Majambazi wa nne sugu wamekamatwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za uporaji wa kutumia silaha,Morogoro.


Jeshi la polisi mkoa wa morogoro limefanikiwa kukamata majambazi sugu 4 risasi 20 na bastola moja kwa tuhuma za kuhusika na uporaji wa kutumia slaha  na wengine kupora  pochi  za wanawake na simu kwa kutumia pikipiki katika maeneo mbalimbali.
Kamanda wa polisi mkoa wa morogoro Leonardi Paulo amesema  mnamo februari 26 mwaka huu eneo la kilakala mjini morogoro kwenye geti la kampuni ya BH LADWA wakati kijana Bhayik Peter 26 akiwa na wenzake saba kwenye gari wakisubiri kufunguliwa geti ghafla majambazi walifyatua risasi hewani na kupora shilingi milioni 56 na hundi ya shilingi miloni tano na kutokomea kusikojulikana.
 
Katika hatua nyigine kamanda paulo amesema mnamo machi 26 eneo la nanenane mjini morogoro watu watatu wakiwa kwenye pikipiki walimgonga  kwa nyuma Mwanahawa Athuman29 akitokea kwenye kibanda cha huduma ya M-Pesa  wakitaka kumnyan’ganya pesa ambapo alipiga kelele kuomba msaada  wasamalia wema walifika katika eneo hilo na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja abubakari salum.
 
Watuhumiwa wote  watafikishwa  mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika na jeshi la polisi linaendelea na msako kuwakamata wale wote wanaojihusisha na uhalifu huo.
 
Powered by Blogger.