Coastal Union kujiuliza kwa Kagera Sugar

Kagera Sugar
Dar es Salaam. Coastal Union haijawahi kushinda katika michezo sita iliyocheza hadi sasa na itabidi iingie uwanjani leo kusaka ushindi wake wa kwanza mbele ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga.
Mechi nyingine za leo za Ligi Kuu Tanzania Bara ni kati ya Prisons itakayokuwa ugenini kuikabili Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Ndanda watakuwa wenyeji wa Toto African kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, wakati Majimaji watacheza na African Sports kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Coastal Union inashika nafasi ya pili kutoka mkiani ikiwa na pointi tatu, lakini si tu haijawahi kushinda mechi yoyote, lakini haijawahi hata kufunga hata bao la kuotea tangu kuanza kwa Ligi Kuu Bara msimu huu.
Kinachofurahisha ni kuwa kati ya michezo sita iliyocheza Coastal Union, mitatu imecheza kwenye uwanja wake wa nyumbani wa CCM Mkwakwani na ndiyo hiyo iliyowapatia pointi tatu baada ya kutoka sare tatu, hivyo Mtibwa Sugar wanapaswa leo kujipanga kuwakabili.
Kocha wa Coastal, Union Jackson Mayanja aliliambia gazeti hili kuwa watahakikisha wanashinda mchezo wa leo ili kupata ushindi wao wa kwanza kwani wamechoka kuwa wasindikizaji tangu ligi ianze.
“Tunacheza nyumbani na Mtibwa, ni timu ngumu, kwani ipo nafasi za juu kwenye ligi, hivyo haitakuwa kazi rahisi, lazima tupambane hasa kuhakikisha tunashinda mchezo huo.
“Tangu tumeanza ligi tumekwenda kwa kusuasua, hivyo wachezaji wangu hawana budi kukomaa kesho (leo),” alisema Mayanja.

Powered by Blogger.