Mafuriko yaleta balaa Mwanza Share bookmark Print Email Rating

Mafuriko yaleta balaa Mwanza

Share bookmark Print Email Rating
Askari wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji akishuka baada ya kumuokoa mtoto eneo la Mabatini, jijini Mwanza lililokumbwa na mafuriko baada ya Mto Mirongo kufurika kutokana na mvua iliyonyesha jana. Picha na Michael Jamson 
Na Waandishi Wetu, Mwananchi

Posted  Jumatano,Decemba3  2014  saa 9:15 AM
Kwa ufupi
Mtendaji wa kata asema siyo makubwa kwa sababu hakuna mtu aliyefariki dunia.
SHARE THIS STORY
0
Share

Mwanza. Baadhi ya wakazi wa Kata ya Mbugani, Mtaa wa Mbugani A na B wameathiriwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha jana kwa saa nne.Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi hao walisema mvua hiyo imesababisha vitu vyao kusombwa na maji na nyumba kubomoka.
Esther Misanga, mkazi wa mtaa huo, alitaja baadhi ya vitu vilivyoharibiwa na mvua hiyo kuwa ni magunia 20 ya mahindi, magunia 10 ya daga na mifuko 20 ya unga wa sembe, vyote vikiwa na thamani ya jumla ya Sh2 milioni.
“Nimepoteza magunia 50 ya mahindi na unga wa dona. Nimepata hasara kubwa sana. Sikutegemea yangetokea mafuriko makubwa kama haya,” alisema Misanga.
Alisema Serikali iliwaahidi kuwahamisha maeneo hayo kutokana na kupata adha ya mafuriko ya mara kwa mara, lakini hadi sasa utekelezaji huo haujafanyika.
“Serikali ilituahidi kutupatia maeneo kule Kisesa, lakini tangu wazungumze hadi sasa mwaka umepita hawajatuonyesha maeneo hayo. Tunaiomba Serikali ifanye kila liwezekanalo ituhamishe katika eneo hili tunusuru maisha yetu,” alisema Misanga.
Akizungumza kwa simu, mtendaji wa Kata ya Mbungani, Baruani Hawadhi alisema maafa hayo siyo makubwa kwa kuwa hajapata taarifa za vifo vya watu zaidi ya uharibifu wa mali za watu.


w

KP Dec

Kp Nov
Kp Oct
Kp Sept
              source Mwananchi

Powered by Blogger.