Mmiliki wa meli za mizigo Mwanza aigomea serikali Kuondoa meli zake katika bandari tatu.


Mmiliki wa meli za mizigo Mwanza aigomea serikali Kuondoa meli zake katika bandari tatu.
Mmiliki wa meli nne za mizigo za kampuni ya Mkombozi Marine Fishing, Kitano Chacha ameigomea serikali kuondoa meli zake katika bandari namba tatu, iliyopo eneo la mwaloni kirumba jijini Mwanza linalodaiwa kumilikiwa na kampuni ya RS Pederson Transport tangu mwaka 1991 na kusababisha meli ya mizigo ya MV. Luxury iliyokuwa imebeba tani 150 za samaki kushindwa kutia nanga.
Licha ya kaimu mkuu wa wilaya ya Ilemela Baraka Konisaga, ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Nyamagana kutumia zaidi ya saa tatu kutafuta suluhu ya mgogoro baina ya mkurugenzi wa RS Pedersen Transport Ltd Richard Birikaa na mmiliki wa kampuni ya Mkombozi Marine Fishing kitana chacha kuanzia eneo la bandari namba tatu lililopo mwaloni kirumba hadi katika ofisi ya afisa mtendaji wa kata ya kirumba, kuhusu mwafaka wa meli ya MV. Luxury kutumia bandari hiyo kwa ajili ya kushusha na kupakia mizigo mbalimbali ya wafanyabiashara, Kitana Chacha amekataa katakata kuondoa meli zake.
 
Kauli ya mfanyabiashara huyo Kitana Chacha imemlazimu kaimu mkuu wa wilaya ya Ilemela Baraka Konisaga kutoa msimamo wa serikali.
 
Mgogoro huo wa kugombea eneo la ghati ambao umedumu kwa siku nne na kusababisha wananchi zaidi ya 300 kukosa ajira kwa muda katika bandari hiyo, umepelekea baadhi ya wafanyabiashara kupaaza sauti zao. 
 
Kuhusu madai kwamba jeshi la polisi mkoani Mwanza limewekwa mfukoni na mmiliki huyo wa kampuni ya Mkombozi Marine Fishing, kamanda wa polisi mkoani hapa kamishna msaidizi mwandamzi wa polisi Valentino Mlowola anasema
Powered by Blogger.