HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA



Ama kwa hakika, wasanii wasanii wa Hip Hop na Bongo Fleva si kwamba wanajigamba tu kuwa wao ni wataalamu wa kutumia vina, lakini pia vina hiyo vinajidhihirisha katika tungo zao. Hebu tuangalie baadhi ya tungo kuona jinsi wasanii wanavyozingatia matumizi ya vina katika tungo zao. Tukianza na msanii Profesa Jay katika wimbo wake wa Kubwa Kuliko:
Ubeti wa 1
Yo fani ni fani muulize, Bishanga Bashaija,
Sanaa ya Bongo kwa wasanii haina faida,
Ona wenzetu Mantoni mambo safi kuku kwa mrija,
Na mimi nataka niishi kama Kadija Kadija,
Wasanii wa Bongo bado tunakufa maskini,
Nasubiri kiama changu na sijui kitafika lini,
Wazee wa serikalini semeni tatizo ni nini?
Mnataka mle jasho langu nikienda futi sita ardhini,
Hapa jasho la mtu haliliwi wala mtu haibiwi,
Jay najivinjali kama kutumia kizizi,
Machozi yananilenga nikimkumbuka mzee Nyanyusa,
Pamoja na umuhimu wake wabongo walimsusa,
Baadhi ya mafao yake wabongo wamefanya asusa,
Kwa mtu mwenye akili lazima hii itakugusa,
Tunaposema Watanzania tudumishe sanaa yetu,
Lazima mtuwekee mazingira safi ya sanaa yetu,
Marijani Rajabu tulimuita jabali la muziki,
Alifanya maajabu,alivumilia mikimikiki,
Kinachonipa ghadhabu, bwana sanaa ya Bongo hailipi,
Tofauti na chati yake, ndugu yetu amekufa na dhiki,
Sasa kipi ni kipi maana ufanisi haufanyiki,
Sababu viongozi wetu mnatamaa hauridhiki,
Wakati ni huu wa kujifunza watanzania,
Umoja wa wasanii wa bongo hiyo ndiyo njia.

Kiitikio
Ninaposema Jay kubwa kuliko,
Siko niliko ndiko liko zindiko (Yataka moyo)
Ninaposema Jay kubwa kuliko,
Siko niliko ndiko liko zindiko (Yataka moyo)
Sanaa yataka wito (yataka moyo)
Sanaa ya Bongo nzito (yataka moyo)
Sanaa ujiko mwiko (yataka moyo)
Sanaa yataka wito (yataka moyo)

Ubeti wa 2

Salamu Nicko zingilada popote roho ilipo,
Wasanii wenzako wa Bongo bado tunafanya  zindiko,
Wasalimie sana kuzimu walio hai na waliolala,
Waambie tunasuasua tu na akina Mzee Jangala,
Hardblasterz, Sikinde na Remmy Ongala,
Underground Soul  na Gangwe na Baby Stara,
Uncle Kabaino, IK pale Kimara,
OTTU Jazz na Agley Face kule Ilala,
Tunasubiri kudra za imani kwa Mungu kwa waja wake,
Tunaotafuta labda tutapata faraja zake,
Mambo si mambo yameongezeka tu matukio,
Na ajali, rushwa na UKIMWI tu ndiyo kivutio,
Sanaa imedumaa najua hiyo huwezi shangaa,
Lakini hali ya sasa ni mbaya na inatukatisha tamaa,
Soko limekuwa bovu wasanii hatuungwi mkono,
Wananchi hawana kitu kila siku wanafanya mgomo,
Kiasi wanachokipata kinaishia kwenye bia na ngono,
Na kuhusu masoko ya nje serikali imefungwa mdomo,
Mapromota wengi matapeli, ukilemaa wanakuacha feli,
Unaangua kilio, ulichotegemea kinakuwa siyo,
Wepesi kutimua mbio, wewe linakupitia fagio,
Na sasa wametuacha na kuleta wasanii wan je,
Hatimiliki ndiyo kwanza inasua sua ndani ya Bunge.

Kiitikio
Ninaposema Jay kubwa kuliko,
Siko niliko ndiko liko zindiko (Yataka moyo)
Ninaposema Jay kubwa kuliko,
Siko niliko ndiko liko zindiko (Yataka moyo)
Sanaa yataka wito (yataka moyo)
Sanaa ya Bongo nzito (yataka moyo)
Sanaa ujiko mwiko (yataka moyo)
Sanaa yataka wito (yataka moyo)

>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>
Powered by Blogger.