Penny Apangua Tetesi za Kupata Mrithi wa Diamond, Asema Mabusu Anayopigwa na Sweddy na Kushikwa Kiuno ni Kawaida


Aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Diamond Platinumz, Penniel Mungilwa ‘Penny’ ameonekana kuwa karibu na kijana aitwae Sweddy, hali iliyoibua maswali mengi kwa mashabiki wake kuwa huenda ndo mrithi wa Diamond.

Baada ya gazeti la Ijumaa march 9 kuandika kuwa Penny amepata mrithi wa Diamond, Bongo5 iliamua kuwatafuta wote wawili Penny na Sweddy na kuzungumza nao kuhusiana na uvumi huo.

Penny ameiambia Bongo5, kuwa karibu na kijana huyo haimaanishi kuwa ni mpenzi wake.

Hahahahaha hah yakawaida haya mabusu,” alisema Penny, sisi ni washikaji, Sweddy namjua toka akiwa mdogo ndo maana unaniona naye kila sehemu,” alimalizia huku alicheka Penny.

Sweddy naye alisema kuwa Penny ni mshikaji wake huku akidai kumpiga mabusu hata hadharani ni kawaida yake na wameshazoea.

Penny ni mshikaji wangu wa muda sana, mimi nina demu wangu na yeye anajua kila kitu, haya mabusu yakawaida tu, tumeshazoea,” alisema Sweddy huku akicheka.
Powered by Blogger.