MITAZAMO (NADHARIA) MBALIMBALI JUU YA SANAA ZA MAONYESHO


Tukizingatia nadharia hii huenda tukaamini kuwa sanaa za maonyesho ni tamthilia tu. Kitu ambacho kinaleta mashaka kidogo.  Inafahamika kuwa tamthilia ni utanzu ulioletwa na wakoloni hapa Afrika Mashariki. Kwa hiyo, kuamini nadharia hii ni sawa na kusema kuwa hakuna sanaa za maonyesho zenye asili ya hapa Tanzania ama Afrika Mashariki. Au kwa upande mwingine ni sawa na kusema kuwa kabla ya mkoloni kutuletea tamthilia sisi tulikuwa hatuna sanaa za maonyesho zetu wenyewe. Wazo hili si kweli na ni wazo potofu.   (Taz. Mhando &Balisidya 1976).

Kimsingi mtazamo huu unatokana na fasili ya sanaa za maonyesho inayodai kuwa sanaa za maonyesho ni kitendo chochote chenye sifa za mchezo, mchezaji, uwanja wa kuchezea na watazamaji. Ingawaje ufafanuzi huu ni sawa lakini hata hivyo mtazamo huu ni dhaifu kwani ulitokana na watu waliokuwa wakifafanua sanaa za maonyesho wakiegemea zaidi kwa zile za utamaduni wa kizungu. Ufafanuzi huu haukuzifikiria sanaa za maonyesho zenye ya utamaduni wa Kitanzania.

Dosari kubwa katika ufafanuzi huu imo katika neno mchezo (play). Neno hili lina maana duni likilinganishwa na hali na umuhimu wa sanaa za maonyesho zenye asili ya Kitanzania/Kiafrika. Tukichukua kwa mfano unyago, jando, kusalia mizimu, au masimulizi ya hadithi, ambayo ni mifano ya sanaa za maonyesho zenye asili ya Kitanzania, tunakuta zile sifa zote nne zipo. Isipokuwa tunajua kuwa shughuli zote hizi siyo mchezo na umuhimu wao hauruhusu hata kidogo kuingiza neno mchezo. Shughuli hizi zina maana muhimu ambayo inahusu maisha ya binadamu katika jamii yake. Ni shughuli zinazobeba wazo maalum lenye lengo la kujenga utu wa mwanajamii. Basi vipi tuseme shughuli hizi zina sifa ya mchezo?  Wenzetu wazungu wanaridhika na neno hili kwa  sababu sanaa za maonyesho za utamaduni wao mara nyingi zinafanywa kwa masihara tu. Sanaa za maonyesho zao zaidi ni kwa madhumuni ya kujiburudisha au pengine kutafuta kipato. Lakini kila aina ya sanaa za maonyesho ya Kitanzania ina dhana fulani ndani yake, kwa mfano dhana kuhusu maana ya maisha, kuhusu utekelezaji wa madaraka ya kiutu uzima,  kuhusu ushujaa, mafunzo ya historia ya jamii n.k.
>>>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>
Powered by Blogger.