FAIDA ZA KULA EMBE KIAFYA:


FAIDA ZA KULA EMBE KIAFYA:
EMBE ni tunda la mwembe ambao ni mti wenye ukubwa wa wastani una rangi ya kijani kibichi kila wakati.
Kabla ya kuzaliwa embe mti huu huwa na maua ya rangi ya waridi hadi nyeupe katika vishada vya maua na msimu wake ni kati ya Desemba hadi Aprili.
Tunda la embe umbo lake hutofautiana, mengi yao huwa aidha na rangi ya kijani, manjano ama nyekundu.
Embe inaweza kuiva ikiwa mtini lakini ili kuzuia uharibifu kutoka kwa ndege na popo ambao hula tunda hili, wakulima huamua huvuna mara tu inapokomaa kwa kuangusha ikiwa bado haijaiva.
Utagundua kuwa embe imekomaa kwa kuiangalia rangi kwani hubadilika kutoka rangi ya kijani hadi ya manjano au nyekundu.
Kuna aina nyingi za embe kama vile embe dodo, embe mali, embe bolibo, embe nuka, embe kidney, embe Julie Manzano na kadhalika.
Watu wengi hupenda kula embe ikiwa imeiva lakini ulaji wake ikiwa bado mbichi ni jambo muhimu sana kiafya.
Nyama ya tunda hili ni tamu pia ina virutubisho kwani ni chanzo cha upatikanaji wa vitamini A na C mwilini mwa binadamu.
Embe ina kiasi cha wastani cha thiamin na niacin na asilimia 10 hadi 20 ya sukari inayosaidia mwili iwapo mtu anakula tunda hili.
Maembe pia yanaweza kugandishwa, kukaushwa kwa jua na kuweza kutumika siku nyingi zijazo.
Maembe pia yanaweza kuwekwa kwenye makopo viwandani ama kupikwa katika jemu na watu kutumia baada ya muda fulani.
Lakini embe pia hutumika kutengeneza jeli, pai, achari kama Mengo pickle ambayo hupendwa na watu wengi na kwa hakika huwa ghali kutokana na tunda lenyewe kupendwa na watu.
Kuna watengenezaji wa aiskrimu huamua kutumia tunda hili kutengeneza na wengi hupenda kutumia kutokana na harufu yake nzuri.
Watu wengi hutumia tunda hili kutengeneza juisi ama ikiwa yenyewe tu au kwa kuchanganya na matunda mengine.
Matunda ambayo hutumika kuchanganya na embe ni ndizi, nanasi, parachichi, zabibu, papai na kadhalika.
Kuna wengine hutumia mchanganyiko huo kwa kula bila kusagwa na wengine huamua kusaga na kugeuza kuwa juisi ambayo inaweza kutumika bila kuongeza sukari kwa kuwa matunda hayo yote yana sukari ndani yake.
Powered by Blogger.