Haya ni majina ya malipo yanayotolewa kwa shughuli/haja mbalimbali.
Mifano
- ada : ( bill )
malipo kwa mganga au hospitali
- fidia : ( fine, faini )
malipo ya mtu baada ya kumkosea mwengine au kumtia gharama/hasara
- karo : ( fee )
malipo kwa ajili ya mafunzo (shuleni)
- kiingilio : ( entry fee )
malipo yanayotozwa watu ili kushiriki katika jambo fulani
- kiinua mgongo : ( tip )
malipo anayotoa mtu kama shukrani kwa jambo alilotendewa au analotaka kutendewa
- kodi : ( rent )
malipo kwa kutumia nyumba au kiwanja. aghalabu hulipwa kila mwezi.
- marupurupu : ( allowances )
pesa za matumizi ya kila siku
- mtaji : ( capital )
pesa ambazo mtu huhitaji ili kuanzisha biashara
- nauli : ( fare, ticket )
malipo ya kusafiri
- riba : ( interest )
pesa zaidi mtu anazopata kwa kuweka pesa kwenye banki kwa muda fulani au malipo zaidi mtu anayohitajika kulipa juu ya kiasi alichochukua kama mkopo.
- rushwa : ( hongo )
malipo yanayolipwa kinyume cha sheria ili kumfanya mtu akupendelee katika jambo fulani.
- ushuru : ( tax )
malipo kwa serikali