Msamiati wa Malipo

Msamiati wa Malipo



Haya ni majina ya malipo yanayotolewa kwa shughuli/haja mbalimbali.

Mifano

  1. ada : ( bill ) 
    malipo kwa mganga au hospitali
  2. fidia : ( fine, faini ) 
    malipo ya mtu baada ya kumkosea mwengine au kumtia gharama/hasara
  3. karo : ( fee ) 
    malipo kwa ajili ya mafunzo (shuleni)
  4. kiingilio : ( entry fee ) 
    malipo yanayotozwa watu ili kushiriki katika jambo fulani
  5. kiinua mgongo : ( tip ) 
    malipo anayotoa mtu kama shukrani kwa jambo alilotendewa au analotaka kutendewa
  6. kodi : ( rent ) 
    malipo kwa kutumia nyumba au kiwanja. aghalabu hulipwa kila mwezi.
  7. marupurupu : ( allowances ) 
    pesa za matumizi ya kila siku
  8. mtaji : ( capital ) 
    pesa ambazo mtu huhitaji ili kuanzisha biashara
  9. nauli : ( fare, ticket ) 
    malipo ya kusafiri
  10. riba : ( interest ) 
    pesa zaidi mtu anazopata kwa kuweka pesa kwenye banki kwa muda fulani au malipo zaidi mtu anayohitajika kulipa juu ya kiasi alichochukua kama mkopo.
  11. rushwa : ( hongo ) 
    malipo yanayolipwa kinyume cha sheria ili kumfanya mtu akupendelee katika jambo fulani.
  12. ushuru : ( tax ) 
    malipo kwa serikali
Powered by Blogger.