PAPAI NI DAWA: ZIFAHAMU FAIDA KUMI NA NANE ( 18 ) ZA MTI WA MPAPAI

PAPAI NI DAWA: ZIFAHAMU FAIDA KUMI NA NANE ( 18 ) ZA MTI WA MPAPAI
Watu wengi hulitumia tunda la papai kwa sababu ya utamu wake.
Hata hivyo mbali na kuwa na ladha nzuri, tunda la papai lina faida lukuki kwa afya ya mwanadamu.
UTAJIRI WA VITAMINI
Tunda la papai lina vitamini A,B,C,D, na E jambo linalo liweka tunda hili katika kundi la matunda na vyakula vyenye utajiri mkubwa wa vitamin.
FAIDA ZA KIAFYA ZA TUNDA LA PAPAI
Tunda la papai lina faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Miongoni mwa faida hizo ni pamoja na kuwa na uwezo wa :
Mbegu za Papai
1. Kutibu tatizo la Shida ya kusaga chakula tumboni
2. Kutibu Udhaifu wa tumbo
3. Kutibu Kisukari na asthma au pumu.
4. Kutibu Kikohozi kitokacho mapafuni
Mizizi Ya Papai
5. Kutibu Kifua kikuu
6. Tunda hili huleta afya nzuri ukitumia kila siku
7. Maziwa yanayotoka katika jani lake huponya vidonda
8. Vilevile yanasaidia kutibu sehemu palipoungua moto
9. Kama hiyo haitoshi, maziwa yanayotoka katika jani la mpapai yanatibu kiungulia na Ugonjwa wa colon (njia ya haja kubwa ndani)
Majani Ya Mpapai
10. Pia yanasaidia kutofunga choo
11. Maganda ya tunda la papai yanasaidia kutibu tatizo la kuungua, vipele na saratani ya ngozi.
12. Mbegu zake zinatibu ini zikitafunwa 10 – 12 kwa siku 5.
13. Majani yake yakaushie ndani, yanatibu pumu. Inapoanza kubana yachome majani yaliyokaushwa kisha jifukize, kule kubanwa kutakisha.
14. Majani yake yanasaidia katika kutibu shinikizo la damu.
15. Papai likimenywa na kupondwa linafaa Sana katika masuala ya urembo kwani linaweza kutumika Kama vile unavyotumia lotion kulainisha uso.
16. Mbegu za papai zina uwezo wa kutibu homa. Meza mbegu za papai kiasi cha kijiko cha chakula mara 3 kwa ajili ya kutibu homa.
17. Mbegu za papai zilizokaushwa ndani kisha zikasagwa kuwa unga zinatibu malaria, tumia kijiko 1 cha chai changanya na uji, kunywa mara 3 kwa siku 5 Mgonjwa wa kifua kikuu akila matunda haya kwa muda mrefu atapona bila dawa nyingine.
18. Mizizi yake ikipondwa na kulowekwa katika maji yaliyochemshwa, lita 2 na nusu kwa dakika 15, yanatibu figo, bladder, yanazuia kutapika. Nusu kikombe cha chai kutwa mara 3 kwa siku 5.
Powered by Blogger.