Uchaguzi wa ubunge waanza Misri

Uchaguzi Misri
Uchaguzi wa ubunge ambao umesubiriwa kwa muda mrefu nchini Misri unaanza huku watu wakipiga kura katika balozi tofauti kote duniani.
Vituo vya kupigia kura nchini Misri vitafunguliwa siku ya jumatatu.
Kundi la Muslim Brotherhood lililoshinda uchaguzi wa ubunge miaka mitatu iliyopita kabla ya kupigwa marufuku halitashiriki uchaguzi huo.
Bunge jipya linatarajiwa kuwa na wabunge wengi wafuasi wa aliyekuwa mkuu wa majeshi Abdul Fattah al sisi ambaye alichukua madaraka mwaka 2013 na kuchaguliwa kuwa rais mwezi Mei mwaka uliopita.
bbcswahil
Powered by Blogger.