Filikunjombe, rubani makada CCM wafa katika ajali ya helikopta

Marehemu Deogratius Filikunjombe, aliyekuwa Mgombea ubunge jimbo la Ludewa kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
Mgombea ubunge jimbo la Ludewa kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Deogratius Filikunjombe, rubani na abiria wengine wote wamekufa baada ya helkopta kuanguka na kuteketea katika hifadhi Selou.
Jeshi la Polisi pamoja na Bunge limethibitisha leo mchana kutokea ajali hiyo mbaya na miili ya marehemu inasubiriwa uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katika ajali hiyo, Meya anayemaliza muda wake wilaya ya Ilala, Jerry Silaa amempoteza baba yake mzazi, William Silaa ambaye ndiye aliyekuwa akirusha helkopta hiyo iliyoanguka jana jioni.
Kabla ya vyombo hivyo viwili kuthibitisha kutokea vifo hivyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliiambia Mwananchi Digital kuwa ilikuwa inawawia vigumu kupata taarifa kutoka katika timu ya uokoaji kutokana na mazingira ya ajali kuleta utatanishi.
“Timu ya uokoaji inashughulikia suala hilo. Ila hatuwezi kusema iwapo wamefariki wote ama la kwa amana helkopta imeungua na pia ile ni mbuga, kuna wanyama wakali,” Waziri amesema.
Hata hivyo, katika kurasa za Twitter na Instagram za Meya Silaa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, January Makamba zilitoa rambirambi hata kabla ya Jeshi la Polisi kuthibitisha vifo katika hifadhi hiyo kubwa nchini.
-
Powered by Blogger.