Siasa Paul Kagame anarudi Madarakani mwaka 2017? Hii hapa kutoka Mahakamani Rwanda..

Mahakama Kuu Rwanda imepokea Shauri kutoka Vyama vya Upinzani Rwanda ambavyo vinahitaji Rais Paul Kagame asigombee Urais kwa awamu nyingine tena baada ya kumaliza awamu mbili za kuiongoza Nchi hiyo.
Jopo la Majaji nane litajadili ishu hiyo, japo Serikali iliweka pingamizi Mahakamani kwamba kisijadiliwe chochote lakini jopo hilo linaloongozwa na Jaji Immaculee Nyirinkwaya lilitupilia mbali pingamizi hilo na Shauri litaendelea kusikilizwa Mahakamani September 23 2015.
Rwanda's President Paul Kagame attends the opening ceremony of the 24th Ordinary session of the Assembly of Heads of State and Government of the African Union (AU) at the African Union headquarters in Ethiopia's capital Addis Ababa, January 30, 2015. REUTERS/Tiksa Negeri
Rais wa Rwanda, Paul Kagame
Rais Kagame hakuwahi kutamka kama atagombea awamu ya tatu ya Urais au hapana, lakini kila alipoulizwa amekuwa akijibu kwamba hayo ni maamuzi ya Watu wa Rwanda wenyewe kumruhusu aendelee au hapana.
Kumekuwa na mvutano wa muda mrefu kuhusu ishu ya Katiba ya Rwanda kufanyiwa mabadiliko ili kumruhusu Kagame agombee tena Urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2017 lakini upande wa Upinzani wameonekana kutokubaliana kabisa na mapendekezo hayo.
gty_obama_ethiopia_presser_02_mm_150727_4x3_992
Rais Barack Obama alipokuwa Ethiopia July 2015.
Rais wa Marekani Barack Obama ni mmoja ya Viongozi ambao hawakubaliani na kitendo cha  Kiongozi yoyote kubadili Katiba ili aendelee kubaki Madarakani >>> ‘Nadhani mimi ni Rais bora kabisa, hata nikisema nigombee Urais wa Marekani kwa mara nyingine ninashinda… Hakuna mtu anatakiwa kuwa Rais milele, ni vizuri mkapeana nafasi na mwingine aje aongoze akiwa na mawazo mapya‘- Hii ni nukuu ya alichokisema Rais Obama akiwa kwenye ziara Ethiopia July 2015.
Powered by Blogger.