Wahitimu wa chuo cha Must wapigiwa debe la ajira

Wahitimu wa chuo cha Must wapigiwa debe la ajira

 

Meneja wa mradi huo, Dk Danielle Pascallaqua kutoka Italia alisema vyuo vya Must, DIT na ATC kwa sasa vimepata vifaa vya kisasa vya kufundishia.

Mbeya. Wamiliki wa viwanda na kampuni nchini wameshauriwa kuwasiliana na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (Must) kama wanahitaji mafundi mchundo na wahandisi ili waweze kuwapata vijana wenye elimu sahihi.Naibu makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Osmund Kaunde alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na viongozi mbalimbali wa viwanda, taasisi na kampuni zilizoko mkoani hapa katika kikao maalumu kilichoandaliwa kwa ajili ya kuelezea umuhimu wa ushirikiano kati ya waajiri na vyuo vikuu nchini.
Profesa Kaunde alisema chuo chake kimeanzisha tovuti ambayo waajiri wanaweza kutangaza mahitaji ya watalaamu wanaowataka na tovuti hiyo itatoa fursa kwa wahitimu wenye sifa kuomba kazi.
“Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Tanzania na nchi ya Italia na unahusisha vyuo vitatu vya Must, Taasisi ya Ufundi Dar es Salaam (DIT) na Chuo cha Ufundi Arusha (ATC),” alisema.
Meneja wa mradi huo, Dk Danielle Pascallaqua kutoka Italia alisema vyuo vya Must, DIT na ATC kwa sasa vimepata vifaa vya kisasa vya kufundishia.
Naye mratibu wa kuhamasisha wasichana wasome masomo ya ufundi na uhandisi wa Must, Dk Lusajo Minga alisema mpango huo umeongeza idadi ya wasichana kutoka 11 mwaka 2005/06 hadi wasichana 269 kwa mwaka 2013/14.
Alisema wasichana hao wameonyesha umahiri katika masomo ya ufundi mchundo na uhandisi na wana uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi mahali popote duniani.
  chanzo;mwananchi


Powered by Blogger.