Mtunzi hana thamani
Mtunzi hana thamani
WENZETU wamejaliwa, nchi kuwaridhia,
Mshairi kwa sanaa, kazi muhimu kupewa,
Na ofisi kuingia, ushairi kuandaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mtunzi huteuliwa, nafasi akachukua,
Mshairi namba moya, nchi ikamchagua,
Akatunga na kusia, nchi yanayosisimua,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Taifa humtambua, mashairi kuyalea,
Jamii yakaifaa, kwenye shibe na njaa,
Na watu kuwausia, yote yenye manufaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Uongo huushushua, na kweli kuing'amua,
Watu akawaongoa, na nchi kutengenea,
Amani ikaenea, na umoja kukomaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mshairi Tanzania, ni kichafu kitambaa,
Kamasi cha kutolea, kuishia kwenye jaa,
Hakuna anayemjua, walal kumsaidia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyuo vinaugua, kwa homa ya malaria,
Maruerue kujaa, jinamizi kaingia,
Nao watindikiwa, ushairi unavia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyuo vatindikiwa, ushairi umepwaya,
Washindwa kuitumia, sanaa kufundishia,
Wakawasha mshumaa, na fikra kuzagaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mengi wakayaibua, tungo na fikra pia,
Mawazo wakachimbua, nchi kujaa kufaa,
Chemchemi ikajaa, hekima kutopotea,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyombo vya habari baa, sanaa yanyanyapaa,
Ila vichache radhia, Radio tunazojua,
Vipindi huviandaa, malenga tukasikia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Magazeti nayo pia, ushairi yaonea,
Ukurasa yakataa, tungo kuzikubalia,
Machache hutokea, nafasi inapokuwa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Hakuna Mtanzania, wa kuhariri sheria,
Mashairi kuyajua, msasa akayatia,
Yeyote huchaguliwa, kazi hii akapewa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Televisheni balaa, sanaa hazijajua,
Muziki washikilia, hata tuchoke sikia,
Sasa ni kama kinyaa, kelele zinavyojaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Watunzi tuombe dua, watu macho kufungua,
Sanaa kuangalia, vizazi ikavifaa,
Isije ikajifia, na hazina kupotea,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mshairi kwa sanaa, kazi muhimu kupewa,
Na ofisi kuingia, ushairi kuandaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mtunzi huteuliwa, nafasi akachukua,
Mshairi namba moya, nchi ikamchagua,
Akatunga na kusia, nchi yanayosisimua,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Taifa humtambua, mashairi kuyalea,
Jamii yakaifaa, kwenye shibe na njaa,
Na watu kuwausia, yote yenye manufaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Uongo huushushua, na kweli kuing'amua,
Watu akawaongoa, na nchi kutengenea,
Amani ikaenea, na umoja kukomaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mshairi Tanzania, ni kichafu kitambaa,
Kamasi cha kutolea, kuishia kwenye jaa,
Hakuna anayemjua, walal kumsaidia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyuo vinaugua, kwa homa ya malaria,
Maruerue kujaa, jinamizi kaingia,
Nao watindikiwa, ushairi unavia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyuo vatindikiwa, ushairi umepwaya,
Washindwa kuitumia, sanaa kufundishia,
Wakawasha mshumaa, na fikra kuzagaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Mengi wakayaibua, tungo na fikra pia,
Mawazo wakachimbua, nchi kujaa kufaa,
Chemchemi ikajaa, hekima kutopotea,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Vyombo vya habari baa, sanaa yanyanyapaa,
Ila vichache radhia, Radio tunazojua,
Vipindi huviandaa, malenga tukasikia,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Magazeti nayo pia, ushairi yaonea,
Ukurasa yakataa, tungo kuzikubalia,
Machache hutokea, nafasi inapokuwa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Hakuna Mtanzania, wa kuhariri sheria,
Mashairi kuyajua, msasa akayatia,
Yeyote huchaguliwa, kazi hii akapewa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Televisheni balaa, sanaa hazijajua,
Muziki washikilia, hata tuchoke sikia,
Sasa ni kama kinyaa, kelele zinavyojaa,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !
Watunzi tuombe dua, watu macho kufungua,
Sanaa kuangalia, vizazi ikavifaa,
Isije ikajifia, na hazina kupotea,
Hathaminiwi mtunzi, hapa kwetu Tanzania !