Mvua ya muda mfupi yaleta mafuriko jijini Dar es Salaam.


Mvua ya muda mfupi yaleta mafuriko jijini Dar es Salaam.
Mvua zilizonyesha kwa muda mfupi katika jiji la dar es Salaam zimesababisha mafuriko katika maeneo ya katikati ya jiji na kusababisha baadhi ya maduka kufungwa na magari kuzimika barabarani kutokana na kuingiwa na maji kulikotokana na tatizo sugu la miundombunu ya maji taka.
ITV imetembelea katika maeneo mbalimbali ya jiji hapo katika makutabo ya barabara ya Morogoro na Bibi titi imeshuhudiwa idadi kubwa ya maduka kufungwa kutokana na hofu ya kuingiliwa na maji yaliyokuwa yamefurika barabarani ambapo baadhi ya madereva wakilazimika kusukuma magari yao baada ya kuziba kutokana na kuingia maji huku watembea kwa wakilazika kupita kwenye maji hali inayoweza kuhatarisha afya zao. 
 
Wakizungumza na waandishi wa habari, baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameitaka serikali kutenga fedha na kuweka mikakati maalumu ili kuondoa kero sugu ya tatizo la miundombinu ya maji taka katika jiji la Dar es Salaam.
 
Aidha ITV imepita katika eneo la Jangwani na kukuta eneo maalumu ya ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi yaendayo haraka likiwa limezungu kwa maji ambapo baadhi ya wananchi wanaoishi maeneo hayo wameitaadharisha serikali mradi huo hautaweza kufanya kazi kama inavyokusudiwa hususani wakati wa mvua bila kuongeza kina cha daraja la mto msimbazi ili kuwezesha maji mengi kuelekea baharini.
Powered by Blogger.