Wazee waandamana tanga kufuatia kunyang’anywa mashamba yao bila kulipwa fidia.

Wakazi zaidi ya 300 ambao wengi wao ni makundi ya wazee hasa akina mama wameiomba serikali kuingilia kati kufuatia mashamba yao waliyopewa na baba wa taifa hayati mwalimu jullius nyerere mwaka 1973 kunyang'anywa bila kulipwa fidia yeyote hatua ambayo imesababisha wazee hao kuishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa maisha yao.
Wakizungumza baada ya maandamano hayo  wazee hao wamesema maeneo hayo ya mwakidila walipewa kisheria na mwalimu nyerere na hakukuwa na hati yoyote yenye kuonesha kuwa wao hawana haki ya kufanya shughuli zao za kilimo katika eneo hilo na badala yake wameomba watafutiwe maeneo mengine kwanza ya kufanya shughuli zao badala ya kuwaondoa kwa nguvu kama vile sio raia wa Tanzania.
 
Hata hivyo baadhi ya viongozi wa wazee hao wameiomba serikali kuangalia suala hilo kwa jicho la huruma kwa sababu kama sheria za mipango miji zinawabana na kuwataka kuondoka katika eneo la''mwakidila kwa ramsingi'' wao wangeanza kupewa kipaumbele kwanza kwa kupimiwa maeneo ya ujenzi wa nyumba za kudumu badala ya kuwanyng'anya na kuwauzia wafanyabishara kutoka nje ya eneo hilo waliloishi kwa zaidi ya miaka miaka zaidi ya 50.
 
Kufuatia hatua maafisa mipango miji wa jiji la tanga wamesema kuwa wao hawawezi kulizungumzia suala hilo kwa sababu eneo hilo ni la jumuiya ya umoja wa vijana ccm mkoa wa tanga kama jinsi alivyonukuliwa mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa tanga Bwana. Salim Perembo  wakatiakizungumza kwa njia ya simu akiwa safarini kutoka mjini dodoma kurejea mkoani tanga.
 
Powered by Blogger.