HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA


Na siyo bandia ka kontena lile la BOT,
Situkuzi kilicho feki kama TOT,
Mi ndio Roma ntasimama kaka KKT,
Ahsante Bongo, macho juu, Nyamongo, TBC,
Mistari yangu mitamu kama miwa ya TPC,
Na kwa hizo fomu MC utalazwa KCMC,
Kodi ya walalahoi pombe TRA,
Miili yao ndio biashara ndani ya BBA,
Fataki anatoa mikopo ndani ya TIA,
Licha ya mimba haina uhakika mpaka DNA.

Katika ubeti huu tunamuona msanii akiamua kutumia vifupisho katika kila mstari na vifupisho hivyo alivyoviteua kuvitumia vinakamilisha vina katika ubeti mzima.

Vilevile, mtindo wa wasanii kutunga na kuimba mashairi yao papo kwa papo kwa mtindo ambao wao huuita mitindo huru huku wakizangatia suala la mizani, ni ushaidi mwingine unaoonesha kuwa muziki huu unaonekana kuathiriwa na wanajadi zaidi kuliko wanausasa. Samwel na wenzake (washatajwa, uk. 63-64) wanaeleza kuwa, msanii wa Hip Hop au Bongo fleva anapotunga papo kwa papo huongozwa na fomula na hasa ile ya urari wa vina na mizani. Wanaendelea kusisitiza kuwa, fomula hii humfanya (msanii) kila mara kuhakikisha anapachika maneno ambayo yana vina. Wakimtolea mfano msanii Roma, wanatueleza kuwa katika tamasha la Epiq Nation jijini Mwanza alitoa ghani za papo kwa papo ambazo zinaonekana kuzingatia urari wa vina, kama inavyoonekana hapa chini katika ghani hizo ambap msanii ametumia vina vya ao na to ili hali mashairi hayo ameyatoa kichwani papo kwa papo;
Mwanza, msishindane na mwanamke pedeshee atamuhonga noah,
Wanaume mjitahidi ipo siku mtatoboa,
Mimi ni Rais wa ghetto,
Sina kabisa mchecheto,
Na wala sipigi punyeto,
Namiliki mademu kwa kipato,
Mwanza sema oyee kwa Epiq Nation.

Chanzo: Samwel na wenzanke (washatajwa, uk.64)

Ama kwa hakika, tukiangalia tungo za wasanii wa muziki wa Hip Hop na Bongo Fleva tutakubaliana kuwa mashairi yao kwa upande wa kuzingatia vina katika tungo zao inaelekea kuonesha kuwa wasanii wa muziki huu wanaonekana kuathiriwa sana na wanajadi.

Aidha kipengele kingine ni mizani, Abedi (keshatajwa) anafasili kuwa, mizani ni vipimo vinavyopima urefu wa kila mstari, kila silabi moja ni mizani moja. Yeye anaona shairi zuri ni lile lenye mizani16, lakini anatambua pia kuna mashairi yasiyotimiza mizani hii, hivyo anatoa maelekezo ya namna ya kuweka kina cha kati katika mashairi yenye mizani pungufu ya 16. Kupitia maelekezo haya tunaona hata wasanii wa Bongo Fleva na Hiphop wanazingatia idadi ya mizani na katika utunzi wao japo hawafuati mizani 16. Mara nyingi wamekuwa wakitumia mizani pungufu au zaidi ya 16. Mfano katika wimbo wa profesa J ametumia mizani 12. Katika wimbo wake wa kubwa kuliko hasa katika kiitikio kama inavyojionesha katika ubeti ufuatao;
   ‘ninaposema jay kubwa kuliko,
    Siko niliko ndiko liko zinduko,
    Ninaposema jay kubwa kuliko

Tukichunguza mashairi ya Hip Hop na Bongo Fleva tutaona kuwa hawazingatii ya nane nane kila kipande cha mstari ili kupata mizani 16, mara nyingi mashairi yao mizani huweza kutofautiana kati ya mstari mmoja na mstari mwingine katika ubeti mmoja lakini suala la urari wa vina huzingatiwa kama inavyojionesha katika mfano tulioutoa hapo juu, ambapo kila mstari unaishia na kina cha ko. Tukiangalia pia mfano ufuatao kutoka kwa msanii Ali Kiba katika wimbo wake wa Mwana:
Ubeti wa kwanza
Mali ni nyingi nyumbani, kipi kilichokukimbiza,
Ona babiyo mamiyo, wote wanakulilia,
Mtoto peke yako nyumbani, kipi kimekukimbiza,
Ona babiyo mamiyo, wote wanakulilia,
Ndani ya Dar Es Salaama, ulikuja bure,
Tena kimwana kimwana, hujui kuchuna,
Na zile lawama, za wallokuzoeza,
Ulikuja jana na leo tofauti sana,
Tena bora yule wa jana wa leo tofauti sana,
Dakikia mbili mbele nyuma, kichwa kinauma,
Mbona unawatesa sana,
Mbona unajitesa sana,
Ndani ya Dar Es Salaam mambo matamu hakukuhisha hamu,
We bado mtoto kwa mama hujayajua mengi,
Mwenda tezi na omo marejeo ngamani,
Amesema sana mama, dunia tambara bovu,
Kuna asali na shubiri, ujana giza na nuru,
We mwana wewe mwana, mwana jeuri sana,
Ulichokifuata hukupaa, umekosa ulivyoacha,
Kwa baba yako mwana, na mama yako mwana,
Kwa vicheche ulivyotaka, na vingi ulivyoacha,

Tukiangalia wimbo huu, tutaona kuwa mizani haijazingatiwa sana, kwani kila mstari unaweza kuwa na mizani tofauti na mstari mwingine ndani ya ubeti huo huo. Kwa mfano mstari wa kwanza una mizani 17 kipande cha kwanza cha mstari kina mizani 8 na kipande cha pili kina mizani 9, wakati mstari wa pili una mizani 16, kipande cha kwanza una mizani 8 na kipande cha pili una mizani 8. Lakini pamoja na tofauti hiyo, ya mizani, urari wa vina unazingatiwa kama inavyoonekana katika kila beti, vina vya za, a, na, cha vimetawala.

>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>
Powered by Blogger.