Home / Mahusiano / KOSEA KUCHAGUA KILA KITU, LAKINI SIYO MWENZA-2 KOSEA KUCHAGUA KILA KITU, LAKINI SIYO MWENZA-2


Karibu mpenzi msomaji wangu katika safu hii ya mapenzi na maisha. Wiki iliyopita niliishia pale niliposema kwamba, ni dhahiri kwamba, katika uhusiano kila mmoja aliyemkubali mwenzake aliamua kutoka moyoni kwamba ndiye chaguo lake.

Nilisema kwamba, wengi walidiriki kugombana na ndugu zao, marafiki au hata kukejeliwa na jamii kwa sababu ya kuwa na uhusiano na mtu f’lani lakini kwa vile waliona ndiyo chaguo waliamua liwalo na liwe.
Watu wa kundi hili, inapotokea kuumizwa kimapenzi hulia sana kuliko mtu aliyefiwa. Kilio kikubwa kinatokana na kumbukumbu za kuonywa, kupoteza vitu au kuharibu uhusiano ili ampate ampendaye ambaye aliona ni chaguo lake.

Hulia sana kwa sababu aliamini huyo ndiye angekuwa mshauri mkuu katika maisha na angemzika au kumzika atakapomaliza safari ya maisha yake hapa duniani.
TUNAENDELEA TATIZO LIKO HAPA SASA
Unapompata mwenza ambaye kinyume na matarajio yako anakusaliti huku ukiwa unampenda kupita kiasi ndipo maumivu au kulizwa kunapotokea.

Lakini kwa kawaida, mwenza anapomliza mwenzake, kwa wakati ule huwa hajui kama maumivu yale yanaweza kuja kumtokea siku moja katika maisha yake.Wengi wanaposababisha wenza wao kulia wenyewe hujiona wapo sawa. Hawana tatizo na wala hawasababishi kilio chochote bali huenda hao wanaolia ni kwa kukosa kufikiri tu.
UTAFITI WANGU WA KINA NA KWELI
Mimi katika utafiti wangu wa kina na wa kweli, nimebaini kwamba, kila anayemsababishia mwenzake maumivu kwenye uhusiano, yeye akawa ‘komfotabo’ ni lazima siku moja na yeye atakuja kulizwa na mwingine. Iko hivyo!
Wapo wanawake, wanaume wameshawaliza wenzao kwa kuanzisha mahusiano mengine ambayo waliyaona ni bora na yaliyojaa starehe lakini baadaye wakaja kulizwa wao baada ya mategemeo yao kule kugonga mwamba.

NI VYEMA IKAWA HIVI


Powered by Blogger.