HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA


HardBlasterz, Gang Stars With Matatizo (GWM), Wagumu Weusi Asilia, Young Da Mob, Afro Reign, Jungle Crewz Pose, Bantu Pound, Hardcore unit kwa kutaja machache. Wasanii na makundi ya kuimba (Bongo Fleva) ni kama vile, Mawingu Band, Lady Jay Dee, Stara Thomas, Unique Sisters, Nurueli, 4Kruz kwa kutaja wachache Mhagama (keshatajwa), Mbilinyi (keshatajwa), Mwanjoka (keshatajwa).
Aidha kabla hatujaingia katika kiini cha mjadala wetu, tuwaangalie kwanza wanajadi na wanausasa ni mambo gani wanayoyasimamia na kuyasisitiza katika utungaji wa mashairi. Ushairi wa kijadi ni ushairi unaozingatia urari wa vina na mizani kuwa ndiyo  roho na uti wa mgongo wa mashairi ya Kiswahili kwao hawataki kukiri kuwa mashairi yalaiyotungwa katika mtiririko (masivina) ni mashairi (Mulokozi na Kahigi, 1979:1) kwa maana hiyo kwa pamoja na vipengele vingine katika ushairi wa jadi ni kuzingatia vina kama anavyotuambia Abeid (1952:viii), “Neno moja tukumbuke katika utungaji, nalo ni hili ya kuwa mawazo ya mtungaji yazue vina, siyo vina kuzua mawazo.”

Madai haya yanaonekana kuungwa mkono na wanajadi wengine kama vile, Chirahdin, Mayoka, Kandoro, Al-amin Mazrui na Ibrahim Shariff kuwa vina na urari wa mizani ndiyo vitambulisho vya ushairi wa Kiswahili (Mulokozi na Kahigi, 1979:11). Jambo la msingi hapa ni kuwa wanajadi wanakumbatia sana suala la vina na mizani katika tungo za mashairi. Ili kuwa na shairi zuri, mwanajadi Sheikh Amri Abeid anataja mambo manne muhimu yanayopaswa kuzingatiwa katika ushairi ambayo ni, mizani, vina, kituo na kujitosheleza. Wanajadi wengine wanaotaja mambo muhimu yanayotakiwa kuzingatiwa katika ushairi ni pamoja na, Massamba (1983) anataja vina, mizani, kituo, muwala, Kibao (1983) naye anataja, mizani, vina, urari, muwala, utoshelevu na kuwa na maana wakati Komba (1977) anataja, mizani, vina, kituo na utoshelevu. Ama kwa hakika tukiwachunguza wataalamu hao tutagundua kuwa, wanachosisitiza shairi lenye sifa za ujadi linatakiwa kuzingatia vipengele vifuatavyo, Mizani, vina, kituo na kujitosheleza.

Kwa upande wao, wanausasa wanaona shairi si lazima lifuate urari wa vina na mizani, Mathalani, Mulokozi na Kahigi (1982;25) wanasema ushairi ni sanaaa inayopambanuliwa kwa mpangilio maalum wa maneno fasaha na yenye muwala kwa lugha ya mkato, picha, sitiari au ishara katika usemi maandishi au mahadhi ya nyimbo, ili kuleta wazo au mawazo, kufunza au kueleza tukio au hisi fulani kuhusu maisha au mazingira ya binadamu kwa njia inayogusa moyo. Kwa maoni yao wanausasa wanaona kuwa shairi ni sanaa yenye mpangilio mzuri wa maneno, lugha ya mkato na matumizi mengine ya lugha ili kutoa mawazo wao hawasisitizi juu ya kuzingatia urari wa vina na mizani kama wafanyavyo wanajadi.
 Mahenge inatupa mwanga kuhusiana na maana ya Hip Hop ambayo kwa kiasi kikubwa tunakubaliana nayo lakini dai la kusema usimuliaji au usemaji unapangwa kivina kwa kufuata mdundo wa ala za muziki ambao ulisharekediwa si sahihi kwani sasa hivi wasanii wengi wa Hip Hop wanaimba juu ya midundo ya muziki ambayo haijarekodiwa vyombo vya muziki vinapigwa sambamba na wao wakiimba na wakati mwingine hurap kwa mtindo unaojulikana kama mitindo huru yaani kutoa mashairi ya papo kwa papo kwa kufuata midundo ya muziki inayopigwa au bila kuwepo kwa midundo ya miziki yaani akapela.

>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>
Powered by Blogger.