Mchezaji afariki baada ya kupigwa kichwa

Mchezaji Franco Nieto aliyefariki baada ya kupiwa na jiwe kwenye kichwa wakati wa mechi nchini Argentina
Mchezaji wa Argentina Franco Nieto ,mwenye umri wa miaka 33 amefariki baada ya kupigwa kwenye kichwa wakati wa mechi siku ya jumamosi.
Nieto ,nahodha wa kilabu ya kijimbo ya Tiro federal alishambuliwa na genge baada ya mechi kati ya wapinzani wao wa jadi Chacarita Juniors katika mji wa Aimogasta kazkazini magharibi mwa Argentina.
Mechi hiyo ilisimamishwa kwa dakika 15 kabla ya kukamilika baada ya refa kuwapa kadi nyekundu wachezaji wanane kwa kupigana.
Mwaka huu watu 15 wamefariki katika ghasia zilizosababishwa na soka nchini Argentina,Binamu wa Nieto,Pablo Nieto amesema kuwa watu watatu walimzunguka mchezaji huyo alipokuwa akielekea katika gari lake na mkewe na mtoto wao wa mwezi mmoja.
Walimpiga kwa ngumi na mateke kabla ya mmoja ya watu hao kumpiga na jiwe katika kichwa na kumwacha bila fahamu.
Alifanyiwa upasuaji siku ya jumanne lakini akafariki siku ya jumatano.
Afisa mkuu wa polisi katika eneo hilo Fabian Bordon ameviambia vyombo vya habari kwamba watu watatu wamekamatwa kutokana na shambulizi hilo.
Ghasia zinazosababishwa na soka ni tatizo kubwa nchini Argentina.
Kulingana na shirika moja lilisokuwa la kiserikali Salvemos el Futbol,vifo vinavyosababishwa na ghasia za soka vimeongezeka mwaka huu.
Washukiwa wakuu ni genge la Barras Bravas ambao hudhibiti maneo ya kukalia katika viwanja vya mpira na barabara karibu na viwanja hivyo.
   chanzo;bbcswahili