Tanzania mwenyeji wa Jukwaa la vijana Afrika na China


Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (UVCCM ) ,Sixtus Raphael Mapunda
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete anatarajiwa kuzindua Jukwaa la kimataifa la  vijana kutoka nchi 43 za Africa na China lenye  lengo la kudumisha urafiki ,ushirikiano wa kimaendeleo  katika Nyanja za kiuchumi ,kijamii na kisiasa.
Mkutano wa Jukwaa hilo ambalo Tanzania ni mwenyeji wake  utahusisha pia vyama vya siasa 57, wafanyabiashara vijana 32 ambao kwa pamoja watajadili ushirikiano kati ya China na bara la Afrika katika kuleta maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa (UVCCM ) ,Sixtus Raphael Mapunda amesema jukwaa hilo litafanyika kuanzia machi 27 hadi 31 mwaka huu katika ukumbi wa Hoteli ya Ngurudoto Mkoani Arusha
“Tunatarajia kupokea ugeni mkubwa wakati wa mkutano wa jukwa hili,  nchi 43 kutoka Afrika zitahudhuria, vyama vya siasa  57 vitashiriki pia kutakuwa na wafanyabiashara vijana 32 kutoka nchi mbalimbali za Africa.
Amesema Tanzania itawakilishwa na  vijana 70 na vijana wengine 50 watatoka nchini China ambapo lengo kuu ni kujadili fursa zilizopo  na jinsi ya kuzifikia kwa ajili ya maendeleo ya Vijana wa Africa ikiwa ni pamoja na kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza Afrika.
Mapunda ameongeza  kuwa hii ni mara ya tatu ya kufanyika kwa mkutano wa jukwaa hilo  ambapo mara ya kwanza lilifanyiak mwaka 2011 katika mji wa Windhoek nchini Namibia na kufuatiwa mwaka 2012 Beijing China ambapo  walijadili uhusiano wa fursa katika  biashara utumike kwa maendeleo.
Amesema  kuwa  jukwaa hilo litajadili maendeleo ya mahusiano kati ya Africa na China ,ushiriki uhusiano wa vijana katika maendeleo  na wajibu wa asasi zisizo kuwa za kiserikali katika kukuza mahusiano na  maendeleo kati ya china na Africa.
Aidha amesema mgeni rasmi katika ufunguzi wa jukwaa hilo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dr.Jakaya Kikwete ambapo ataambatana na Waziri wa mambo ya ndani wa China, Waziri wa Biashara na Viwanda, Dk Abdallah Kigoda na Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene
Powered by Blogger.