MAANA NA WAKATI: JIFUNZE NAMNA MAANA ZA MANENO YA KISWAHILI ZINAVYOBADILIKA KULINGANA NA WAKATI

 
 
 MAANA NA WAKATI:
JIFUNZE NAMNA MAANA ZA MANENO YA KISWAHILI  ZINAVYOBADILIKA   KULINGANA NA WAKATI

Kisu-neno hili kwaa maana ya awali au sanifu ni kifaa kirefu kilichotengenezwa kwa chuma au bati kilicho bapa au chenye ncha kali upande mmoja, na matumizi yake makubwa ni kukatia vitu vinavyoshikika. Kwa mfano ‘’Naomba Kisu nikatie hii kamba’’.Lakini kwa maana ya sasa ambayo tunasema kudhoofika kwa maana ya msingi, neno Kisu linatumika kumaanisha msichana au binti mrembo kwa mfano; Salima ni Kisu mtaa mzima.Na mara nyingi neno hili hutumika sana na vijana hasa wanaoishi mjini.

Kiwembe-kwa maana ya zamani ni kifaa cha bapa chenye makali kotekote, lakini kutokana na neno hili kudhoofika kimaana sasa vijana na watu wazima wanaoishi maeneo ya mjini hutumia kumaanisha mtu ambaye hatulii kwenye mahusiano yake ya mapenzi yaani mtu asiyekuwa na mpenzi mmoja. Kwa mfano; Jackson ni kiwembe cha mtaa.

Mjomba-kwa maana ya awali Mjomba ni ndugu wa kiume wa mama au kaka wa mama lakini kutokana na kudhoofika kwa maana ya maneno sasa neno mjomba linatumika kumaanisha Polisi hususani wale wa barabarani,na hutumika sana na waendesha vyombo vya moto ambao ni makonda pamoja na madereva wao kwa mfano pindi wanapogundua mbele kuna Polisi husema “Funga mlango mbele kuna wajomba”.

Chombo-kwa maana ya msingi ni kitu chochote cha kufanyia kazi kwa mfano; katika muktadha wa nyumbani mama anaweza akasema “Mwanangu lete chombo cha kuwekea chakula” Lakini kwa sasa kutokana na kudhohofu kwa maaana ya neno, chombo hutumika kumaanisha msichana mrembo au mzuri kwa mfano; “Grace ni chombo” ikimaanisha Grace ni msichana mrembo.Na watu wanaotumia sana msamiati huu kwa maana hiyo ni vijana wa rika zote wanaoishi maeneo ya mjini.

Umeme-maana yake ya msingi ni nishati ya mwanga au miale inayotoa mwanga lakini kwa sasa neno umeme limepewa maana nyingine na wanajamii ambayo tunasema ni kudhohofika kwa maana, sasa umeme unaamaanisha Ugonjwa wa UKIMWI kwa mfano;”Miaka mitano sasa tangu Chande awe na umeme.” Wanachomaanisha vijana hapa ni kwamba tangu Chande kuathirika kwa UKIMWI ni miaka mitano.

Kifaa-kwa maana ya msingi ya neno kifaa ni kitu au chombo kinachotumika kufanyia kazi lakini kutokana na kudhohofu kwa maana ya neno kwa sasa neno kifaa hutumika kumaanisha msichana mrembo kwa vijana wa kiume lakini kwa upande wa vijana wa kike hulitumia kurejelea mwanaume hodari na mwenye juhudi kazini au katika kufanya mapenzi.kwa mfano “Hashimu ni kifaa kile” hapa wanawake ambao ni vijana humaanisha Hashimu ni mwanaume hodari wa mapenzi.

Kigodoro-kwa maana ya awali ni kipande kidogo cha godoro kwa mfano mtu anaweza kusema “Naomba kigodoro nifanye mto”, Lakini kwa maana ya sasa neno hili limedhohofu maana yake ya awali na kutumika kumaanisha sherehe za mtaani zinazoambatana na muziki unaokesha kwa mfano “Leo kuna kigodoro mtaa wa pili” Hapa wakazi wa mjini takribani wa rika zote wanaoishi mjini humaanisha kwamba mtaa wa pili kuna sherehe ambayo inakesha mpaka asubuhi.

Mlima-kwa maana ya awali neno hili linamaana ya kwamba sehemu ya ardhi iliyoinuka sana kwa mfano;”Chuo kikuu cha Dodoma kimejengwa kwenye milima” Lakini kutokana na neno mlima kudhohofu kimaana sasa vijana hususani wa kiume hutumia kumaanisha makalio makubwa ya mwanamke kwa mfano vijana hawa huweza kusema “Mlima wa Subira ni hatari” wakimaanisha Subira anamakalio makubwa sana.

Mashine-kwa maana ya awali neno hili linamaanisha kifaa au chombo kinachotoa nguvu ya kuendeshaa, Lakini kwa maana ya sasa ambayo ni zao la kudhohofu kwa maana ya neno sasa wanawake na vijana wa kike wanatumia msamiati huu kurejelea Kiungo cha uzazi cha mwanaume (uume).kwa mfano “Saidi anamashine kubwa” wakimaanisha kuwa Saidi anauume mkubwa.

Kipanga-kwa maana ya awali ni aina ya ndege mkubwa aina ya Tai ambaye huwa anakula wanyama na wadudu wadogo, Lakini kutokana na kudhohofu kwa maana sasa neno kipanga linatumika kumaanisha mtu mwenye akili nyingi darasani au sehemu ya kazi.Na neno hili linatumiwa zaidi na wanafunzi pamoja na walimu wao katika muktadha wa elimu.Kwa mfano “Elizabeth ni Kipanga kwa wanafunzi wa mwaka wa pili”.

Asali-maana ya msingi ni maji matamu mazito yanayotengenezwa na nyuki lakini kwa maana ya sasa ambayo ni kudhoohofu kwa maana ya neno watu ndani ya jamii wanalitumia neno asali kumaanisha mpenzi au mtu anayempenda kwa mfano; “Ester anasemaBryson ni asali wake”

Kamanda-kwa maana ya awali neno hili linamaanisha mkuu wa jeshi au polisi kwa mfano “Jenerali Mamnyange ni Kamanda wa jeshi la wananchi wa Tanzania” Lakini kwa sasa neno hili limedhohofu kimaana kwa vijana wengi wanalitumi kumaanisha rafiki wa karibu wa mtu hususani kwa vijana wa kiume kwa mfano “Naona kamanda umepumzika”.Hapa vijana hawamaanishi aliyepumzika ni mwanajeshi au polisi ila ni rafiki yake tu.

Ndezi-kwa maana ya awali ni mnyama wa mwituni mwenye umbo kama panya lakini ni mdogo kuliko paka.Ila kutokana na kudhohofu kwa maana sasa vijana wanalitumia neno ndezi kumaanisha mtu mzembe ndani ya jamii kwa mfano;”Mavula ni ndezi sana”

Nyoka-kwa maana ya awali ni mdudu mrefu mwembamba mwenye magamba asiye na miguu kwa mfano “Nyoka aina ya Moma ni mkali sana” Lakini kwa maana ya sasa ambayo kitaalamu tunasema ni kudhohofu kwa maana ya neno, Nyoka inatumika kumaanisha mtu msaliti au mnafiki na pia katika mkutadha wa migodini nyoka n wafanyakazi wanaoingia chini na kubeba vifurushi vya mchanga kuvitoa juu.

Chale-kwa maana ya awali ni alama au mkato anaokuwa nao mtu mwilini baada ya kuchanjwa na mganga kwa mfano;”Salome anachale nyingi mgongoni” Lakini kwa maana ya sasa kutokana na kudhoofu kwa maana inatumika kumaanisha mtu mwenye hisia za haraka kutambua au kuhisi vitu au hali hususani ya hatari,kwa mfano Jambazi ndeka anamachale sana hakamatwi na Polisi.

Mshikaki-kwa maana ya awali ni nyama iliyokatwa vipande vipande na kuchomekwa kwenye uchelewa au msumali kisha kuchomwa,kwa mfano “Jana nilinunua mshikaki na chipsi” Lakini kutokana na kudhohofu kwa maana sasa katika jamii neno hili linatumika kumaanisha ni mkao wa watu zaidi ya wawili kwenye pikipiki, kwa mfano: “Watu waliopanda mshikaki wamepata ajali mbaya”.

Msala-kwa maana ya awali ni mkeka mdogo unaotumiwa kusaliwa na watu wa dini ya kiislam hususani wanawake wakiwa nyumbani,kwa mfano; “Mama Abdul aliusafisha msala wake kabla ya kuanza kusali” Lakini kwa maana ya sasa kutokana na kudhohofu kwa maana neno msala linatumiwa na vijana kumaanisha jambo ambalo sio salama,jambo lenye matatizo au shida au kitu cha shari au hatari kwa mfano; “John kapelekwa kituo cha polisi kuna msala kafanya”.

Mzuka-kwa maana ya awali ni ni zimwi au pepo kwa mfano; “Swaumu amenisimulia hadithi ya mzuka” Lakini kwa maana ya sasa neno mzuka limepoteza hadhi yake kimaana kwani kwa sasa vijana wanalitumia kama ifuatavyo;kwenye muktadha wa salamu humaanisha ni shwari,salama,Amani kwa mfano; “mtu anapoulizwa unaonaje na hali hujibu mzuka yaani shwari au safi” lakini kwenye muktadha wa kawaida hutumika kumaanisha morari au mdadi wa kufanya kitu kwa mfano; “Leo sina mzuka wa kusoma” kwa maana kwamba leo hana morari au hamu ya kusoma.

Askari-kwa maana ya awali ni mtu anayelinda na kuhani Nchi kwa mfano “Julias ni askari wa Jeshi la polisi” lakini kwa maana ya sasa ambayo inaonyesha jinsi neno hili linavyodhohofika kimaana sasa vijana wanalitumia neno hili kama kijana yeyote mkakamavu na shupavu au jasiri kwa mfano “Bapipo ni askari wangu” kwa maana ya Bapipo ni jasiri au shupavu.Lakini pia neno hili hili vijana hulitumia kumaanisha rafiki  kwa mfano unaweza ukakuta kijana kawakuta wenzake wamekaa akitaka kuwasalimu utasikia anasema “Askari wangu vipi naona stori zimekolea” na wakati hakuna ambaye analinda au ni askari wa jeshi fulani, wote ni raia wa kawaida.

Chana-kwa maana ya kawaida neno hili linatumika kumaanisha kitendo cha kupasua kitu kama vile karatasi, nguo n.k kwa mfano; “Joyce anachana nguo” Lakini kutokana na maana ya neno hili kudhohofika sasa watu ndani ya jamii wanalitumia kumaanisha kitendo cha kuimba nyimbo au mashairi kwa kufokafoka kwa mfano; “Mr Blue anachana siku hizi” kwa maana ya kwamba siku hizi Msanii Mr Blue anaimba mashairi ya kufokafoka.

Mistari-kwa maana ya awali neno hili linatumika kuonesha muondelezo wa mchoro ulinyooka kwa mfano; “Mwalimu alisema kila mwanafunzi achore mstari mnyoofu” Lakini kwa maana ya sasa kutokana na kudhohofu kwa maana ya neno jamii inalitumia neno hili kurejelea mashari ya nyimbo kwa mfano; “Kama kweli wewe ni msanii tupe mistari”.

Ubao-kwa maana ya awali ni kwamba neno hili linatumika kumaanisha sehemu ya gogo au mti iliyopasuliwa vizuri lakini kwa sasa ndani ya jamii neno hli la ubao linatumika kumaanisha njaa yaani hali ya kuhisi njaa kwa mfano; “Jamani mimi ninaubao tutakula saa ngapi?”

Chonga-kwa maana ya awali neno hili linamaana ya kwamba ni kitendo cha kufanya ncha kwa kutumia chombo chenye makali kwa mfano; “Hamisi anachonga mshale kwa kutumia kisu” ila kwa sasa kutokana na kudhohofu kwa maana ya neno siku hizi neno hili wanajamii wanaalitumia kumaanisha kitendo cha mtu kuongea sana kwa mfano; “Janeth anachonga kama chiriku” kwa maana kwamba Janeth anaongea sana.

Uwawa-kwa maana ya awali neno hili linatumika kumaanisha kitendo cha kutolewa uhai kwa mfano “Mzee Rashidi ameuwawa jana usiku na majambazi” lakini kwa sasa neno hili limedhohofu maana yake ya awali kwani vijana analitumia kumaanisha hali ya mtu kutokuwa na pesa kwa mfano; “Hapa nilipo nimeuwawa namtafuta wa kunikopesha.”

Msenge-kwa maana ya awali linamaana ya mwanaume mwenye kufanyiwa vitendo vya kishoga au mwanaume hanithi lakini kwa jamii ya sasa hususani vijana wa kiume wanalitumia kumaanisha kijana yeyote wa kiume hata kama hana tabia hizo kwa mfano utawasikia vijana wengi katika maongezi yao wakisema “Yule msenge Bwire ni anajua huwa habahatishi” kwa maana Bwire ni kijana anayejua mambo kwa uhakika na wala sio shoga au hanithi.

Zege-kwa maana ya awali ni mchanganyiko wa kokoto,mchanga,saruji na maji ambayo hutumika katika kujengea kwa mfano; “Nyumba yetu imejengwa kwa msingi wa zege” lakini kutokana na kudhohofu kwa maana neno zege sasa linamaana ya chakula ambacho ni mchanganyiko wa  viazi mbatata na mayai(chipsi yai) kwa mfano; “Naomba zege mbili haraka” kwa maana kwamba anaomba chipsi yai.

Mende-kwa maana ya awali neno hili lina maana ya mdudu mwenye rangi ya kahawia mwenye mabawa na miguu mine ambao hupenda kukaa sana chooni kwa mfano; “Chooni kwao kuna mende wengi” lakini kwa sasa neno hili linatumika kumaanisha mtu ambaye ni mlevi wa pombe,kwa mfano; “Bokasa ni mende wa kijijini” kwa maana Bokasa ni mtu mlevi kijijini.

Ngano-kwa maana ya awali mmea aina ya nafaka unaotumika kutengenezea chakula lakini kwa sasa kwasababu ya kudhohofu kwa maana ya neno watu ndani ya jamii wanalitumia kumaanisha kilevi aina ya pombe hususani bia kwa mfano; “Usiku wa jana tulikula sana ngano” kwa maana usiku huo walikunywa sana pombe.

Fataki-kwa maana ya awali ni karatasi zilizotengenezwa na kutiwa baruti ndani ambazo hutumiwa mara nyingi kwenye sherehe kwa mfano; “Usiku wa mwaka mpya tulirusha fataki tatu” lakini kutokana na kudhohofu kwa maana ya neno sasa neno hili wanatumia kurejelea mwanaume mtu mzima anayetembea na wasichana wenye umri mdogo hususani wanafunzi wa shule kwa mfano; “Mzee Jangara ni Fataki”kwa maana kwamba Mzee Jangara anatembea na wasichana wadogo kama wajukuu zake au watoto wake.

Maji-kwa maana ya awali ni kwamba neno hili linamaanisha kiowevu kinachopatikana katika bahari, mvua au maziwa lakini kwa kudhohofu kwa maana ya neno watu ndani ya jamii wanalitumia neno hili kumaanisha Kilevi aina cha pombe kwa mfano; “Minja na Chibago wanapiga maji sio mchezo” hii inamana kwamba Minja na Chibago wanakunya sana pombe.

Bandua-kwa maana ya awali inamaana ni kitendo cha kutenganisha au kuachanisha vitu vilivyogandiana au ni kitendo cha kuondoa kitu kilichobandikwa kwa mfano; “Mama kasema nibandue magazeti yote ukutani” lakini kutokana na kudhohofu kwa maana ya neno sasa vijana wanalitumia neno bandua kumaanisha kitendo cha watu kufanya tendo la ndoa kwa mfano; “Hassan kambandua Sara usiku wa jana” kwa maana ya kwamba Hassan jana alifanya mapenzi na Sarah.

Ngoma-kwa maana ya awali ni ala ya muziki inayotengenezwa kwa kuwamba ngozi kwenye mzinga kwa mfano; “Ngoma zilipigwa kwenye harusi ya dada” lakini kwa maana ya sasa neno hili linatumika kumaanisha ugonjwa wa UKIMWI kwa mfano; “Bakari amekufa kwa ngoma”
Hii inamaana kuwa Bakari alifariki kwa ugonjwa wa UKIMWI.

Chemka-kwa maana ya awali ni hali ya kupata joto lakini kwa sasa neno hilo linatumika kumaanisha kitendo cha mtu kushinwa kufanya kitu kwa mfano; “Chausiku amechemka kufaulu mtihani” yaani Chausiku kashindwa kufaulu mtihani.

Msimbazi-kwa maana ya awali ni eneo linalopatikana jijini Dar es salaam maeneo ya kariakoo hususani eneo la kilabu ya simba na pia maeneo ya kigogo ambapo kuna kituo cha ufundi cha kanisa katoliki, lakini kwa sasa neno msimbazi hutumika kumaanaisha noti ya shilingi elfu kumi kwa mfano; “Fomu ya usajili inauzwa kwa msimbazi tu” kwa maana kwamba fomu hiyo inauzwa shilingi elfu kumi tu.

Bati-kwa maana ya awali inamaana ya bamba la chuma lenye mikunjokunjo kama matuta madogo hutumika kuezekea nyumba kwa mfano; “Baba kanunua bati hamsini kwa ajili ya kumalizia ujenza wa nyumba” lakini kwa sasa neno bati linatumika kumaanisha shilingi mia ya kitanzania ka mfano; “Kama unabati naomba ninunue nyembe” kwa maana kuwa anaomba shilingi mia anunue nyembe.

Kilo-kwa maana ya awali ni kwamba neno hili linatumika kumaanisha uzani wa kitu kwenye latini kwa mfano; “Dada ameagizwa mchele kilo mbili” lakini kwa maana ya sasa neno kilo linamaana ya shilingi laki moja za kitanzania kwa mfano; “Juzi nimeokota kilo nne” akiwa na maana kwamba Juzi ameokota shilingi laki nne za kitanzania.

Dongo-kwa maana ya awali ni sehemu ya udongo iliyomeguka lakini kwa sasa vijana wengi wa kiume na wa kike wanatumia neno dongo kumaanisha majungu au kejeli kwa mfano; “Deusi anapenda madongo sana” kwa maana kwamba Deusi anapenda kejeli au kuapiga majungu watu.

Kamba-kwa maana ya awali ni mnyama wa baharini mwenye magamba na miguu mingi ambaye huliwa kwa mfano; “Mzee Jongo mevua kamba wengi baharini” lakini kwa sasa neno hili linatumika kumaanisha kitendo cha kusema uongo kawa mfano; “Feizar ni mtu wa kamba” kwa maana Feizar ni mtu anaesema uongo.
Powered by Blogger.