FONETIKI AU UTAMKWAJI WA SAUTI-FONIMU ZA KISWAHILI SANIFU


Maana Ya Fonetiki 

Fonetiki ni taaluma inayojishughulisha na jinsi sauti yo yote inavyotolewa au inavyopatikana. Hii ni sayansi huru ambayo inatumia nadharia za sayansi halisi kama vile fizikia, uhandisi, baiolojia, nk. na kufaidi matokeo ya kiutafiti ya taaluma hizi. Mathalani, ili mwanafonetiki aelewe jinsi ala za sauti zinavyofanya kazi wakati wa utolewaji wa sauti, atafaidika na maelezo ya kibaiolojia kuhusu namna mfumo wa mwili wa mwanadamu unavyofanya kazi.

Mgulu, (2001:48) anadai: ‘ ... fonetiki ni moja tu, lakini fonolojia zipo nyingi kama lugha zenyewe zilivyo nyingi. Kwa mfano, hatuna fonetiki ya Kiingereza au fonetiki ya Kiswhili. Fonetiki ni fonetiki tu. Kwa upande mwingine, tuna fonolojia za lugha mbalimbali ambazo hutofautiana. Tunazo, kwa mfano,  fonolojia ya Kiswahili, fonolojia ya Kiingereza, fonolojia ya Kifaransa, fonolojia ya Kinyamwezi, fonolojia ya Kindendeule, nk.

Tunapozungumzia upatikanaji wa sauti za lugha za binadamu, tunafafanua jinsi sauti za lugha husika zinavyotamkwa katika bomba la sauti la mwanadamu. (Tazama Jedwali 3.5).Tunazibainisha ala, hususani alasogezi na alapahala husika katika kuitamka sauti husika. Alasogezi ni ile ala ambayo inaweza kujimudu wakati wa utamkwaji wa sauti husika. Alapahala au Ala-tuli ni ile ala ambayo haiwezi kujimudu wakati wa utamkwaji wa sauti husika. (Tazama Kielelezo 3.1). Ni alasogezi ambayo hujisogeza kwenye alapahala husika wakati wa utamkwaji wa sauti husika (Nchimbi, 1979).

3.2.2   Utamkwaji wa Sauti-Fonimu za Kiswahili
Ieleweke kwamba hewa itokayo kwenye chemba ya mapafu ambayo sisi sote twaitumia kwa kupumua ili tuishi, ndiyo hiyo hiyo itumikayo katika utamkwaji wa sauti za lugha za binadamu. Hewa hiyo itapitishwa kwenye chemba zilizomo katika bomba la sauti kwa mujibu wa sauti inayotarajiwa kutamkwa hadi nje ya bomba la sauti kwa kupitia chemba ya midomo au chemba ya pua



Hewa hiyo ikipitia chemba ya pua tu au chemba ya pua na chemba ya midomo, basi hisia za sauti itakayotamkwa zitakuwa za sauti-ng’ong’o. Alasogezi ya kidaka-tonge huwa imejishusha kutoka kwenye ukuta wa marakaraka (paroi pharangale) ili hewa hiyo ipate ku


Lakini hewa hiyo, isipopitia chemba ya pua, ikapitia chemba ya midomo tu hadi nje, basi hisia za sauti itakayotamkwa zitakuwa za sauti-sing’ong’o. Alasogezi ya kidaka-tonge huwa imejikweza na kujibandika kwenye ukuta wa marakaraka kitendo ambacho hakiruhusu hewa kupenya hadi kwenye chemba ya pua. (Tazama Kielelezo 3.4).


Tutaanza kufafanua utamkwaji wa sauti-fonimu-irabu za Kiswahili, ukifuatiwa na ufafanuzi wa utamkwaji wa sauti-fonimu-konsoni za Kiswahili. Ufafanuzi utafanywa kwa kuzingatia vigezo vin’ne, navyo ni:
(a)    utamkwaji ki-alapahala,        
(b)    utamkwaji ki-sampuli,
(c)    utamkwaji ki-ughuna,
(d)    utamkwaji ki-ung’ong’o na,  
(e)    msimamo wa midomo hususani kuhusu  utamkwaji wa fonimu-irabu.             

3.2.3   Utamkwaji wa Fonimu-Irabu-Mama za Lugha za Binadamu
Irabu-mama katika lugha zote za binadamu ni /i a u/ ambazo utamkwaji wake katika bomba la sauti unajitokeza kwenye alapahala ya burutio-gumu/kaakaa-gumu ikishirikiana na alasogezi ya ulimi-kati ki-alasogezi-pahala kama ilivyo kwenye Kielelezo 3.5.


Katika Kielelezo 3.5 alasogezi-pahala za irabu, irabu-mama /I/ inajidhihirisha kuwa ni ya juu-mbele wakati irabu-mama /U/ ni ya juu-nyuma. Irabu-mama /A/ ni ya chini-kati.

Vigezo vya kufafanulia matamshi ya irabu ni kama ifuwatavyo:

 (i)       Kwa Mujibu wa Alapahala:ni burutio-gumu; ama sehemu ya mbele, ama sehemu ya kati, ama sehemu ya nyuma ya burutio-gumu.

 (ii)      Kwa Mujibu wa Alasogezi: ni ulimi; ama sehemu ya mbele (ulimi-mbele), ama sehemu ya kati (ulimi-kati), ama sehemu ya nyuma ya ulimi (ulimi-nyuma).

(iii)     Kwa Mujibu wa Midomo: ni ama midomo-tandazi au midomo-futuzi.

(iv)      Kwa Mujibu wa Mpenyo: ni ama mpenyo-mwembamba, ama mpenyo-mwembamba-kiasi, ama mpenyo-mpana.

(v)       Kwa Mujibu wa Kidaka-Tonge: ni ama irabu-ng’ong’o ama irabu-sing’ong’o

(vi)      Kwa Mujibu wa Nyuzi za Sauti/Glota: ni ama irabu-ghuna ama irabu-sighuna.

3.2.4   Utamkwaji wa Fonimu-Irabu //i e a o u/
Fonimu-irabu za kiswahili sanifu ni /i e a o u/. Fonimu-irabu-mbele za kiswahili sanifu ni /a e i/ na fonimu-irabu-nyuma ni /a o u/. Fonimu-irabu na nusu-irabu-mbele /a e i j/.
           
Wakati wa utamkwaji wa fonimu-irabu-mbele / a e i /, alasogezi ya ulimi-kati hujikweza kuelekea kwenye alapahala ya burutio-gumu-mbele. Mpenyo unaofanyizwa kati ya alasogezi ya ulimi-kati na alapahala yake ya burutio-gumu-mbele ni mpana wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [a], ni mpana kidogo wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [e] na ni mwembamba wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [i].

Mpenyo huu wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [i] unapofanyizwa kuwa mwembamba zaidi , basi matamshi ya sauti-endelezi ya nusu-irabu [j] hudhihirika, yaani [a e i j]. Aidha, midomo hubakia tandazi (Nchimbi,1979). Alasogezi ya kidaka-tonge huwa imejikweza na kujibandika kwenye ukuta wa marakaraka kitendo ambacho hakiruhusu hewa kupenya hadi kwenye chemba ya pua. Hisia ya sauti inayosikika ni sauti-sing’ong’o.

Utamkwaji wa Fonimu-Irabu na Nusu-Irabu-Nyuma /a o u w/:Wakati wa utamkwaji wa fonimu-irabu-nyuma / a o u /, alasogezi ya ulimi-kati hujikweza kuelekea kwenye alapahala ya burutio-gumu-nyuma. Mpenyo unaofanyizwa kati ya alasogezi ya ulimi-kati na alapahala yake ya burutio-gumu-mbele ni mpana wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [a], ni mpana kidogo wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [o] na ni mwembamba wakati wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [u]. Aidha, alasogezi ya mdomo-chini na alapahala ya mdomo-juu hujifutua, na kwa hiyo, kufanyiza mpenyo aina ya mviringo.

Mpenyo huu wa matamshi ya sauti-endelezi ya irabu [u] unapofanyizwa kuwa mwembamba zaidi, basi matamshi ya sauti-endelezi ya nusu-irabu [w] hudhihirika, yaani [a o u w], na midomo hubakia futuzi. Alasogezi ya kidaka-tonge huwa imejikweza na kujibandika kwenye ukuta wa marakaraka kitendo ambacho hakiruhusu hewa kupenya hadi kwenye chemba ya pua. Hisia ya sauti inayosikika ni sauti-sing’ong’o.

Kielelezo 3.7:  Alasogezi-Pahala za Irabu na Nusu-Irabu za Burutio-Gumu-Nyuma na Midomo-Futuzi  [o u w]
Tija itokanayo na mfumo wa matamshi ya sauti-irabu za kiswahili sanifu: maelezo yanayotokana na (a) utamkwaji wa fonimu-irabu za burutio-gumu-mbele  [a  e i] na nusu-irabu [j] na (b) utamkwaji wa fonimu-irabu za burutio-gumu-nyuma  [ o u] na nusu-irabu [w], yanatuwezesha kufanyiza (i) Jedwali ya mfumo wa matamshi ya irabu za kiswahili sanifu [i e a o u], (ii) Tarapezi ya mfumo wa irabu za kiswahili sanifu [i e a o u], na (iii) Jedwali la mfumo wa matamshi ya nusu-irabu/konsoni za kiswahili sanifu [j w], kama ilivyo katika Jedwali 3.6.  

Jedwali 3.6:  Jedwali ya Mfumo wa Matamshi ya Irabu za Kiswahili Sanifu [i e a o u]


ALAPAHALA YA KITAMKWA


Burutio-gumu Mbele.
Burutio-Gumu Kati.
Burutio-Gumu Nyuma

MPENYO

i


u

UNG’ONG’O
Mwembamba
   (Juu)



Sing’ong’o
Mpana Kiasi
   (Kati)

e


o
Mpana
 (Chini)



a







Ulimi-kati mbele
Midomo-tandazi/sifutuzi
Ulimi-kati nyuma
Midomo-futuzi/sitandazi


ALASOGEZI YA KITAMKWA



Kielelezo 3.8: Tarapezi ya Mfumo wa Irabu za Kiswahili Sanifu [i e a o u]
Jedwali 3.7:  Jedwali ya Mfumo wa Matamshi ya Nusu-Irabu/Konsoni za Kiswahili Sanifu [j w]

MSIMAMO WA MIDOMO
ALAPAHALA YA KITAMKWA
UGHUNA
BURUTIO-GUMU
BURUTIO-LAINI
Midomo tandazi
J


Ghuna


Midomo futuzi

w



Ulimi-Kati                     Ulimi Nyuma


ALASOGEZI


  
ZOEZI

1.     Zitaje chemba (cavities) zinazolijenga bomba la sauti la mwanadamu.

2.     Zitaje alasogezi (articulators) zilizomo katika bomba la sauti la mwanadamu.

3.     Zitaje alapahala (places of articulation) zilizomo katika bomba la sauti la mwanadamu.

4.     (a)    Tofautisha matamshi ya irabu-mbele na irabu-nyuma.
(b)    Eleza tofauti kati ya matamshi ya irabu [i] na nusu-irabu [j], au irabu [u] na nusu-irabu [w].

5.     Eleza tofauti kati ya alasogezi na alapahala.

>>>>>>INAENDELEA>>>>>

Powered by Blogger.