HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA

Wasanii wengi wa bongo bado tunaishi kwenye ujima,
Kiasi tunachotafuta wenye choyo wanatuzima,
Siyo lazima tupate tanuzi la kuendesha benzi au bima,
Tunachanga tuthaminiwe watanzania tupate heshima,
Nje ya mipaka, tufanye kile tunachokitaka,
Sanaa iwe ajira tuepushe wimbi la vibaka,
Heri yako Irene Ngoi milioni hazikupigi chenga,
Nakutakia kila la heri popote unapokwenda,
Si Mr. Teacher, GK wala Mzee Jongo,
Anayelidhika na maslahi ya msanii wa hapa bongo,
Yo Solo Thang, Simple X hata Onyango,
Yo Mika Mwamba, Mr Paul sina kinyongo,
Masoud Kipanya,  nathamini unachokifanya,
Oscar Makoye dodosa kusanya kusanya,
Yo African Stars, Vijana Jazz, Tatu Nane,
Sisi wote ni wasanii kwahiyo tushirikiane,
Tusaidiane kwenye pilika pilika za fani sa tuungane,
Siyo mizengwe kibao, tuwe pamoja tusitosane,
Mr 2, KU, Fid Q, TBT Crew,TQ,
Fanya mavitu kwani wakati ndiyo huu,
Soggy Doggy, Mad Brain, Eazy Braze, Hard crew,
Heyo, X Plastaz, Juma Nature na Manzese Crew,
Tuff B, Sos B, Killa B, Stieve B, Master T, Caz T,

Tukiangalia shairi hili la Profesa Jay, tunaona kuwa katika ubeti wa kwanza vina vya, a, ni,i,sa,tu, kin a ia na katika ubeti wa pili tunaona kuwa vina vya, o,la,ra,ke,a,mo,no na e wakati katika ubeti wa tatu vina vya ma,ka,nga,ngo,nya,ne na u vinajitokeza.

Vilevile tukimtumia msanii mwingine Diamond Platznum katika wimbo wake wa Kesho tunaona pia matumizi ya vina yanazingatiwa, hebu tuangalie wimbo wenyewe;
Kiitikio
Minataka kesho twende nikupeleke nyumbani
Nataka kesho twende ukamuone mama x2
Ubeti wa 1.
Kwanza kabisa ntanyonga Tai
T"shirt na Jeans ntatupa kidogo..
Unite Nasibu usiniite Dai
Asije kukuona muhuni akapandisha Mbogo...
Naukifika uagize Chai
Savanna Takila uzipe kisogo...
Kuhusu mavazi kimini haifai
Tupia pendeza ila za Hekima Logo...
 Even though wanaponda eti we ni kicheche
Waambie ndoo chaguo langu sasa wanicheke x2
Kiitikio
Minataka kesho twende nikupeleke nyumbani
Nataka kesho twende ukamuone mama x2

Ubeti wa 2.

Usilete swaga za Nainai
Ukanyoa kiduku kama Moze Iyobo..
Eti shoping twende Tai
wakati Dadaangu anaduka kigogo..
Ukikuta Nguna usikatae
we zuga unapenda hata kama wa Muhogo..
Kuhusu kabila mbona Sadai
Mama angu hana noma hata kama Mgogo
 Even though wanaponda eti we ni kicheche
Waambie ndoo chaguo langu sasa wanicheke x2
Vina vinavyojitokeza katika ubeti wa kwanza wa wimbo huu ni, ai,go na e na katika ubeti wa pili vina vinavyojitokeza ni ai,o,go na e.
Tukimtumia msanii mwingine Joh Makini katika wimbo wake wa Najiona Mimi (I see me) tunaona pia matumizi ya vina yanapewa kipaumbele kama tulivyoona kwa wasanii wengine, hebu tuangalie shairi lenyewe:

Ubeti wa 1.
Namuona Baba Mmoja Tu Juu Najiona Mimi
Namuona Mama Mmoja Tu Chini Najiona Mimi
Naziona chuki zao upendo najiona mimi
Mabegani Msalaba Wa Ndoto Mtoto Wa Mageto
Ziwe Kweli Zisiishe Kisongo Segerea Ya Keko
Juu Ya Ukweli Ndo Nifie Steven Biko
Najiona Mimi Yanapoanzia Mabadiliko
Fikra Potofu Badili Hizo
Ndoto Sio Kuzikalia Skani Mkilialia
Ndoto Ni Kuamka Mbio Kuzikimbilia
Mziki Una Hela Mwanzo Unapoingia
Hela Nyingi Zipo Mwishoni Hutozifikia For Real
Hapo Kati Kuna Kisu Siuna Jambia
Wale Papa Wabakaji Mpira Hawatotumia
Ulikuwa Mpaka Powder Utapakwa Rukaria
Na Usiambie Mtu Labda Yesu Na Maria
Baba Nikiwa Club Nakunywa Local Bia
Naomba Mziki Unaopigwa Uwe Ni Local Pia
Nyeusi Kwenye T-shirt Ndo Logo Gear
Makini Joh Na Bado Flow Ni..........Pia

Kiitikio
Ahh Internationally
I See Overtaking Wale
Najiona Mimi
Ahh I See My Sele I See Nobody Nobody Else
Najiona Mimi
Eeh Mungu Bwna Nifanyie Wepesi

I See Me International
I See Me Overtaking Wale
Najiona Mimi Eeh*2

>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>
Powered by Blogger.