Watuhumiwa 40 wa mauaji ya tembo wakamatwa huku wengine wakiwekwa chini ya uangalizi maalum.


Kikosi kazi,maalumu kilichoundwa na serikali, kufuatilia mwenendo wa mtandao  wa  ujangili nchini kimefanikiwa kuwakamata watuhumumiwa muhimu zaidi ya 40 na kuwaweka  wengine chini ya uangalizi maalum, baada  ya  kuanza  kwa  operesheni hiyo  mwaka  2013
Mratibu wa kikosi hicho  katika eneo la ikolojia ya Serengeti,ambaye pia  ni mkuu wa kitengo cha kupambana na ujangili wa mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro (NCAA)Bw.Robert Mande amewaambia waandishi wa chama cha wanahabari za maliasili na utalii(TJT) kuwa hayo ni matokeo ya ushirikiano wa vikosi vya kuzuia ujangili,katika mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro hifadhi ya Serengeti,Manyara na Tarangire. 
Bw.Mande amesema tayari baadhi ya watuhumiwa wamefikishwa mahakamani na kazi ya kufatilia mtandao huo inaendelea licha ya  kukabiliwa na changamoto nyingi zinazotokana na ukubwa na uzito walinao watuhumiwa wa mtandao huo.
 
Uchunguzi ulioshirikisha makundi  mbalimbali wakiwemo wananchi wanaoishi jirani  umeonyesha kuwa mtandao huo unajumuisha watu wa ngazi mbali mbali wakiwemo wataalam kuua  tembo na kutoa meno kwa mudamfupi,madalali,na wamekuwa wakipewa mikopo yamagari, silaha na mahitaji mengine ya kufanya ujangili ili kufanikisha kazi hizo na kutoa  rushwa kwa  baadhi ya watendaji wanaojaribu kukwamisha kazi yao.
 
Kaimu meneja wa idara ya utalii wa mamlaka ya Ngorongoro Bw.Asanaeli Merita, amesema  changamoto ya ujangili uliokuwa umeshika kasi hivi  karibuni kwa upande mwingine  imeongeza chachu  ya udhibiti na umakini kwa kila idara na baadhi ya matokeo  yameonekana  yakiwemo  kuongezeka  kwa  mapato.
 
Kati ya mwaka 2013 na 2014 Tanzania ilikumbwa na wimbi kubwa la ujangili hasa wa  meno ya tembo ambao licha ya kwamba kwa sasa umedhibitiwa ulitishia uwepo wa  wanyama  hao  na pia uchumi wa tanzania ambao kwa kiasi kikubwa unategemea sekta  ya  utaliii.
 
Powered by Blogger.