Sadiki alia na wezi wa maji Dar


 
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said meck Sadiki akishiriki katika kupanda miti katika chanzo cha maji mtaa wa Mangolandege kata ya ukonga, Manispaa ya Ilala. Picha na Eunice Laurian 
KATIKA kuelekea kilele cha maadhimisho  ya siku ya maji Duniani, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki amesema Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka inatarajia kuanza kuzalisha maji kiasi cha lita 710milioni zaidi ya mahitaji ya sasa ambayo ni lita 450milioni ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
Akizungumza leo na waandishi wa habari kuhusu namna Serikali itakavyoshiriki maadhimisho hayo, Sadick amesema pamoja na kuwepo kwa changamoto kama vile uhaba wa vyanzo vya maji, Ukame, uchafunzi wa vyanzo vya maji pamoja na wizi wa maji Serikali imeendelea kubuni mbinu mbadala wa kukabiliana na changamoto hizo.
Amesema Upanuzi wa mitambo ya Ruvu juu na Ruvu chini, uchimbaji wa visima virefu vya maji , ujenzi wa bwawa la Kidunda na upanuzi wa mifumo ya majisafi na majitaka ni moja ya mikakati ya kuhakikisha kuwa malengo ya kuzalisha maji kwa kiwango kinachohitajiwa yanafikiwa.
“Mkoa wa Dar es Salaam unatekeleza jumla ya miradi 41 ya visima vya maji katika halmashauri zote, pia tunatekeleza miradi mingine 15 chini ya ufadhili wa Ubelgiji, miradi yote hii imebuniwa ili kuhakikisha kuwa zaidi ya wananchi 3.8 milioni wanapata maji safi na salama”, amesema Sadiki.
Amesema shughu za maadhimishi zimeanza leo kwa  kuelimisha  wananchi  kuhusu  sera  ya maji  ikiwa ni pamoja na kuzindua bomba la maji na kupanda miti katika mtaa wa Mongolandege Kata ya Ukonga Manispaa ya ilala, jiini  Dar-es-saalam.
Sadiki  ametoa wito kwa wananchi wa Dar es Salaam kutunza kulinda na kuheshimu miradi yote ya maji kwa kuzingatia kauli mbiu ya maadhimishi ya mwaka huu  ianyosema Maji kwa maendeleo endelevu
Amesema  miradi iliyo kamilika kwa sasa na iliyoanza  kutoa huduma ni miradi  14 ambayo ni  Ilala miradi 5 ya segerea  ugombolwa,pugu kimani  , Temeke miradi  5 ya  kijichi, kibonde majiB  na  Uwazi, Kinondoni  miradi  4 ya  Tandale, Mburahati na  Kwembe”
Amesema zaidi ya asilimia 50 ya maji yanayozalishwa kwa siku hupotea ama kuibiwa na watu wasiokuwa na mapenzi mema , hivyo aliziagiza mamlaka husika kuhakikisha kuwa inachukua hatua kali dhidi ya wale wote watakaobainika kuiba maji kwa njia moja ama nyingine.
Pamoja na hayo Sadiki aliitaka Dawasa kuhakikisha kuwa inakarabati mara kwa mara mifumom yake ya maji ili kupunguza kama si kumaliza kabia upotevu wa maji unaotokana na miundombinu iliyochakaa.
 Aidha  Sadiki  ametoa wito kwa wawekezaji kujitokeza na kuwekeza katika sekta hiyo kwani ni moja ya sekta muhimu kwa ustawi wa taifa.
Powered by Blogger.