HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA

Historia ya muziki wa kizazi kipya (Hip Hop na Bongo Fleva)
Muziki wa Hip Hop tunaarifiwa kuwa uliasisiwa na Wamarekani wenye asili ya Kiafrika katika mji wa Bronx huko New York katika miaka ya 1970 (Omari, keshatajwa:1). Nchini Tanzania unakadiliwa kuwa uliingia miaka ya 1980 Omari (keshatajwa), Mwanjoka (2011), Mbilinyi (keshatajwa), Reuster-Jahn (2014). Katika kipindi hiki vijana wengi hususani wale waliotoka katika familia zenye uwezo walianza kuimba mashairi (muziki) ya rap kwa kuiga nyimbo zilizokuwa zikiimbwa na wanamuziki wa Marekani wakati huo. Chachage aliwahi kuandika kuwa, katika mazingira hayo ndipo baadhi ya vijana waliokuwa wakijitambulisha kwa kusikiliza muziki wa  Reggae  wa Bob Marley na kucheza  ‘Break Dance’  katika miaka ya 1980, ili kujinusuru na kuyasahau matatizo yao, walipoanza kujipambanua na muziki wa  Hip Hop (Bongo Fleva). Mwanzoni ulikuwa ni muziki ulioambatana na kuiga kisisisi muziki huo. Kuiga kisisisi maana yake kuiga kitu kama kilivyo.

Madai haya ya kuiga muzuki wa Marekani yanaungwa mkono na Mwanjoka (keshatajwa, 8) anaposema,“Mbali na kuiga nyimbo, vijana hao wa Tanzania waliingiwa na mapenzi ya ndani  zaidi na muziki huo hata kujikuta wakiiga mavazi, mitindo ya nywele, mienendo hadi kuongea toka kwa wanamuziki hao wa Marekani na Ulaya.”

Hivyo tunaona kuwa wasanii wa Hip Hop na Bongo Fleva mwanzoni walianza kuimba kwa kunakiri na kukariri mashairi ya wasanii hao wa nje na hata midundo waliyokuwa wanaitumia ilikuwa ni midundo hiyo hiyo ya wasanii wa nje. Mbilinyi (keshatajwa, 32) anaongezea kwa kusema kuwa, “Kama kulitokea na aliyerap kwa kutumia lugha ya Kiswahili basi alitumia flow (kutiririka) ya nyimbo za mamtoni zilizokuwa maarufu kama ambavyo alikuwa anafanya mkongwe Saleh Jabir katika nyimbo kama Ice Ice Baby ya Vanilla Ice na OPP ya Naught by Nature ilikuwa ndiyo staili ya kipindi hicho.” Ufafanuzi katika mabano ni wetu.

Lakini baadaye wasanii wakaachana na uigaji wa muziki wa kimagharibi na kuanza kutunga nyimbo zao binafsi kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza jambo linaloendelea mpaka sasa ingawa tungo za Kiswahili ndiyo hupewa nafasi kubwa. Na msanii wa kwanza kabisa kuanza kuandika na kuimba kwa Kiswahili alikuwa ni Salehe Jabir ambaye kwanza tunaelezwa kuwa alianza kubadilisha nyimbo za Kiingereza kwa kutumia Kiswahili zilizotamba kipindi hicho na baadaye akaanza kutunga nyimbo zake mwenyewe. Hapo ndipo ikachochea wasanii wengi kuona kumbe inawezekana kurap kwa Kiswahili ndiyo nao wakaanza kujitokeza kutunga na kuimba kwa lugha ya Kiswahili, Mbilinyi (keshatajwa) na Mwanjoka (Keshatajwa).
Baadhi ya wasanii na makundi ya Hip Hop wanaotajwa kuwa ni waasisi wa muziki huu walikuwa ni, Fresh XE, BBG, Adili Kumbuka, Salehe Jabir, KBC, Samia X, The BIG, Rymson, 2 proud (Sugu), makundi ni kama vile, Kwanza Unit, Deplowmatz
>>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>>>>
Powered by Blogger.