bado majeshi yake yapo DRC na masharti ya Umoja wa Mataifa ya kushiriki katika Brigedia ya Kimataifa hayajabadilika na wala Serikali ya Tanzania haijatoa maelekezo tofauti kwa majeshi yake mbali na yale yaliyotolewa mwanzoni mwa operesheni hiyo na UN.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, wakati akiwatakia heri ya Mwaka Mpya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini katika hafla iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete alizungumzia shutuma zinazotolewa dhidi ya Tanzania kuhusiana na DRC kuwa ni za kupuuzwa.
Wakati Rais Kikwete akizungumza hayo, Jarida la News of Rwanda, juzi lilidai kuwa Tanzania haiwezi kuwashambulia waasi wa FDLR wanaofanya mashambulizi yao Mashariki mwa DRC.
Jarida hilo liliandikwa kuwa uthibitisho wa kauli yao unatokana na kupishana kwa kauli kati ya Waziri wa Mambo ya Nje ya Tanzania, Bernard Membe na Rais Kikwete.
“Viongozi hao wanatoa ujumbe tofauti kuelezea namna Tanzania inavyolishughulikia kundi la FDLR,” linasema jarida. Lilisema kauli hizo zinakinzana na kutoa picha kuwa Tanzania haina nia ya kuisaidia DRC.
“Rais anasema watakishambulia, Waziri anasema hawana nia, nani wa kuaminiwa,” limenukuliwa jarida hilo.
ti huohuo, Rais Kikwete jana aliendesha Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi kwenye ofisi ya CCM, Kisiwandui mjini Zanzibar.
Powered by Blogger.