Wanamichezo wanaoutaka ubunge mwaka huu

Wakati vuguvugu la uchaguzi mkuu wa mwaka huu likiendelea nchini, Tasnia ya michezo nayo imeanza kupata msukumo kwa wanamichezo kujitosa katika kinyang’anyiro hicho kwenye uchaguzi utakaofanyika baadaye mwaka huu.
Tayari wanafamilia wa michezo wanne, wametangaza nia ya kuhakikisha wanachukua majimbo kwenye uchaguzi huo kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Wanamichezo hao ni: Wilhelm Gidabuday (anagombea kupitia Chadema)

 

 Bondia Mada Maugo
 Huyu ana kumbukumbu nzuri katika tasnia ya michezo hasa riadha kwani alikuwa mstari wa mbele kukosoa maandalizi waliyopewa wanariadha wa Tanzania walioshiriki michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka jana nchini Scotland.
Gidabuday amejitosa kuwania ubunge wa Jimbo la Hanang kwa tiketi ya Chadema, jimbo linaloshikiliwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu, Mary Nagu wa CCM.
“Kwa kuamini kwamba kugombea nafasi yoyote ni haki ya msingi kikatiba, mimi kabla ya kujitathmini mwenyewe nimefanyiwa tathmini na watu wa rika tofauti ndani ya jamii, makundi hayo yakiwakilisha watu wenye busara katika jamii na kuniweka katika orodha ya watu wenye sifa stahiki,” anasema Gidabuday.
Ataitetea michezo bungeni
“Wananchi wa Hanang pia wameridhishwa na harakati zangu za kutetea wanamichezo, hususan riadha kitaifa, Watanzania wengi wananifahamu kwa jina la (mwanaharakati wa michezo Tanzania). Harakati zangu michezoni zimenifanya kuaminiwa na wadau wa michezo kote Tanzania,” anasema Gidabuday.
“Sheria namba 12 ya Baraza la Michezo Tanzania (BMT) ya mwaka 1967 licha ya kukosa meno, lakini pia imedharauliwa na viongozi wa wizara, BMT wenyewe na taasisi zilizokusudiwa kusimamiwa na sheria hiyo, na matokeo ya udhaifu huo umesababisha ufisadi ndani ya vyama vya michezo, ndiyo maana Tanzania tumekuwa watalii katika viwanja vya michezo kimataifa.
 Ili kuondoa hali hiyo nitatoa hoja binafsi sheria hii ibadilike sambamba na kuikumbusha Serikali umuhimu wa kuwa na kijiji cha michezo,” anasema Gidabuday.
Mada Maugo (anagombea kupitia Chadema)
Bondia huyu anajitosa kwa mara ya kwanza kuwania ubunge wa Jimbo la Rorya kwa tiketi ya Chadema, jimbo hilo sasa linaongozwa na Lameck Airo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Powered by Blogger.