AFYA KWANZA


FENESI.

   Kama ilivyo ada ni wasaha mwingine ambao tunamshukuru mungu kwa kutupa uzima na kukutana tena katika makala yetu ya kila siku.Tunapaswa kumshukuru mungu kwani bila yeye hakuna ambalo tunalifanya na kuwa sahihi
Leo nitakupeleka moja kwa moja kuona umuhimu wa tunda aina ya fenesi kiafya ya ndani na nje ya mwili.






Tunda la fenesi ni moja kati ya matunda yenye sukari kwa kiasi chake,ulaji wa 100g za fenesi hukupa karolizi 90 kutokana sukari aina ya fructose na sucrose zilizomo ndani ya tunda hili.Kutokana na ukweli kwamba matunda mengi huwa na virutubisho vingi vinavyofanana hasa vitamini C,utaona kazi nyingi za baadhi ya matunda pia hufanana.Tuangalie faida za tunda hili kiafya kama ilivyo kawaida yetu:

MAGONJWA YA MOYO.
Sababu mojawapo ya magonjwa ya moyo ni pamoja na sukari kuwepo kwa wingi ndani ya mzunguko wa damu hii husababisha kuongezeka kwa kasi ya usafirishaji wa damu na mapigo ya moyo (blood pressure).Hii hupunguzwa kutokana na tunda la fenesi kuwa na kiwango cha sukari ambayo husaidia kurekebisha sukari mwilini.Hata hivyo mafuta yapatikanayo ndani ya fenesi hayana lehemu,hivyo ni mafuta sahii kutumika na yana uwezo mkubwa wa kukabiliana na tatizo la pressure hasa ya kupanda.
 
HUTIBU TATIZO LA DAMU.
Uwepo wa potasium na baadhi ya madini kama folic acid ndani ya tunda hili husaidia kwa kiasi kikubwa kusulihisha suala la damu.Kwa kuwa na anti oxidant Fenesi husaidia kuondoa sumu mwilini na kukupunguzia kasi ya magonjwa ya kansa na kulipunguzia ini kazi nzito ya kupambana na sumu mwilini.

MIFUPA NA MENO.
Mifupa huwa dhaifu kutokana na umri,vyakula tunavyokula pamoja na maradhi lakini vyote hivyo huweza kuepukika kama utaamua kuanza leo afya lishe na tunda hili.Fenesi lina madini mengi ya magnesium na kalisium ambayo husaidia kwa kiasi fulani katika kuimarisha mifupa.Hata magonjwa ya meno hutibiwa kwa fenesi kwani lina kiwango kikubwa cha vitamini Cambayo hufanya kazi nzuri katika kuimarisha uimara wa meno.
 
HULINDA NGOZI.
Dawa sahihi ya ngozi zilizojikunja (kama za wazee) ni Fenesi,hii ni kutokana na kiasi kikubwa cha mafuta ambacho tunda hili kinacho ambacho husaidia katika kulainisha ngozi na kuipa muonekano mwaroro.Sio hadithi za dhahania bali ni ukweli kwamba mafuta ya ngozi yatokanayo na fenesi ndio yaliyothibitishwa kuwa mafuta bora kwa afya ya ngozi ya binadamu.Fenesi huipa ngozi mwonekano kama wa ngozi ya mtoto mdogo,hivyo kwa akina dada si vyema sana kuhangaika na vipodozi vyenye madhara na gharama kubwa bali ubadilishe mazoea na kuanza kutumia fenesi kwa uzuri wa ngozi yako.
 
UNG"AAVU WA MBONI ZA MACHO.
Kutokana na uwepo wa vitamini A ambayo kazi yake kubwa ni kuyafanya macho yawe na uwezo mzuri wa kuona,pia hupatikana ndani ya tunda hili nakufanya kuwa na kazi muhimu ambayo inahitajika kila siku kwani tatizo la macho kwa kiasi kikubwa huathiri mwenendo mzima wa maisha yetu ya kila siku.
      Ulaji wowote uliopitiliza ni hatari kwa afya yako hata kama kitu hicho kitakua na faida mara mia,unatakiwa kula kistaarabu na kwa kiasi na sio kwamba umejua kuna faida za kutumia chakula hicho ukatumia zaidi.Mchanganyo wa fenesi na vyakula vingine huleta sumu ndani ya mwili wako,kaa na taadhari
 ONYO: USIJARIBU KULA FENESI NA KUNYWA SODA YA COCOA-COLA KWA MFUATANO.
 Kufanya hivyo unahatarisha maisha yako kwa muda mchache sana,kwani mchanganyiko huo husababisha utengenezwaji wa sumu ifananayo na nyoka aina ya cobra.
Utafitii uliofanyika china umedhihirisha jambo hilo:
Powered by Blogger.