HISTORIA YA MUZIKI WA HIP HOP NA BONGO FLEVA NA JINSI UNAVYOONEKANA KUATHIRIWA ZAIDI NA WASHAIRI WA KIMAPOKEO KULIKO WANAUSASA



Ubeti 2
Najiona Mimi Na Mitasi To Mary Mary
Utu Ndo Kitu Changu Ni Hery Hery
Maksi Za Show Zangu Ni A Very Very
Natia Neno Halleluya Kwenye Hali Bery
Wametuacha Mbali Na Zao Serikali Wakiunda Magari
Serikali Yangu Bando Inaunda Leseni
Ndo Maana Najiona Mimi Juu Tu Nikiunda Top Ten
Na Amka Na Hangover Ya Hela Siamki Na Deni
Na Amka Na Hangover Ya Hasira Siamki Na Demu
Nakiri Hizi Ndoto Ka Ndoto Si Grammy,BET,MTV NA Channel O
Nawakilisha Daraja Mbili Na Ngalelo
Najiona Mimi Juu Mamileo
Mawazo Juu Ya Pesa Zangu Under My Pilo
Lord Jesus My Hero Ohhh
Naona Injili Ina Shilling Siingilii Kanisani Siitilii Maanani
Sigara Saratani Siingilii Madukani
Nishida Au Umaskinii Ndo Maana Kitaa Inaua
Sugar Mamy Hajuwi Kushika Mooo
Anajuwa Kushika Mua Utashika Hela Ama Dua

Kiitikio
Ahh Internationally
I See Overtaking Wale
Najiona Mimi
Ahh I See My Sele I See Nobody Nobody Else
Najiona Mimi
Eeh Mungu Bwna Nifanyie Wepesi

I See Me International
I See Me Overtaking Wale
Najiona Mimi Eeh*2

Ubeti 3 
I See Me International
I See Me Overtaking Walee
Ahh I See My Self I See Nobody Nobody Else
Napiga Goti Eeh Mungu Bwna Anifanyie Wepesi
Mwanzo Na Mwisho Si Niwe Alfa Na Omega Yes
Nalisha Neno Kwa Kila Rika Na Kila Ezi Ahhh
Mm Sio Jino Kwa Jino Nyoka Kwa Kisigino
Zima Ni Lako Neno Makini Joh uwa Simo
Ndoto Zangu Sio Zinoo
Molinge Sokoine All I Do Is Holla Up
All I Do Is Winning Najiona Kwenye Hella Mingi
Chap Chap Shule Mingi Kauli Yangu Mbiu Ni Kauli Kaa Kata Usikate Ringi
 

Tukiangalia shairi hili utaona kuwa msanii pia amezingatia matumizi ya vina, mathalani katika ubeti wa kwanza, vinajitokeza vina vya, mi, to,ko,zo,ia, katika ubeti wa pili vinajitokeza vina vya ri, ni,o na lo na ua, wakati katika ubeti wa tatu vinajitokeza vina vya e,si,no,mo,na ngi.
Aidha wasanii wengine, huandika mashairi yenye vina vya kati na mwisho vinavyofanana kama wanavyofanya wanajadi, Abedi (kashatajwa, uk. 5) anasema, baadhi ya watungaji (wanajadi) mwanaweka vina vya kati vya namna moja katika beti zote. Athari hii, pia tunaweza kuiona katika shairi lifuatalo kutoka kwa msanii Diamond katika wimbo wa My Nomber One;
Ubeti wa 1
Kwanza mapenzi safari, ujana ni maji ya moto
Walinenaga zamani...
Pili tumetoka mbali, matatizo changamoto
tu visa visa fulani...
tatu kidonda chako, kwangu maradhi
Mama tu usononekapo kwangu simanzi..x2
Kwa mahaba uliyonipa nimenogewa 
ni vurugu patashika punguza kidogo..
Na mengine kadharika toto si unanielewa?
Hapo hapo uliposhika...ukiongeza kidogo
mi mwenzako ntaumia

Tukiangalia ubeti huu, tutaona kuwa, katika kila kipande cha mstari cha kwanza ameweka vina vya kati vinavyolingana rejea silabi zilizokolezwa wino.

Aidha, Katika shairi hili, ubeti wa kwanza tunaona vina vya mi,to,ko na ia vimetumika wakati katika ubeti wa pili vina vya ri, ni mu, o,ni na ua hujitokeza na katika ubeti wa tatu vina vya no na ngi hujitokeza pia. Hawa ni wasanii wachache tulioamua kuwatumia kuonesha jinsi wanavyoonekana kutawaliwa na wanajadi hususani katika vipengele vya matumizi ya vina ama kwa hakika wasanii wengi wa muziki wa Hip Hop na bongo fleva wameathiliwa na utumiaji wa vina katika mashairi yao kama wanavyosisitiza wanajadi. Na wakati mwingine wasanii wa Hip Hop na Bongo Fleva huamua kutumia vifupisho ili mradi tu kuhakikisha kuwa vina vinapatikana katika tungo zao kama tunavyoweza kuona katika wimbo wa Mathematic wa Roma Mkatoliki hususani ubeti wa kwanza:
Nimeshatikisa nyavu mi ndo MVP,
Wanakimbia depo hapo nipo CCP,
Niliwapigisha kuruta kwata la JKT,
Nina kipaji mimi kushinda hata THT,
Nawapangisha foleni kama benki ya NMB,
Mi nemesoma PCM siyo PCB,
So hata tufungwe mimi ni Asernal siyo Man U,
Kibonde we ni member wa Loan Board au TCU,
Nchi imeuzwa vigogo wanatuita ATM,
Tuwakemee mafisadi wote wa CCM,
Kuvua gamba haiwasafishi mbele ya CUF,
CHADEMA mwone Makamba, JK kwa TFF,
Sihitaji dancer wala mapanga yale ya TMK,
Show zangu zangu longolongo zile za Y2K,
>>>>>INAENDELEA>>>>>>>>

Powered by Blogger.