SWALI: Jadili uhusiano wa fasihi simulizi na fasihi andishi.


 
 
 
UTANGULIZI
Tangu kutawala kwa fasihi andishi Ulaya, Asia na kutumiwa na wenye nguvu za kisiasa na kiuchumi fasihi simulizi ilidharauliwa ikatwezwa, ikadunishwa na kushushwa hadhi huku fasihi andishi ikitukuzwa na kuendelezwa. Taaluma ya fasihi simulizi hivi leo inashughulikiwa kwa nguvu nyingi ili kuondokana na fikra duni zilizorithiwa toka kwa wataalamu wa kigeni kuwa sanaa kongwe ya fasihi simulizi ni ya kishenzi. Pamoja na dharau juu ya fasihi simulizi bado ukweli unabaki kuwa sanaa hii ndiyo ghala halisi la fasihi andishi. Hata sasa imebainika kuwa tenzi za Kigiriki zinazodaiwa kutungwa na manju aitwaye “Home” hazikuwa zimeandikwa kwa zaidi ya miaka miatano (500) ndipo baadaye zikaja kuhifadhiwa katika maandishi. Hivi majuzi pia wanateknolojia wameanza kukubali kuwa sehemu kubwa ya Biblia ni fasihi simulizi ya Wayahudi walioishi zama mbalimbali. Kimsingi fasihi simulizi na fasihi andishi ni kitu kimoja isipokuwa njia zinazotumiwa na fanani na hadhira katika kuwasilisha ujumbe.
KIINI
Fasihi simulizi na fasihi andishi zinahusiana katika vipengele mbalimbali kama ifuatavyo:
(i)              Fasihi simulizi huweza kuwasilishwa kupitia maandishi na fasihi andishi huweza kutumia ala za fasihi simulizi kunogesha kazi yake na kufikisha ujumbe wake. Hivyo maandishi sio kigezo cha kuitenganisha kabisa fasihi simulizi na fasihi andishi.
(ii)            Ukichunguza kazi mbalimbali za fasihi andishi utabaini kila mwandishi ameathiriwa na fasihi simulizi kwa namna fulani. Wapo walioathiriwa kifani na wengine kimaudhui.
(iii)          Zote mbili ni kazi za sanaa zinazotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa hadhira yake.
(iv)          Pili fasihi simulizi na fasihi andishi zote mbili zinaundwa kwa fani na maudhui
(v)            Zote ni kazi za kisanaa zitumiazo maneno teule kufikisha ujumbe
(vi)          Zote maudhui yake humhusu mwanadamu na maisha yake katika kumletea maendeleo katika Nyanja zote.
HITIMISHO

Fasihi simulizi na fasihi andishi ni sanaa za lugha zinazotofautiana njia za uwasilishaji tu lakini maudhui yake yanafanana.
Powered by Blogger.