CUF yasema Ukawa imeanza kuleta matumaini ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao.


CUF yasema Ukawa imeanza kuleta matumaini ya ushindi katika uchaguzi mkuu ujao.

 
Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Profesa Ibrahimu Lipumba amesema umoja wa vyama ulioundwa wakati wa mchakato wa katiba mpya marufu Ukawa umeanza kuleta matumaini ya kushinda katika uchaguzi mkuu ujao hapo mwakani baada ya kufanya vizuri katika uchaguzi wa serekali za mitaa ulio malizika hivi karibuni. 
Akizungumza kwenye mkutano wa hadahara ulio hudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi wa mkoa kaskazini Pemba kwenye uwanja wa Jadida wete amesema umoja huo umepata mafanikio makubwa licha ya kasoro nyingi zilizo jitokeza katika uchaguzi huo wa serekali za mitaa.
 
Kwa upandewake katibu mkuu wa chama hicho Malim Seif Sharif Hamad amesema ingawa uchaguzi huo niwamara ya kwanza lakini mungano huo wa vyama umeweza kuonyesha umoja na mshikamano na kuleta mafanikio. 
 
Mapema mwakilishi wa jimbo chakechake Omar Ali Shehe aliwataka wana chama wachama hicho kufata utaratibu ulio wekwa kwa masheha kuchukua vitambulisho vyao vya mazanzibar mkaazi iliwajiweke tayri kujiandikisha katika daftari lakudumu la wapiga kura nae makamo mwenyekitu wa CUF Juma Duni Haji amewataka wananchi kuhakikisha wanajiandisha ilikuweza kila moja wao kuwa mpiga kura.
 


Powered by Blogger.