MICHAKATO YA KIMOFOLOJIA INAVYOTUMIKA KUUNDA MANENO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI


MICHAKATO YA KIMOFOLOJIA INAVYOTUMIKA KUUNDA MANENO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI.

Mofolojia ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno. Vipashio hivyo vya lugha huitwa mofimu (Rubanza, 1996).
Mofolojia ni tawi la taaluma ya isimu ambalo huchunguza maumbo ya maneno na hususani: maumbo ya mofimu. (Mathews, 1974)
Hartman (1972) anasema kuwa mofolojia ni tawi la sarufi ambalo hushughuliia na uchunguzi na uchambuzi wa maumbo, fani na aina zao maneno yalivyo sasa pamoja na histori zao.
Mofolojia huchunguza mofimu na alomofu zake fulani na jinsi ambavyo hukaa pamoja kuunda maneno mbalimbali katika lugha zinamotumika (Richard na wenzake 1985).
Kwa ujumla, mofolojia ni tawi la isimu ambalo huchunguza maneno ya lugha fulani na aina zake za maneno hasa upande wa upangaji wa mofimu mbalimbali zitumikazo kwa ajili ya kuunda maneno. Pia wana taalamu mbalimbali wamefasili maana ya maneno kwa mitazamo mabalimbali kama ifuatavyo.
Tuki, (1970) Neno ni mkusanyiko wa sauti ambazo huweza kutamukika na kuandikwa kwa pamoja na kuleta maana.
Massamba na wenzake (2003) wanafasi neno kwa kutafasili maelezo ya Lynos (1968:194- 208) kuwa neno linawez kufafanuliwa katika misingi ya kiumbo sauti yaani kwa kuchunguza sauti zinazounda umbo zima, kiontografia kwa kuchunguza herufi zinazotumika katika kuliandaka umbo lake, kisarufi kwa kuchunguza kile kinachowakilishwa na umbo husika katika lugha.
Katika lugha ya Kiswahili, maumbo ya kimatamshi na ya kimaandishi huweza kuwakilisha umbo moja au maumbo kadhaa ya kisarufi. Mfano,  katika lugha ya Kiswahili kuna umbo la Kimaandishi kaa. Kisarufi umbo hili linawakilisha maumbo matatu yenye maana tofauti kama ifuatavyo.
Kaa- tendo la kuketi kitako
Kaa- aina ya samaki
Kaa- kipande cha ukuni chenye moto au kilichochomwa.
Kwa ujumla, neno ni sehemu ya lugha yenye kituo kidogo mbele na nyuma yake, au kwa maandishi ni jumla ya herufi zenye maana zilizotengwa kwa nafsi nyuma na mbele.
Maneno katika lugha ya Kiswahili huweza kuundwa kupitia michakato mbalimbali kama vile kimofolojia, na kifonolojia, kwa kutumia mchakato wa kimofolojia, neno huweza kuundwa kupita kanuni mbalimbali kama vile, udondoshaji, uyeyushaji, Muungano wa sauti, nazali kuathiri konsonanti, konsonanti kuathiri nazali, Ukaakaishaji, usilimishaji au usilimisho na mchato wa msinyao.
Katika mchakato wa udondoshaji, kiambishi awali m- ambacho huonekana katika umbo la nje la maneno kama mu- tu, mu- gonjwa, mu – kanda. Katika kanuni au mchakato huu wa undoshaji. Irabu “u” hudondoshwa pale inapofuatiwa na konsonanti halisi katika mpaka wa mofimu. Mfano.
Mu+ tu= mtu
Mu+ gonjwa= mgonjwa
Mu+ kanda= mkanda
Mu + guu = mguu
>>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>>>>>
Powered by Blogger.