Msamiati wa Walemavu

Haya ni majina yanayopewa watu waliolemaa sehemu mbalimbali za mwili. Kiungo cha mwili husemekana kwamba kimelemaa pale ambapo hakiwezi kufanya kazi yake vizuri kama inavyohitajika. Kwa mfano, macho yasiyoweza kuona chochote, miguu isiyoweza kutembea n.k.

Mifano

  1. bubu : ( dumb, mute ) 
    mtu asiyeweza kuongea
  2. chongo 
    mtu mwenye jicho moja
  3. gumba 
    mwenye nundu mgongoni
  4. kibogoyo 
    mtu asiye na meno
  5. kigugumizi 
    mtu mwenye shida ya kutamka maneno
  6. kilema 
    mtu aliyelemaa miguu na mikono - asiyeweza kutembea wala kushika chochote
  7. kipofu : ( blind ) 
    mtu asiyeweza kuona.
  8. kiwete 
    mtu aliyelemaa miguu. asiyeweza kutembea
  9. kiziwi : ( deaf ) 
    mtu asiyeweza kusikia.
  10. matege 
    mwenye miguu iliyopinda
  11. punguani 
    mtu asiyekuwa na akili timam
Powered by Blogger.