SWALI: Fasihi simulizi siyo mali ya jamii nzima kama kale. Eleza

 
 
 SWALI: Fasihi simulizi siyo mali ya jamii nzima kama kale. Eleza

UTANGULIZI
Hapo kale fasihi simulizi ilipotendwa hadharani iligeuka kuwa mali ya jamii nzima. Ndiyo maana hatujawahi kusikia nani anamiliki methali hii ama wimbo huu nakadhalika. Fanani alipoitenda tu jamii nzima ilikuwa huru kuitoa na kuitumia pahala popote pale.
Zama hizi hali imebadilika, watu ama vituo mbalimbali vya habari na waimbaji mbalimbali huimba na kutangaza uhalali ama umiliki wa wimbo husika. Mtu yeyote anayeuchuku au kuutoa hata nakala aweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Sayansi na teknolojia imeiondoa fasihi simulizi kwenye dhana ya umiliki wa jamii nzima na kutuingiza katika mfumo wa kibepari ambapo sasa, fasihi simulizi ni mali ya mtu binafsi. Hali hii inatokana na sababu zifuatazo:

KIINI
Njia za uhifadhi wa fasihi simulizi kwa sasa zinahusisha matumizi makubwa ya zana za kisayansi na kiteknolojia ambazo ni ghali na hivyo msanii huingia gharama kubwa kuiandaa na kuikamilisha kazi ya fasihi Gharama hizo huifanya kazi hiyo inapokamilika kuwa mali ya yule aliyeingia gharama ambaye ni msanii.
Hali ya uchumi, kutokana na kushamiri kwa ubepari hivi sasa kila mtunzi anafanya hivyo akilenga kujipatia pesa kupitia ubunifu alionao, hali hii inaifanya fasihi simulizi kumilikiwa na mtunzi mwenyewe kutokana na kazi husika kuwa chanzo cha kipato kwa mtunzi.
Kuibuka kwa matabaka katika jamii nako kunachochea fasihi simulizi kuwa mali ya mtu binafsi kwa sababu wenye pesa hutumia nguvu yao kiuchumi kushawishi watunzi kutoa burudani kupitia fasihi na kasha kuwalipa, kuibuka kwa wasambazaji wa kazi za fasihi huchochea kuwepo kwa watunzi wengi wanaolenga pesa na hivyo kuzidisha umiliki binafsi wa fasihi simulizi.

HITIMISHO

Kwa ujumla umiliki wa fasihi simulizi kwa sasa umehama toka kwa jamii nzima hadi kwa mtunzi kutokana na maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia katika jamii na kushamiri kwa ubepari duniani hali inayochochea kutafuta pesa kuwa ndio kipaumbele.
Powered by Blogger.