Riwaya mpya ya Kiswahili


riwaya yenyewe na pia ugeni na wizi wa utandawazi wenyewe. Katika Nagona kwa mfano, tunapata maneno kama ‘Ego’, ‘Id’, ‘Superego’, ‘Sphinx’, ‘Cogito’, ‘Causa’ ‘Ultima’, ‘Disciplina Voluntatis’, ‘De Anima’, ‘Politica’, ‘Metaphysica’, ‘De Poetica’, ‘Totem’, ‘Oedipus Complex’, ‘Neurosis’, ‘ashab’, ‘tabilin’ na ‘tafsir’. Katika Babu Alipofufuka tunaona maneno kama ‘Gangar Wa’azu’, ‘Doggy’, ‘Neo- Casino’, ‘Proteus’, ‘Limonsin’, ‘shoyu’, ‘sake’, ‘beetles’, ‘spring chicken’, ‘semaa wa twaa’, ‘FKK’, ‘CD-ROM’, ‘Mona Lisa’, ‘zerha’, ‘manekineko’. Katika Dunia Yao tunapata maneno kama ‘Muse’, ‘CD’, ‘video’, ‘TV’, ‘taj’widi’, ‘maulidi’, ‘kasida’, ‘C Licence’, ‘TX’, ‘chip’, ‘Hillman’, ‘Vauxhall’, ‘mamluki’, ‘The Aritos’, ‘New World Order’, ‘WTO’, ‘Globalisation’, ‘sanctions’, ‘RAP’, ‘Paradise’, ‘I Need to Know’, ‘fantastic’, ‘Skyscrapers’, ‘cloning’, ‘dialectics’, ‘Zeus’, ‘Mnemosyne’, 14 Neno lenyewe kama jina la mhusika mkuu ‘Ndi-‘ limemeguka, limevunjika. ‘Calliope’, ‘Clio’, ‘Erat’o’, ‘Euterpe Melpomene’, ‘Polyhymnia’, ‘Terpsichore’, ‘Thalia’, ‘Urania’ n.k. Katika kipengele hiki pia tunaingiza uvunjaji wa kanuni za kisarufi, kiutanzu na kiujumi katika matini ya baadhi ya riwaya za mwelekeo huu. Uvunjaji huu unalinganishwa na uvunjaji wa kanuni kadha katika jamii ambazo zilidhaniwa zimeshakita na zisingeweza kuvunjwa kamwe. Ni wazi kwamba katika Babu Alipofufuka na Dunia Yao kanuni za sarufi zinavunjwa makusudi kama tunavyoona katika Babu Alipofufuka...[u]wanja-wa-ndege-wa-kimataifa alisimama kujitayarisha kwa ufunguzi wa milango (uk.29) ... komputa alimwambia kwamba mkewe Bi. Kiluba alikuwa akimsubiri kumbi la chini (uk.67). Au katika Bina-Adamu tunagundua kauli kama ...[I]nasemwa kuwa ... (uk.35) ambayo imechukuliwa moja kwa moja kutokana na Kiingereza balada ya Kiswahili Inasemekana kuwa ... [W]anaamini kwamba ukoo wao ni tukufu (uk.38) badala ya Ukoo wao ni mtukufu ... [H]apana, labda ni kimo changu cha mtoto (uk.45) badala ya Hapana, labda kimo changu cha utoto ... Matumizi wa sanaahati15 – yaani namna ya kucheza na mwandiko wa maneno ili kutoa hisia fulani ya kimaana au ujumi ni njia nyingine ya matumizi ya lugha kuelezea hali na taathira za utandawizi katika baadhi ya riwaya hizi, hasa katika Babu Alipofufuka, Dunia Yao na Bina-Adamu. Katika Babu Alipofufuka ukosefu wa uaminifu na kigeugeu cha utandawazi wenyewe na viongozi wakuu wa nchi wanaoutekeleza kwa shauku, unaelezewa katika mabadiliko ya uherufi katika sura mbalimbali kama vile tunavyoona katika neno Proteus linavyochorwa kiwimawima, kimlalo (kiyombo), kimkolezo, kimfifio, kiudogo na kiukubwa. Kwenye Dunia Yao tunapata nambari 36 ya miaka ya uhuru wa Zanzibar inakolezwa makusudi ili msomaji atafakari mafanikio na mashindikano ya wakati wa baada ya uhuru wa miaka hiyo 36. Maneno Wewe na mimi (uk.20) yanatofautishwa kwa mkozesho na udogowesho kusisitiza ubinafsi na ule ukilamtu- na-lake wa siku hizi. Usichochote nao unasisitizwa katika mpromoko wa maneno cider na nonentity. Neno Superboyswawili linalosisitiza Umarekani na Urusi wakati wa vita baridi linatiliwa mkazo na mkolezo wa wino. Neno ilhamu linalosisitiza kuzuka kwa riwaya mpya katika wakati wa utandawazi na kuwepo mtindo wa riwaya ndani ya riwaya (metafiction) au uzungumziaji wa riwaya ndani ya riwaya hasa kujibu hoja ya baadhi ya wahakiki kwamba riwaya sharti ichukue mkondo wa uhalisia – limekozeshwa wino pia. Bina-Adamu inatumia mkolezo wa wino au/na yombo na herufi kubwa katika msisitizo wa baadhi ya maneno yake kama Njia ya UHALISIA, UMERO-JAPA, Gastarbeiter, Nurenibaga, daktari wa kifo, Osagyefo n.k. Muhimu sana katika mbinu hii ni jinsi inavyotofautisha sauti za wasimulizi na wahusika mbalimbali katika riwaya ambamo herufi wima, herufi mlalo au yombo na herufi yombo zilizokolezwa, zinatafautisha wasimulizi na wahusika mbalimbali katika riwaya hii. Pia mbinu ya kuingiza mtindo wa utanzu mwingine katika utanzu wa riwaya kama vile tunavyoona Kezilahabi anapojenga matini yenye mtiririko wa kitamthilia (wa mazungumzo na majibu) katika sura 8 (uk. 47-52) yote inayojadili ufisadi, ngono na ukandamizaji wa kisiasa ulivyotawala duniani. Pia mwandishi huyu anavyotumia ufupisho wa sura yenyewe kama vile sura ya 10 (uk. 62) ambayo ina aya nne ndogondogo tu. Kwa kweli, riwaya za Kezilahabi ni fupi mno, kwa kiasi cha Nagona kuwa na kurasa 62 na Mzingile 70. 15 Tafsiri ya graphicart Mbinu ya mkarara wa kauli na maneno teuzi ni muhimu pia katika matumizi ya lugha –mbinu inayorejelea utandawazi/utandawizi na kusisitiza baadhi ya matokeo yake ambayo msomaji anatakiwa ayape uzito katika kuyafikiri. Katika Nagona maneno ‘ukweli’, ‘mshumaa’, ‘vichaa’, ‘vicheko’, ‘ungamo kuu’, ‘ukimya’, ‘njia’, ‘barabara’, ‘mto’, ‘paa’, ‘ndege’, ‘mti’, ‘msitu’, ‘milima’, ‘mabonde’, ‘duara’, ‘vitabu’, ‘ukosefu wa watu’, ‘paka’, ‘mkombozi’, ‘ajali’, ‘ndoto’, ‘maluweluwe’, ‘uta’ na ‘mshale’ ni maneno yanayorudiwarudiwa kila wakati. Katika Mzingile ‘mwanga’, ‘karne’, ‘kichaa’, ‘mkombozi’, ‘safari’, ‘ndoto’, ‘mto’, ‘giza’, ‘mzee’ na ‘ukungu’ ni baadhi ya maneno yanayorejewa kila baada ya muda. Katika Babu Alipofufuka maneno ‘Proteus’, ‘Limonsin’, ‘Doggy’, ‘mzuka’, ‘Neocasino’, ‘kimya’ na ‘kompyuta’ ni maneno yanayotajwa sana. Katika Bina-Adamu maneno ‘Bina-Adamu’, ‘P.P’, ‘huntha’, ‘Wotan’, ‘mto’, ‘safari’, ‘njia’, ‘Fyura’, ‘Yanguis’, ‘utandawazi’, ‘global village’ na ‘wizi’ ndiyo yanayojitokeza sana. Lakini mbali na neno moja moja, baadhi ya kauli au picha zinazojengwa kwa maneno mengi ambazo hurudiwa tena na tena kama tunavyoona katika Babu Alipofufuka (uk.92, 96) kauli ya La, hatutaki, hata ikiwaje hatulali tena... na katika Bina-Adamu (uk.140, 148) picha ya kuwa Ulimwengu umekuwa kijiji kidogo siku hizi, mipaka haipo tena ... inarudiwa tena na tena ingawa kwa maneno mengine. Kauli ya Hii ndiyo bustani yao ya Eden inarejewa mara kadha (uk.64, 110). Pia katika kitabu hikihiki tunakuta kauli Sio sisi tu akina Churchill, ukoo wa Kaiser, ukoo wa Gaulle, kina Franco na muhimu zaidi P.P. anafanya hivyo! Huu ni ulimwengu wa uwongo... (uk.50, 51). Picha nyingine zinazorudiwarudiwa katika riwaya hii ni ile ya hofu, ujinga, wizi, ufisadi, unanganyi na unyang’anywaji. 4.0 Hitimisho Mjadala tuliouendeleza katika makala haya unarejelea na kuthibitisha tasnifu maarufu katika somo la fasihi; ile tasnifu inayosisitiza kwamba, kama maisha ya mwanadamu mwenyewe, fasihi nayo lazima ibadilike hasa wakati wa matukio makuu ya kutisha au kufurahisha kama utandawazi/utandawizi ambayo yanabadilisha kwa kiasi kikubwa, maisha ya watu wa jamii fulani. Kwa sababu lugha ni nyenzo ya msingi ya kubunia na kuwasilishia kazi ya fasihi, basi lugha haina budi kukidhi kimaumbo, kimiundo na kikazi, mahitaji ya kazi ya fasihi na mahitaji ya jamii yenyewe inayobadilika. Marejeo Bertoncini, Elena. (2002): When Grandfather Came to Life Again – S. A. Mohamed’s New Novel Beyond Realism – makala iliyotolewa kwenye Kongamano la Kiswahili, Bayreuth. Dittemer, Clarissa. (2002/2003): Said Ahmed Mohameds “Babu Alipofufuka” ein magischrealistischer Roman – Kazi Maalum kwa Somo la Riwaya Mpya ya Kiswahili, Sehemu ya Fasihi za Kiafrika kwa Lugha za Kiafrika, Chuokikuu cha Bayreuth. Gromov, M. D. (1998). Nagona and Mzingile – Novel, tale or Parabole? Katika Jarida la ‘Afrikanische Arbeitspapiere 55: Kiswahili Forum V’, uk.73-78. ____________. (2004). Post-modernistic Elements in Recent Kiswahili Novels. Katika ‘The Nairobi Journal of Literature: The Journal of the Department of Literature, University of Nairobi’, 2, uk.28-36. International Labour Force and Information Group. 1998. An Alternative View of Globalisation, ILRIG, Cape Town. Jauch, Herbert (ed.). (2001). Playing the Globalisation Game: The Implications of Economic Liberalisation for Namibia, Labour Resource and Research Institute (LaRRI) Windhoek. Kezilahabi, E. (1990). Nagona. Dar-es-salaam University Press. ___________. (1990). Mzingile. Dar-es-salaam University Press. Khamis, Said A.M. 1999. Defamiliarisation and Experimentation in the Kiswahili Novel: A Case Study of Kezilahabi’s Novel: Nagona. Hotuba isiyochapishwa ya kupokea uprofesa Chuo Kikuu cha Bayreuth (Inaugural lecture). ________________. (2001). Fabulation and Politics of the 90s in Kezilahabi’s Nagona. Katika Toleo la ‘African Languages Literature in the Political Context of the 1990s’. Bayreuth African Studies 56 (2001): 119-133. ________________. (2003). Fragmentation, Orality and Magic Realism in Kezilahabi’s Novel: Nagona. Katika ‘Nordic Journal of African Studies’ 12(1), uk.78-91. King’ei, Kitula. (2002). Fantasy and Realism in the Modern Kiswahili Novel: A Critical Look at Babu Alipofufuka by Said A. Mohamed – an unpublished literary review. Mkangi, Katama. (1995). Walenisi. East African Educational Publishers: Nairobi. Mkufya, W.E. (1999). Ziraili na Zirani. Hekima Publishers: Dar-es-salaam. Mohamed, Said A. (2001). Babu Alipofufuka. Jomo Kenyatta Foundation: Nairobi. ______________. (2005). Dunia Y ao (kitatolewa na Oxford University Press: Nairobi). _____________. (2005/2006). Mkamandume (kitatolewa na Longhorn (K) Ltd: Nairobi). Murray, A. 2000. Public Sector Restructuring in Namibia – Commercialisation, Privatisation and Outsourcing: Implication for Organised Labour, LaRRI, Windhoek. Nicol Bran (ed.) (2002). Postmodernism and the Contemporary Novel: A Reader, Edinburgh University Press. Offiong, Daniel A. (2001). Globalisation: Post-Neodependency and Poverty in Africa, Fourth Dimension Publishing Co.: Enugu Nigeria. Rettová Alena. 2004. Afrophone Philosophies: Possibilities and Practice – The Reflexion of Philosophical Influences in Euphrase Kezilahabi’s Nagona and Mzingile. Katika Jarida la ‘Kiswahili Forum’ 11, uk. 45-68. 
Robert, Shaaban. (1951). Kusadikika. Nelson: London. 
_____________. (1967). Kufikirika. East African Literature Bureau: Nairobi. Ruigrok W & R van Tulder. 1995. The Logic of International Restructuring, Routledge: London/New York. Topan,
 Farouk, (2002). Babu Alipofufuka by Said A. Mohamed – an unpublished literary review. Wamitila, K.W. (1991). Nagona and Mzingile: Kezilahabi’s Metaphysics. Katika Jarida la Kiswahili 54 la (TUKI), Chuokikuu cha Dar-es-salaam, uk. 62-67.
 ____________. (1997). Contemptus Mundi and Carpe Diem Motifs in Kezilahabi’s Works. Katika Jarida la Kiswahili 60 la (TUKI), Chuokikuu cha Dar-es-salaam, uk. 15-24. 
____________. (2002). Bina-Adamu. Phoenix Publishers, Nairobi.


Powered by Blogger.